< 1 Nyakati 21 >

1 Adui akainuka dhidi ya Israeli na kumchochea Daudi kuhesabu Israeli.
And Satan stood up against Israel, and moved David to number Israel.
2 Daudi akamwabia Yoabu na kwa wakuu wa Jeshi, “Nenda, wahesabu watu wa Israeli kutoka Beerisheba mpaka Dani na uniletee taarifa, ilinijue idadi yao.”
And David said to Joab and to the princes of the people: 'Go, number Israel from Beersheba even to Dan; and bring me word, that I may know the sum of them.'
3 Yoabu akasema, “Yahweh na afanya jeshi lake mara mia zaidi ya lilivyo. Lakini bwana wangu mfalme, kwani wote hawamtumikii bwana wangu? kwa nini bwana wangu anataka hili? Kwa nini ulete hatia kwa Israeli?”
And Joab said: 'The LORD make His people a hundred times so many more as they are; but, my lord the king, are they not all my lord's servants? why doth my lord require this thing? why will he be a cause of guilt unto Israel?'
4 Lakini neno la mfalme halikubadilika kwa Yoabu. Hivyo Yoabu akaondoka na kwenda Israeli yote. Kisha akarudi Yerusalemu.
Nevertheless the king's word prevailed against Joab. Wherefore Joab departed and went throughout all Israel, and came to Jerusalem.
5 Yoabu akatoa taarifa ya idadi ya jumla ya wanaume wa mapambano kwa Daudi. Kulikuwa ndani ya Israeli wanaume 1, 100, 000 walio beba upanga. Yuda peke yake kulikuwa na wanajeshi 470, 000.
And Joab gave up the sum of the numbering of the people unto David. And all they of Israel were a thousand thousand and a hundred thousand men that drew sword; and Judah was four hundred three-score and ten thousand men that drew sword.
6 Lakini Levi na Benjamini hawaku hesabiwa miongoni mwao, kwa kuwa amri ya mfalme ilimuudhi Yoabu.
But Levi and Benjamin he did not number among them; for the king's word was abominable to Joab.
7 Mungu alikwazika na hili tendo, akashambulia Israeli.
And God was displeased with this thing; therefore He smote Israel.
8 Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya hili. Sasa chukua hatia ya mtumishi wako, nimetenda kwa ujinga sana.”
And David said unto God: 'I have sinned greatly, in that I have done this thing; but now, put away, I beseech Thee, the iniquity of Thy servant; for I have done very foolishly.'
9 Yahweh akamwambia Gadi, nabii wa Daudi,
And the LORD spoke unto Gad, David's seer, saying:
10 “Nenda useme kwa Daudi, “Hili ndilo Yahweh anasema: Ninakupa maamuzi matatu. Chagua moja wapo.”
'Go and speak unto David, saying: Thus saith the LORD: I offer thee three things; choose thee one of them, that I may do it unto thee.'
11 Hivyo Gadi akaenda kwa Daudi na kusema, “Yahweh anasema hivi, 'Chagua moja ya haya:
So Gad came to David, and said unto him: 'Thus saith the LORD: Take which thou wilt:
12 kati ya miaka mitatu ya ukame, miezi mitatu unakimbizwa na adui zako na kupatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Yahweh, yani, pigo katika nchi, malaika wa Yahweh akiharibu nchi yote ya Israeli.' Hivyo sasa, amua jibu gani ni mpelekee yeye aliye nituma.”
either three years of famine; or three months to be swept away before thy foes, while the sword of thine enemies overtaketh thee; or else three days the sword of the LORD, even pestilence in the land, and the angel of the LORD destroying throughout all the borders of Israel. Now therefore consider what answer I shall return to Him that sent me.'
13 Kisha Daudi akamwambia Gadi, “Nipo katika shida kubwa sana. Acha nianguke katika mikono ya Yahweh kuliko kuangukia mikono ya mwanadamu, sababu matendo yake ya rehema ni makubwa mno.”
And David said unto Gad: 'I am in a great strait; let me fall now into the hand of the LORD, for very great are His mercies; and let me not fall into the hand of man.'
14 Hivyo Yahweh akatuma pigo Israeli, na watu elfu sabini wakafa.
So the LORD sent a pestilence upon Israel; and there fell of Israel seventy thousand men.
15 Mungu akatuma malaika Yerusalemu kuiharibu. Wakati alipo taka kuiharibu, Yahweh akatazama na kubadili nia yake kuhusu shambulio. Akasema kwa malaika wa uharibifu, “Imetosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Yahweh alikua amesimama eneo la kupeta la Orinani Myebusi.
And God sent an angel unto Jerusalem to destroy it; and as he was about to destroy, the LORD beheld, and He repented Him of the evil, and said to the destroying angel: 'It is enough; now stay thy hand.' And the angel of the LORD was standing by the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
16 Daudi akatazama juu na kuona malaika wa Yahweh amesimama kati ya nchi na mbingu, akiwa na upanga mkonono mwake akiuelekeza Yerusalemu. Kisha Daudi na wazee, wakiwa wamevaa magunia, wakalala chini uso ukiwa kwenye ardhi.
