< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ni orodha ya familia za viongozi wa Israeli, wakuu wa maelfu na mamia, pamoja na maafisa wa jeshi walio mtumikia mfalme kwa namna tofauti. Kila kikosi cha jeshi kilitumika mwenzi hadi mwezi kwa mwaka mzima. Kila kikosi kilikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Now the sons of Israel according to their number, heads of families, captains of thousands and captains of hundreds, and scribes ministering to the king, and for every affair of the king according to [their] divisions, [for] every ordinance of coming in and going out monthly, for all the months of the year, one division of them [was] twenty-four thousand.
2 Kwa mwezi wa kwanza wa kikosi alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
And over the first division of the first month [was] Isboaz the son of Zabdiel: in his division [were] twenty-four thousand.
3 Alikuwa miongoni mwa uzao wa Perezi na mhusika wa maafisa wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
Of the sons of Tharez [one] was chief of all the captains of the host for the first month.
4 Juu ya kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai, wa ukoo wa uliotoka kwa Ahoa. Mikilothi alikuwa wa pili kwa cheo. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
And over the division of the second month [was] Dodia the son of Ecchoc, and over his division [was] Makelloth also chief: and in his division [were] twenty and four thousand, chief men of the host.
5 Mkuu wa jeshi wa mwezi wa tatu alikuwa Benaia mwana wa Yehoiada, kuhani na kiongozi. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The third for the third month [was] Banaias the son of Jodae the chief priest: and in his division [were] twenty and four thousand.
6 Huyu ni Benaia aliye kuwa kiongozi wa wale thelathini na juu ya wale thelathini. Amizabadi mwanae alikuwa katika kikosi chake.
This Banaeas [was] more mighty than the thirty, and over the thirty: and Zabad his son [was] over his division.
7 Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu. Zebadia mwanae akawa mkuu baada yake. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
The fourth for the fourth month [was] Asael the brother of Joab, and Zabadias his son, and his brethren: and in his division [were] twenty and four thousand.
8 Mkuu kwa mwezi wa tano alikuwa Shamihuthi, mzao wa Izra. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The fifth chief for the fifth month [was] Samaoth the Jezraite: and in his division [were] twenty and four thousand.
9 Mkuu kwa mwezi wa sita alikuwa Ira mwana wa Ikeshi, kutoka Tekoa. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The sixth for the sixth month [was] Hoduias the son of Ekkes the Thecoite: and in his division [were] twenty and four thousand.
10 Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The seventh for the seventh month [was] Chelles of Phallus of the children of Ephraim: and in his division [were] twenty and four thousand.
11 Mkuu kwa mwezi wa nane alikuwa Sibekai Mhushathi, kutoka ukoo ulitoka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The eighth for the eighth month [was] Sobochai the Usathite, [belonging] to Zarai: and in his division [were] twenty and four thousand.
12 Mkuu kwa mwezi wa tisa alikuwa Abi Ezeri Manathothi, kutoka kwa kabila la Benjamini. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The ninth for the ninth month [was] Abiezer of Anathoth, of the land of Benjamin: and in his division [were] twenty and four thousand.
13 Mkuu kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai kutoka mji wa Netofa, kutoka ukoo ulio toka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The tenth for the tenth month [was] Meera the Netophathite, [belonging] to Zarai: and in his division [were] twenty and four thousand.
14 Mkuu kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaia kutoka mji wa Pirathoni, kutoka kabila la Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The eleventh for the eleventh month [was] Banaias of Pharathon, of the sons of Ephraim: and in his division [were] twenty and four thousand.
15 Mkuu kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Helidai kutoka mji wa Netopafa, kutoka ukoo uliotoka kwa Othinieli. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The twelfth for the twelfth month [was] Choldia the Netophathite, [belonging] to Gothoniel: and in his division [were] twenty and four thousand.
16 Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kwa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maka alikuwa kiongozi.
