< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ni orodha ya familia za viongozi wa Israeli, wakuu wa maelfu na mamia, pamoja na maafisa wa jeshi walio mtumikia mfalme kwa namna tofauti. Kila kikosi cha jeshi kilitumika mwenzi hadi mwezi kwa mwaka mzima. Kila kikosi kilikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Och detta är förteckningen på Israels barn, efter deras antal med huvudmännen för deras familjer och med över- och underhövitsmännen och med deras tillsyningsmän vilka tjänade konungen i allt som rörde krigsfolkets avdelningar, vilka avdelningar kommo och avgingo skiftevis för var och en av årets alla månader, var avdelning tjugufyra tusen man stark.
2 Kwa mwezi wa kwanza wa kikosi alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Över den första avdelningen, den som tjänstgjorde under första månaden, hade Jasobeam, Sabdiels son, befälet. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
3 Alikuwa miongoni mwa uzao wa Perezi na mhusika wa maafisa wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
Han hörde till Peres' barn och var huvudanförare för alla härhövitsmän som tjänstgjorde under första månaden.
4 Juu ya kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai, wa ukoo wa uliotoka kwa Ahoa. Mikilothi alikuwa wa pili kwa cheo. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Över den andra månadens avdelning hade ahoaiten Dodai befälet, det var hans avdelning; där var ock fursten Miklot. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
5 Mkuu wa jeshi wa mwezi wa tatu alikuwa Benaia mwana wa Yehoiada, kuhani na kiongozi. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den tredje härhövitsmannen, den som tjänstgjorde under tredje månaden, var Benaja, prästen Jojadas son, såsom huvudanförare. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
6 Huyu ni Benaia aliye kuwa kiongozi wa wale thelathini na juu ya wale thelathini. Amizabadi mwanae alikuwa katika kikosi chake.
Denne Benaja var en hjälte bland de trettio och hade befälet över de trettio. Och vid hans avdelning var hans son Ammisabad.
7 Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu. Zebadia mwanae akawa mkuu baada yake. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Den fjärde, den som tjänstgjorde under fjärde månaden, var Asael, Joabs broder, och efter honom hans son Sebadja. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen
8 Mkuu kwa mwezi wa tano alikuwa Shamihuthi, mzao wa Izra. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den femte, den som tjänstgjorde under femte månaden, var hövitsmannen Samhut, jisraiten. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
9 Mkuu kwa mwezi wa sita alikuwa Ira mwana wa Ikeshi, kutoka Tekoa. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den sjätte, den som tjänstgjorde under sjätte månaden, var tekoaiten Ira, Ickes' son. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
10 Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den sjunde, den som tjänstgjorde under sjunde månaden, var peloniten Heles, av Efraims barn. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
11 Mkuu kwa mwezi wa nane alikuwa Sibekai Mhushathi, kutoka ukoo ulitoka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den åttonde, den som tjänstgjorde under åttonde månaden, var husatiten Sibbekai, som hörde till seraiterna. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
12 Mkuu kwa mwezi wa tisa alikuwa Abi Ezeri Manathothi, kutoka kwa kabila la Benjamini. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den nionde, den som tjänstgjorde under nionde månaden, var anatotiten Abieser, som hörde till benjaminiterna. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
13 Mkuu kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai kutoka mji wa Netofa, kutoka ukoo ulio toka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den tionde, den som tjänstgjorde under tionde månaden, var netofatiten Maherai, som hörde till seraiterna. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
14 Mkuu kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaia kutoka mji wa Pirathoni, kutoka kabila la Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den elfte, den som tjänstgjorde under elfte månaden, var pirgatoniten Benaja, av Efraims barn. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
15 Mkuu kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Helidai kutoka mji wa Netopafa, kutoka ukoo uliotoka kwa Othinieli. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Den tolfte, den som tjänstgjorde under tolfte månaden, var netofatiten Heldai, som hörde till Otniels släkt. Och i hans avdelning voro tjugufyra tusen.
16 Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kwa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maka alikuwa kiongozi.
