< 1 Nyakati 16 >

1 Wakaleta ndani Sanduku la Mungu na kuweka katika ya hema ambalo Daudi aliandaa. Kisha wakatoa sadaka ya kuteketeza na sadaka ya ushirika mbele ya Mungu.
They brought in the ark of God, and set it in the midst of the tent that David had set up for it: and they offered burnt offerings and peace offerings before God.
2 Daudi alipo maliza kutoa dhabiu ya kuteketeza na sadaka za ushirika, aliwabariki watu kwa jina la Yahweh.
When David had made an end of offering the burnt offering and the peace offerings, he blessed the people in the name of Jehovah.
3 Alisambaza kwa kila Misraeli, mwanaume na mwanamke, kipande cha mkate, na kipande cha nyama, na keki ya mzabibu.
He dealt to everyone of Israel, both man and woman, to every one a loaf of bread, and a portion of meat, and a cake of raisins.
4 Daudi aliewapangia baadhi ya Walawi kutumika mbele ya sanduku la Yahweh, na kusheherekea, kushukuru na kumsifu Yahweh, Mungu wa Israeli.
He appointed certain of the Levites to minister before the ark of Jehovah, and to celebrate and to thank and praise Jehovah, the God of Israel:
5 Hawa Walawi walikuwa Asafu kiongozi, wa pili kutoka kwake Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaia, Obedi Edomu, na Yeieli. Hawa walikuwa wacheze na vyombo vya uzi na vinubi. Asafu alikuwa apige upatu, kwa kelele.
Asaph the chief, and second to him Zechariah, Jaaziel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Mattithiah, and Eliab, and Benaiah, and Obed-Edom, and Jeiel, with stringed instruments and with harps; and Asaph with cymbals, sounding aloud;
6 Benaia na Yahazieli walikuwa wakupiga tarumbeta kila mara, mbele sanduku la agano la Mungu.
and Benaiah and Jahaziel the priests with trumpets continually, before the ark of the covenant of God.
7 Kisha katika hiyo siku Daudi akawachagua Asafu na kaka zake kuimba hii nyimbo ya shukurani kwa Yahweh.
Then on that day David first ordained to give thanks to Jehovah, by the hand of Asaph and his brothers.
8 Mpeni shukurani Yahweh, liitieni jina lake; fahamisheni mataifa matendo yake.
Oh give thanks to Jehovah. Call on his name. Make his deeds known among the peoples.
9 Mwiimbieni, imbeni sifa kwake; semeni matendo yake ya ajabu.
Sing to him. Sing praises to him. Tell of all his marvelous works.
10 Jisifuni katika jina lake takatifu; mioyo ya wanao mtafuta Yahweh ishangilie.
Glory in his holy name. Let the heart of those who seek Jehovah rejoice.
11 Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuteni uwepo wake siku zote.
Seek Jehovah and his strength. Seek his face forever more.
12 Kumbukeni matendo aliyo ya fanya kwenu, miujiza yake na amri za kinywa chake,
Remember his marvelous works that he has done, his wonders, and the judgments of his mouth,
13 enyi uzao wa Israeli mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wateule wake.
you offspring of Israel his servant, you descendants of Jacob, his chosen ones.
14 Yeye ni Yahweh, Mungu wetu. Amri zake zipo duniani kote.
He is Jehovah our God. His judgments are in all the earth.
15 Tunzeni agano lake akilini mwenu milele, neno alilo liamuru kwa vizazi elfu moja.
Remember his covenant forever, the word which he commanded to a thousand generations,
16 Anakumbuka agano alilo lifanya na Ibrahimu, na nadhiri yake kwake Isaka.
the covenant which he made with Abraham, his oath to Isaac.
17 Hili ndilo alilo lithibitisha kwa Yakobo kama amri maalumu, na kwa Israeli kama agano la milele.
He confirmed the same to Jacob for a statute, and to Israel for an everlasting covenant,
18 Alisema, “Nitakupa nchi ya Kanani kama sehemu ya urithi wako.”
saying, "I will give you the land of Canaan, The lot of your inheritance,"
19 Nilisema hili mlipo kuwa wachache kwa idadi, wachache sana, mlipo kuwa wageni katika nchi.
when you were but a few men in number, yes, very few, and foreigners were in it.
20 Walienda taifa hadi taifa, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
They went about from nation to nation, from one kingdom to another people.
21 Hakuwaruhusu yeyote awatese; aliwahadhibu wafalme kwa ajili yao.
He allowed no man to do them wrong. Yes, he reproved kings for their sakes,
22 Alisema, “Msiwaguse wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
"Do not touch my anointed ones. Do my prophets no harm."
23 Imbeni kwa Yahweh, dunia yote; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
Sing to Jehovah, all the earth. Display his salvation from day to day.
24 Kirini utukufu wake kwa mataifa, matendo yake makuu kwa mataifa yote.
Declare his glory among the nations, and his marvelous works among all the peoples.