And David lifted up his eyes, and saw the angel of the LORD standing between the earth and the heaven, having a drawn sword in his hand stretched out over Jerusalem. Then David and the elders, clothed in sackcloth, fell upon their faces.
17 Daudi akamwambia Mungu, “Sio mimi niliye amuru jeshi kuhesabiwa? Nimefanya hichi kitu kiovu. Lakini hawa kondoo, wamefanya nini? Yahweh Mungu wangu! Acha mkono wako unipige mimi na familia yangu, lakini usiache pigo iliendelee kubaki kwa watu wako.”
And David said unto God: 'Is it not I that commanded the people to be numbered? even I it is that have sinned and done very wickedly; but these sheep, what have they done? let Thy hand, I pray Thee, O LORD my God, be against me, and against my father's house; but not against Thy people, that they should be plagued.'
18 Hivyo malaika wa Yahweh akamuamuru Gadi kusema kwa Daudi, kwamba Daudi aende juu na kujenga madhabahu ya Yahweh katika eneo la kupeta la Oranani Myebusi.
Then the angel of the LORD commanded Gad to say to David, that David should go up, and rear an altar unto the LORD in the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
19 Daudi akaenda kama Gadi alivyo muelekeza cha kufanya kwa jina la Yahweh.
And David went up at the saying of Gad, which he spoke in the name of the LORD.
20 Wakati Orinani akipepeta ngano, aligeuka na kumuona malaika. Yeye na wana wake wanne wakajificha.
And Ornan turned back, and saw the angel; and his four sons that were with him hid themselves. Now Ornan was threshing wheat.
21 Wakati Daudi alipo kuja kwa Orinani, Orinani akatazama na kumuona Daudi. Aliacha eneo la kupeta na akamuinamia Daudi uso wake ukiwa kwenye ardhi.
And as David came to Ornan, Ornan looked and saw David, and went out of the threshing-floor, and bowed down to David with his face to the ground.
22 Kisha Daudi akasema kwa Orinani, “Niuzie hili eneo la kupeta, iliniweze kumjenga Yahweh madhabahu. Nitalipa gharama yote, ili pigo liondolewe kwa watu.”
Then David said to Ornan: 'Give me the place of this threshing-floor, that I may build thereon an altar unto the LORD; for the full price shalt thou give it me; that the plague may be stayed from the people.'
23 Orinani wakwambia Daudi, “Chukuwa kama lako, bwana wangu mfalme. Fanya nalo linalo kupendeza. Tazama, nitakupa ng'ombe kwa sadaka ya kuteketeza, vifaa vya kupeta kwa ajili ya mbao, na ngano kwa sadaka ya mbegu; nitakupa yote wewe.”
And Ornan said unto David: 'Take it to thee, and let my lord the king do that which is good in his eyes; lo, I give thee the oxen for burnt-offerings, and the threshing-instruments for wood, and the wheat for the meal-offering; I give it all'
24 Mfalme Daudi akamwambia Orinani, “Hapana, nina sisitiza kununua kwa bei yote. Sitachukua kilicho chako na kutoa kama sadaka ya kuteketeza kwa Yahweh kama haitanighramu chochote.”
And king David said to Ornan: 'Nay, but I will verily buy it for the full price; for I will not take that which is thine for the LORD, nor offer a burnt-offering without cost.'
25 Hivyo Daudi akalipa shekeli mia sita ya dhahabu kwa hilo eneo.
So David gave to Ornan for the place six hundred shekels of gold by weight.
26 Daudi akajenga madhabahu ya Yahweh pale na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za ushirika. Akamuita Yahweh, aliye mjibu kwa moto kutoka mbinguni kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketezwa.
And David built there an altar unto the LORD, and offered burnt-offerings and peace-offerings, and called upon the LORD; and He answered him from heaven by fire upon the altar of burnt-offering.
27 Kisha Yahweh akampa agizo malaika, na malaika akarudisha upanga kwenye mfuko wake.
And the LORD commanded the angel; and he put up his sword back into the sheath thereof.
28 Daudi alipo ona kuwa Yahweh amemjibu kwenye eneo la kupeta la Orinani Myebusi, alitoa dhabihu pale pale kwa wakati huo.
At that time, when David saw that the LORD had answered him in the threshing-floor of Ornan the Jebusite, then he sacrificed there.
29 Sasa kwa wakati huo, hema la kuabudia la Yahweh, ambalo Musa alilitengeneza nyikani, na madhabahu ya sadaka za kuteketezwa, zilikuwa sehemu ya juu huko Gibeoni.
For the tabernacle of the LORD, which Moses made in the wilderness, and the altar of burnt-offering, were at that time in the high place at Gibeon.
30 Walakini, Daudi hakuweza kwenda huko kumuliza Mungu muelekeo, kwa kuwa alikuwa anaogopa upanga wa malaika wa Yahweh.
But David could not go before it to inquire of God; for he was terrified because of the sword of the angel of the LORD.

< 1 Nyakati 21 >