Och Israels stamhövdingar voro dessa: furste för rubeniterna var Elieser, Sikris son; för simeoniterna Sefatja, Maakas son;
17 Kwa kabila la Lawi, Hashinia mwana wa Kemueli alikuwa kiongozi, na Zadoki aliongoza uzao wa Aruni.
för Levi Hasabja, Kemuels son; för Arons släkt Sadok;
18 Kwa kabila la Yuda, Elihu, mmoja wa kaka zake Daudi, alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli alikuwa kiongozi.
för Juda Elihu, en av Davids bröder; för Isaskar Omri, Mikaels son;
19 Kwa kabila la Zebuluni, Ishimaia mwana wa Obadia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Naftali, Yeremothi mwana wa Azirieli alikuwa kiongozi.
för Sebulon Jismaja, Obadjas son; för Naftali Jerimot, Asriels son;
20 Kwa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaia alikuwa kiongozi.
för Efraims barn Hosea, Asasjas son; för ena hälften av Manasse stam Joel, Pedajas son;
21 Kwa nusu kabila la Manase lililo Gileadi, Ido mwana wa Zekaria alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri alikuwa kiongozi.
för andra hälften av Manasse, den i Gilead, Jiddo, Sakarjas son; för Benjamin Jaasiel, Abners son;
22 Kwa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu alikuwa kiongozi. Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli.
för Dan Asarel, Jerohams son. Dessa voro Israels stamhövdingar.
23 Daudi hakuwa hesabu wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi, kwasababu Yahweh alihaidi kuongeza Israeli kama nyota za mbinguni.
Men David tog i förteckningen icke upp dem som voro under tjugu år, ty HERREN hade lovat att han ville föröka Israel såsom stjärnorna på himmelen.
24 Yoabu mwana wa Zeruia alianza kuhesabu wanaume, lakini hakumaliza. Gadhabu iliangukia Israeli kwa hili. Hii idadi haikuandikwa kwenye nyakati za mfalme Daudi.
Joab, Serujas son, begynte räkningen, men fullbordade den icke, ty genom den kom förtörnelse över Israel; och antalet togs icke upp i någon förteckning i konung Davids krönika.
25 Azimavethi mwana wa Adieli alikuwa mhusika wa hazina za mfalme. Yonathani mwana wa Uzia alikuwa juu ya nyumba za ghala katika mashamba, kwenye miji, na vijijini, na kwenye minara iliyo imarishwa.
Uppsikten över konungens skatter hade Asmavet, Adiels son; över förråden på fälten, i städerna och byarna och fästningstornen Jonatan, Ussias son;
26 Ezri mwana wa Kelubi alikuwa juu ya mashamba, hao walio lima ardhi.
över dem som arbetade på fältet med jordbruket Esri, Kelubs son;
27 Shimei kutoka Rama alikuwa juu ya mashamba ya mizabibu, na Zabdi kutoka Shefamu alikuwa juu ya mizabibu na mhifadhi wa mvinyo.
över vingårdarna ramatiten Simei; över de vinförråd som man hade samlat i vingårdarna sifmiten Sabdi;
28 Mwangalizi wa miti mizeituni na miti ya mikuyu iliyo kuwa bondeni alikuwa Baali Hanani kutoka Gederi, na juu ya nyumba za ghala za mafuta alikuwa Yoashi.
över olivplanteringarna och mullbärsfikonträden i Låglandet gaderiten Baal-Hanan; över oljeförråden Joas.
29 Juu ya mifugo iliyo kuwa inalishwa huko Sharoni alikuwa Shitrai kutoka Sharoni, na juu ya mifugo iliyo kuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.
Över de fäkreatur som betade i Saron saroniten Sitrai, och över fäkreaturen i dalarna Safat, Adlais son;
30 Msimamizi wa ngamia alikuwa Obili Mishimaeli, na juu ya punda wakike alikuwa Yehideia kutoka Meronothi. Juu ya mifugo alikuwa Yazizi Mhagri.
över kamelerna ismaeliten Obil; över åsninnorna meronotiten Jedeja;
31 Hawa wote walikuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.
över småboskapen hagariten Jasis. Alla dessa voro uppsyningsmän över konung Davids ägodelar.
32 Yonathani, mjomba wake Daudi alikuwa mshauri, sababu alikuwa na busara na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakimoni aliwajali watoto wa mfalme.
Men Jonatan, Davids farbroder, var rådgivare; han var en förståndig och skriftlärd man. Jehiel, Hakmonis son, var anställd hos konungens söner.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai kutoka watu wa Waariki alikuwa mshauri wake wa siri.
Ahitofel var konungens rådgivare, och arkiten Husai var konungens vän.
34 Nafasi ya Ahithofeli ilichukuliwa na Yehoiada mwana wa Benaia, na Abiathari. Yoabu alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.
Efter Ahitofel kom Jojada, Benajas son, och Ebjatar. Och Joab var konungens härhövitsman.

< 1 Nyakati 27 >