And over the tribes of Israel, the chief for Ruben [was] Eliezer the son of Zechri: for Symeon, Saphatias the son of Maacha:
17 Kwa kabila la Lawi, Hashinia mwana wa Kemueli alikuwa kiongozi, na Zadoki aliongoza uzao wa Aruni.
for Levi, Asabias the son of Camuel: for Aaron, Sadoc:
18 Kwa kabila la Yuda, Elihu, mmoja wa kaka zake Daudi, alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli alikuwa kiongozi.
for Juda, Eliab of the brethren of David: for Issachar, Ambri the son of Michael:
19 Kwa kabila la Zebuluni, Ishimaia mwana wa Obadia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Naftali, Yeremothi mwana wa Azirieli alikuwa kiongozi.
for Zabulon, Samaeas the son of Abdiu: for Nephthali, Jerimoth the son of Oziel:
20 Kwa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaia alikuwa kiongozi.
for Ephraim, Ose the son of Ozia: for the half-tribe of Manasse, Joel the son of Phadaea:
21 Kwa nusu kabila la Manase lililo Gileadi, Ido mwana wa Zekaria alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri alikuwa kiongozi.
for the half-tribe of Manasse in the land of Galaad, Jadai the son of Zadaeas, for the sons of Benjamin, Jasiel the son of Abenner:
22 Kwa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu alikuwa kiongozi. Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli.
for Dan, Azariel the son of Iroab: these [are] the chiefs of the tribes of Israel.
23 Daudi hakuwa hesabu wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi, kwasababu Yahweh alihaidi kuongeza Israeli kama nyota za mbinguni.
But David took not their number from twenty years old and under: because the Lord said that he would multiply Israel as the stars of the heaven.
24 Yoabu mwana wa Zeruia alianza kuhesabu wanaume, lakini hakumaliza. Gadhabu iliangukia Israeli kwa hili. Hii idadi haikuandikwa kwenye nyakati za mfalme Daudi.
And Joab the son of Saruia began to number the people, and did not finish the work, for there was hereupon wrath on Israel; and the number was not recorded in the book of the chronicles of king David.
25 Azimavethi mwana wa Adieli alikuwa mhusika wa hazina za mfalme. Yonathani mwana wa Uzia alikuwa juu ya nyumba za ghala katika mashamba, kwenye miji, na vijijini, na kwenye minara iliyo imarishwa.
And over the king's treasures [was] Asmoth the son of Odiel; and over the treasures in the country, and in the towns, and in the villages, and in the towers, [was] Jonathan the son of Ozia.
26 Ezri mwana wa Kelubi alikuwa juu ya mashamba, hao walio lima ardhi.
And over the husbandmen who tilled the ground [was] Esdri the son of Chelub.
27 Shimei kutoka Rama alikuwa juu ya mashamba ya mizabibu, na Zabdi kutoka Shefamu alikuwa juu ya mizabibu na mhifadhi wa mvinyo.
And over the fields [was] Semei of Rael; and over the treasures of wine in the fields [was] Zabdi the son of Sephni.
28 Mwangalizi wa miti mizeituni na miti ya mikuyu iliyo kuwa bondeni alikuwa Baali Hanani kutoka Gederi, na juu ya nyumba za ghala za mafuta alikuwa Yoashi.
And over the olive yards, and over the sycamores in the plain country [was] Ballanan the Gedorite; and over the stores of oil [was] Joas.
29 Juu ya mifugo iliyo kuwa inalishwa huko Sharoni alikuwa Shitrai kutoka Sharoni, na juu ya mifugo iliyo kuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.
And over the oxen pasturing in Saron [was] Satrai the Saronite; and over the oxen in the valleys [was] Sophat the son of Adli.
30 Msimamizi wa ngamia alikuwa Obili Mishimaeli, na juu ya punda wakike alikuwa Yehideia kutoka Meronothi. Juu ya mifugo alikuwa Yazizi Mhagri.
And over the camels [was] Abias the Ismaelite; and over the asses [was] Jadias of Merathon.
31 Hawa wote walikuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.
And over the sheep [was] Jaziz the Agarite. All these [were] superintendents of the substance of king David.
32 Yonathani, mjomba wake Daudi alikuwa mshauri, sababu alikuwa na busara na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakimoni aliwajali watoto wa mfalme.
And Jonathan, David's uncle by the father's side, [was] a counsellor, a wise man: and Jeel the son of Achami [was] with the king's sons.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai kutoka watu wa Waariki alikuwa mshauri wake wa siri.
Achitophel [was] the king's counsellor: and Chusi the chief friend of the king.
34 Nafasi ya Ahithofeli ilichukuliwa na Yehoiada mwana wa Benaia, na Abiathari. Yoabu alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.
And after this Achitophel Jodae the son of Banaeas [came] next, and Abiathar: and Joab [was] the king's commander-in-chief.

< 1 Nyakati 27 >