25 Kwa kuwa Yahweh ni mkuu na ni wakusifiwa sana, na ni wakuogopewa kuliko miungu yote.
For great is Jehovah, and greatly to be praised. He also is to be feared above all gods.
26 Kwa kuwa miungu ya mataifa ni sanamu, lakini ni Yahweh aliye umba mbingu.
For all the gods of the peoples are idols, but Jehovah made the heavens.
27 Uzuri wa ajabu na utukufu upo uweponi mwake. Uwezo na furaha upo kwake.
Honor and majesty are before him. Strength and gladness are in his place.
28 Mpeni sifa Yahweh, enyi koo za watu, mpeni sifa Yahweh utukufu na uwezo;
Ascribe to Jehovah, you relatives of the peoples, ascribe to Jehovah glory and strength.
29 Mpeni Yahweh utukufu upasao jina lake. Leta sadaka na mje kwake. Muinamieni Yahweh katika utakatifu wa uzuri wake.
Ascribe to Jehovah the glory due to his name. Bring an offering, and come before him. Worship Jehovah in holy array.
30 Mtetemeke mbele zake, dunia yote. Dunia imeimarishwa; haiwezi kutikisika.
Tremble before him, all the earth. The world also is established that it can't be moved.
31 Mbingu nazo ziwe nafuraha, na dunia ifurahi; na wasema kwa mataifa yote, “Yahweh anatawala.”
Let the heavens be glad, and let the earth rejoice. Let them say among the nations, "Jehovah reigns."
32 Bahari na ingurume, na inayo ijaza ipige kelele kwa furaha. Mashamba yawe na furaha tele, na vyote vilivyomo ndani yake.
Let the sea roar, and its fullness. Let the field exult, and all that is in it.
33 Na miti iliyopo misituni ipige kelele kwa Yahweh, kwa kuwa anakuja kuhukumu dunia.
Then the trees of the forest will sing for joy before Jehovah, for he comes to judge the earth.
34 Toeni shukurani kwa Yahweh, kwa kuwa ni mwema, uaminifu wa agano lake la dumu ata milele.
Oh give thanks to Jehovah, for he is good, for his loving kindness endures forever.
35 Kisha sema, “Tuokoe, Mungu wa wokovu wetu. Tukusanye pamoja na utuokoe kutoka kwa mataifa mengine, ilikwamba tutoe shukurani kwa jina lako takatifu na tufurahi katika sifa zako.”
Say, "Save us, God of our salvation. Gather us together and deliver us from the nations, to give thanks to your holy name, to triumph in your praise."
36 Na Yahweh, Mungu wa Israeli, asifiwe kutoka milele na milele. Watu wote wakasema, “Amina” na wakamsifu Yahweh.
Blessed be Jehovah, the God of Israel, from everlasting to everlasting. And all the people said, "Amen," and praised Jehovah.
37 Hivyo Daudi akamwacha Asafu na kaka zake pale mbele ya sanduku la Yahweh, kutumika daima mbele ya sanduku, kama kazi za kila siku zilivyo itaji. Obedi Edomu pamoja na ndugu sitini na nane walijumuishwa.
So he left there, before the ark of the covenant of Jehovah, Asaph and his brothers, to minister before the ark continually, as every day's work required;
38 Obedi Edomu mwana wa Yeduthuni, pamoja na Hosa, walikuwa wawe walinzi wa lango.
and Obed-Edom with their brothers, sixty-eight; Obed-Edom also the son of Jeduthun and Hosah to be doorkeepers;
39 Zadoki kuhani na makuhani wenzake walikuwa watumike mbele ya hema la Yahweh katika mahali pa juu huko Gibeoni.
and Zadok the priest, and his brothers the priests, before the tabernacle of Jehovah in the high place that was at Gibeon,
40 Walikuwa watoe sadaka za kuteketeza kwa Yahweh kwenye madhabahu ya sadaka za kuteketeza daima asubui na jioni, kwa mujibu wa yote yalio andikwa katika amri za Yahweh, aliyo wapa Waisraeli kama sheria.
to offer burnt offerings to Jehovah on the altar of burnt offering continually morning and evening, even according to all that is written in the law of Jehovah, which he commanded to Israel;
41 Hemani na Yeduthuni walikuwa nao, pamoja na walio chaguliwa kwa jina, kumpa shukurani Yahweh, kwasababu uaminifu wa agano lake la dumu ata milele
and with them Heman and Jeduthun, and the rest who were chosen, who were mentioned by name, to give thanks to Jehovah, because his loving kindness endures forever;
42 Hemani na Yeduthuni walikuwa viongozi wa wao waliopiga tarumbeta, upatu, na vyombo vingine kwa muziki wa kumuabudu Mungu. Wana wa Yeduthuni walilinda lango.
and with them Heman and Jeduthun with trumpets and cymbals for those that should sound aloud, and with instruments for the songs of God; and the sons of Jeduthun to be at the gate.
43 Kisha watu wote walirudi nyumbani, na Daudi akarudi kubariki nyumba yake.
All the people departed every man to his house: and David returned to bless his house.

< 1 Nyakati 16 >