< 1 Wakorintho 12 >

1 Kuhusu karama za rohoni, kaka na dada zangu sitaki mkose kufahamu.
Or, en ce qui concerne les choses spirituelles, frères, je ne veux pas que vous soyez ignorants.
2 Mwajua ya kuwa mlipokuwa wapagani mliongozwa kufuata sanamu zisizoongea, kwa njia zozote mliongozwa nazo.
Vous savez que, lorsque vous étiez païens, vous vous laissiez entraîner vers ces idoles muettes, quelle que soit la manière dont vous vous laissiez entraîner.
3 Kwa hiyo, nataka mfahamu kwamba hakuna yeyote anenaye kwa Roho wa Mungu akisema, “Yesu amelaaniwa.” Hakuna yeyote atakayesema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
C'est pourquoi je vous fais connaître que nul, parlant par l'Esprit de Dieu, ne dit: « Jésus est maudit. » Personne ne peut dire: « Jésus est Seigneur », si ce n'est par le Saint-Esprit.
4 Basi kuna karama tofauti tofauti, bali Roho ni yeye yule.
Il y a plusieurs sortes de dons, mais un seul et même Esprit.
5 Na kuna huduma tofauti tofauti, bali Bwana ni yeye yule.
Il y a diverses sortes de services, et le même Seigneur.
6 Na kuna aina mbalimbali za kazi, lakini Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
Il y a diverses sortes d'œuvres, mais le même Dieu qui opère toutes choses en tous.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
Mais à chacun est donnée la manifestation de l'Esprit pour le profit de tous.
8 Maana mtu mmoja amepewa na Roho neno la hekima, na mwingine neno la maarifa kwa Roho yule yule.
En effet, à l'un est donnée par l'Esprit la parole de sagesse, à un autre la parole de connaissance selon le même Esprit,
9 Kwa mwingine humpa imani kwa Roho yeye yule, na kwa mwingine karama ya uponyaji kwa Roho mmoja.
à un autre la foi par le même Esprit, à un autre le don des guérisons par le même Esprit,
10 Kwa mwingine matendo ya nguvu, na mwingine unabii. Na kwa mwingine uwezo wa kupambanua roho, mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingnine tafsiri za lugha.
à un autre l'action des miracles, à un autre la prophétie, à un autre le discernement des esprits, à un autre la diversité des langues, à un autre l'interprétation des langues.
11 Lakini Roho ni yule yule atendaye kazi hizi zote, kumpa kila mtu karama kwa kadiri ya uchaguzi wake mwenyewe.
Mais c'est un seul et même Esprit qui produit tout cela, distribuant à chacun séparément ce qu'il veut.
12 Kwa maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote ni vya mwili ule ule, vivyo hivyo na Kristo.
Car, comme le corps est un et a plusieurs membres, et que tous les membres du corps, étant nombreux, ne forment qu'un seul corps, ainsi en est-il de Christ.
13 Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi au Wayunani, kwamba tu watumwa au huru, na wote tulinyweshwa Roho mmoja.
Car c'est dans un seul Esprit que nous avons tous été baptisés pour former un seul corps, Juifs ou Grecs, esclaves ou libres, et que nous avons tous été abreuvés dans un seul Esprit.
14 Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi.
Car le corps n'est pas un seul membre, mais plusieurs.
15 Ikiwa mguu utasema, “kwa kuwa mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo haiufanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
Si le pied dit: « Je ne suis pas la main, je ne fais pas partie du corps », il ne fait donc pas partie du corps.
16 Na ikiwa sikio litasema, “kwa kuwa mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo hailifanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
Si l'oreille disait: « Parce que je ne suis pas l'œil, je ne fais pas partie du corps », elle ne ferait donc pas partie du corps.
17 Kama mwili wote utakuwa jicho, kungekuwa wapi kusikia? Kama mwili wote ukiwa sikio, kungekuwa wapi kunusa?
Si le corps tout entier était un œil, où serait l'ouïe? Si tout le corps était une ouïe, où serait l'odorat?
18 Lakini Mungu aliweka kila kiungo cha mwili mahali pake kama alivyopanga mwenyewe.
Mais maintenant, Dieu a placé les membres, chacun d'eux, dans le corps, comme il l'a voulu.
19 Na kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
S'ils étaient tous un seul membre, où serait le corps?
20 Hivyo sasa viungo ni vingi, lakini mwili ni mmoja.
Mais maintenant, ils sont plusieurs membres, mais un seul corps.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “sina haja na wewe.” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, sina haja na ninyi.”
L'œil ne peut pas dire à la main: « Je n'ai pas besoin de toi », ni la tête aux pieds: « Je n'ai pas besoin de toi. »
22 Lakini viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa na heshima kidogo vyahitajika zaidi.
Non, bien plutôt, les membres du corps qui semblent plus faibles sont nécessaires.
23 Na viungo vya mwili tunavyodhani vina heshima kidogo, twavipa heshima zaidi, na viungo vyetu visivyo na mvuto vina uzuri zaidi.
Les parties du corps qui nous paraissent moins honorables, nous les honorons plus abondamment; et nos parties non visibles ont plus de pudeur,
24 Na sasa viungo vyetu vilivyo na mvuto havina haja ya kupewa heshima, kwa kuwa tayari vina heshima. Lakini Mungu ameviunganisha viungo vyote pamoja, na amevipa heshima zaidi vile visivyo heshimiwa.
tandis que nos parties visibles n'en ont pas besoin. Mais Dieu a composé le corps ensemble, en donnant plus d'honneur à la partie inférieure,
25 Alifanya hivyo ili pasiwepo mgawanyiko katika mwili, bali viungo vyote vitunzane kwa upendo wa mmoja.
afin qu'il n'y ait pas de division dans le corps, mais que les membres aient le même soin les uns des autres.
26 Na wakati kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote vyaumia kwa pamoja. Au wakati kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vyote vifurahi kwa pamoja.
Si un membre souffre, tous les membres souffrent avec lui. Quand un membre est honoré, tous les membres se réjouissent avec lui.
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
Or, vous êtes le corps du Christ, et ses membres individuellement.
28 Na Mungu ameweka katika kanisa kwanza mitume, pili manabii, tatu waalimu, kisha wale wote watendao matendo makuu, kisha karama za uponyaji, wale wasaidiao, wale wafanyao kazi ya kuongoza, na wote walio na aina mbalimbali za lugha.
Dieu a établi certains dans l'assemblée: premièrement des apôtres, deuxièmement des prophètes, troisièmement des docteurs, puis des thaumaturges, puis des dons de guérison, d'assistance, de gouvernement et de langues diverses.
29 Je sisi sote ni mitume? Sisi sote ni manabii? Sisi sote ni waalimu? Je sisi sote tunafanya matendo ya miujiza?
Tous sont-ils apôtres? Sont-ils tous prophètes? Sont-ils tous des enseignants? Sont-ils tous des thaumaturges?
30 Je sisi sote tuna karama ya uponyaji? Sisi sote tunaongea kwa lugha? Sisi sote tunatafsiri lugha?
Ont-ils tous des dons de guérison? Parlent-ils tous en diverses langues? Tous interprètent-ils?
31 Tafuteni sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonesha njia iliyo bora zaidi.
Mais désirez ardemment les meilleurs dons. D'ailleurs, je vous montre une voie excellente.

< 1 Wakorintho 12 >