< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta ndani Sanduku la Mungu na kuweka katika ya hema ambalo Daudi aliandaa. Kisha wakatoa sadaka ya kuteketeza na sadaka ya ushirika mbele ya Mungu.
And they brought in the ark of God, and set it in the midst of the tent that David had pitched for it: and they offered burnt offerings and peace offerings before God.
2 Daudi alipo maliza kutoa dhabiu ya kuteketeza na sadaka za ushirika, aliwabariki watu kwa jina la Yahweh.
And when David had made an end of offering the burnt offering and the peace offerings, he blessed the people in the name of the LORD.
3 Alisambaza kwa kila Misraeli, mwanaume na mwanamke, kipande cha mkate, na kipande cha nyama, na keki ya mzabibu.
And he dealt to every one of Israel, both man and woman, to every one a loaf of bread, and a portion [of flesh], and a cake of raisins.
4 Daudi aliewapangia baadhi ya Walawi kutumika mbele ya sanduku la Yahweh, na kusheherekea, kushukuru na kumsifu Yahweh, Mungu wa Israeli.
And he appointed certain of the Levites to minister before the ark of the LORD, and to celebrate and to thank and praise the LORD, the God of Israel:
5 Hawa Walawi walikuwa Asafu kiongozi, wa pili kutoka kwake Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaia, Obedi Edomu, na Yeieli. Hawa walikuwa wacheze na vyombo vya uzi na vinubi. Asafu alikuwa apige upatu, kwa kelele.
Asaph the chief, and second to him Zechariah, Jeiel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Mattithiah, and Eliab, and Benaiah, and Obed-edom, and Jeiel, with psalteries and with harps; and Asaph with cymbals, sounding aloud;
6 Benaia na Yahazieli walikuwa wakupiga tarumbeta kila mara, mbele sanduku la agano la Mungu.
and Benaiah and Jahaziel the priests with trumpets continually, before the ark of the covenant of God.
7 Kisha katika hiyo siku Daudi akawachagua Asafu na kaka zake kuimba hii nyimbo ya shukurani kwa Yahweh.
Then on that day did David first ordain to give thanks unto the LORD, by the hand of Asaph and his brethren.
8 Mpeni shukurani Yahweh, liitieni jina lake; fahamisheni mataifa matendo yake.
O give thanks unto the LORD, call upon his name; make known his doings among the peoples.
9 Mwiimbieni, imbeni sifa kwake; semeni matendo yake ya ajabu.
Sing unto him, sing praises unto him; talk ye of all his marvelous works.
10 Jisifuni katika jina lake takatifu; mioyo ya wanao mtafuta Yahweh ishangilie.
Glory ye in his holy name: let the heart of them rejoice that seek the LORD.
11 Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuteni uwepo wake siku zote.
Seek ye the LORD and his strength; seek his face evermore.
12 Kumbukeni matendo aliyo ya fanya kwenu, miujiza yake na amri za kinywa chake,
Remember his marvelous works that he hath done; his wonders, and the judgments of his mouth;
13 enyi uzao wa Israeli mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wateule wake.
O ye seed of Israel his servant, ye children of Jacob, his chosen ones.
14 Yeye ni Yahweh, Mungu wetu. Amri zake zipo duniani kote.
He is the LORD our God: his judgments are in all the earth.
15 Tunzeni agano lake akilini mwenu milele, neno alilo liamuru kwa vizazi elfu moja.
Remember his covenant for ever, the word which he commanded to a thousand generations;
16 Anakumbuka agano alilo lifanya na Ibrahimu, na nadhiri yake kwake Isaka.
[The covenant] which he made with Abraham, and his oath unto Isaac;
17 Hili ndilo alilo lithibitisha kwa Yakobo kama amri maalumu, na kwa Israeli kama agano la milele.
And confirmed the same unto Jacob for a statute, to Israel for an everlasting covenant:
18 Alisema, “Nitakupa nchi ya Kanani kama sehemu ya urithi wako.”
Saying, Unto thee will I give the land of Canaan, the lot of your inheritance:
19 Nilisema hili mlipo kuwa wachache kwa idadi, wachache sana, mlipo kuwa wageni katika nchi.
When ye were but a few men in number; yea, very few, and sojourners in it;
20 Walienda taifa hadi taifa, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
And they went about from nation to nation, and from one kingdom to another people.
21 Hakuwaruhusu yeyote awatese; aliwahadhibu wafalme kwa ajili yao.
He suffered no man to do them wrong; yea, he reproved kings for their sakes;
22 Alisema, “Msiwaguse wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
[Saying], Touch not mine anointed ones, and do my prophets no harm.
23 Imbeni kwa Yahweh, dunia yote; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Sing unto the LORD, all the earth; shew forth his salvation from day to day.
24 Kirini utukufu wake kwa mataifa, matendo yake makuu kwa mataifa yote.
Declare his glory among the nations, his marvelous works among all the peoples.
25 Kwa kuwa Yahweh ni mkuu na ni wakusifiwa sana, na ni wakuogopewa kuliko miungu yote.
For great is the LORD, and highly to be praised: he also is to be feared above all gods.
26 Kwa kuwa miungu ya mataifa ni sanamu, lakini ni Yahweh aliye umba mbingu.
For all the gods of the peoples are idols: but the LORD made the heavens.
27 Uzuri wa ajabu na utukufu upo uweponi mwake. Uwezo na furaha upo kwake.
Honour and majesty are before him: strength and gladness are in his place.
28 Mpeni sifa Yahweh, enyi koo za watu, mpeni sifa Yahweh utukufu na uwezo;
Give unto the LORD, ye kindreds of the peoples, give unto the LORD glory and strength.
29 Mpeni Yahweh utukufu upasao jina lake. Leta sadaka na mje kwake. Muinamieni Yahweh katika utakatifu wa uzuri wake.
Give unto the LORD the glory due unto his name: bring an offering, and come before him: worship the LORD in the beauty of holiness.
30 Mtetemeke mbele zake, dunia yote. Dunia imeimarishwa; haiwezi kutikisika.
Tremble before him, all the earth: the world also is stablished that it cannot be moved.
31 Mbingu nazo ziwe nafuraha, na dunia ifurahi; na wasema kwa mataifa yote, “Yahweh anatawala.”
Let the heavens be glad, and let the earth rejoice; and let them say among the nations, The LORD reigneth.
32 Bahari na ingurume, na inayo ijaza ipige kelele kwa furaha. Mashamba yawe na furaha tele, na vyote vilivyomo ndani yake.
Let the sea roar and the fulness thereof; let the field exult, and all that is therein;
33 Na miti iliyopo misituni ipige kelele kwa Yahweh, kwa kuwa anakuja kuhukumu dunia.
Then shall the trees of the wood sing for joy before the LORD, for he cometh to judge the earth.
34 Toeni shukurani kwa Yahweh, kwa kuwa ni mwema, uaminifu wa agano lake la dumu ata milele.
O give thanks unto the LORD; for he is good: for his mercy [endureth] for ever.
35 Kisha sema, “Tuokoe, Mungu wa wokovu wetu. Tukusanye pamoja na utuokoe kutoka kwa mataifa mengine, ilikwamba tutoe shukurani kwa jina lako takatifu na tufurahi katika sifa zako.”
And say ye, Save us, O God of our salvation, and gather us together and deliver us from the nations, to give thanks unto thy holy name, and to triumph in thy praise.
36 Na Yahweh, Mungu wa Israeli, asifiwe kutoka milele na milele. Watu wote wakasema, “Amina” na wakamsifu Yahweh.
Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting even to everlasting. And all the people said, Amen, and praised the LORD.
37 Hivyo Daudi akamwacha Asafu na kaka zake pale mbele ya sanduku la Yahweh, kutumika daima mbele ya sanduku, kama kazi za kila siku zilivyo itaji. Obedi Edomu pamoja na ndugu sitini na nane walijumuishwa.
So he left there, before the ark of the covenant of the LORD, Asaph and his brethren, to minister before the ark continually, as every day’s work required:
38 Obedi Edomu mwana wa Yeduthuni, pamoja na Hosa, walikuwa wawe walinzi wa lango.
and Obed-edom with their brethren, threescore and eight; Obed-edom also the son of Jeduthun and Hosah to be doorkeepers:
39 Zadoki kuhani na makuhani wenzake walikuwa watumike mbele ya hema la Yahweh katika mahali pa juu huko Gibeoni.
and Zadok the priest, and his brethren the priests, before the tabernacle of the LORD in the high place that was at Gibeon,
40 Walikuwa watoe sadaka za kuteketeza kwa Yahweh kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketeza daima asubui na jioni, kwa mujibu wa yote yalio andikwa katika amri za Yahweh, aliyo wapa Waisraeli kama sheria.
to offer burnt offerings unto the LORD upon the altar of burnt offering continually morning and evening, even according to all that is written in the law of the LORD, which he commanded unto Israel;
41 Hemani na Yeduthuni walikuwa nao, pamoja na walio chaguliwa kwa jina, kumpa shukurani Yahweh, kwasababu uaminifu wa agano lake la dumu ata milele
and with them Heman and Jeduthun, and the rest that were chosen, who were expressed by name, to give thanks to the LORD, because his mercy [endureth] for ever;
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa viongozi wa wao waliopiga tarumbeta, upatu, na vyombo vingine kwa muziki wa kumuabudu Mungu. Wana wa Yeduthuni walilinda lango.
and with them Heman and Jeduthun [with] trumpets and cymbals for those that should sound aloud, and [with] instruments for the songs of God: and the sons of Jeduthun to be at the gate.
43 Kisha watu wote walirudi nyumbani, na Daudi akarudi kubariki nyumba yake.
And all the people departed every man to his house: and David returned to bless his house.

< 1 Nyakati 16 >