< 1 Nyakati 15 >

1 Daudi akajingea nyumba zake katika mji wa Daudi. Akaanda sehemu kwa ajili ya sanduku la Mungu na hema lake.
And David made houses for himself in the town of David; and he got ready a place for the ark of God, and put up a tent for it.
2 Kisha Daudi akasema, “Walawi pekee ndio watabeba sanduku la Mungu, kwa kuwa walichaguliwa na Yahweh kubeba sanduku la Yahweh, na kumtumikia milele.”
Then David said, The ark of God may not be moved by any but the Levites, for they have been marked out by God to take the ark of God, and to do his work for ever.
3 Kisha Daudi akakusanya Israeli yote Yerusalemu, kuleta sanduku la Yahweh sehemu aliyo iandaa.
And David made all Israel come together at Jerusalem, to take the ark of the Lord to its place, which he had got ready for it.
4 Daudi akakusanya uzao wa Aruni na Walawi pamoja.
And David got together the sons of Aaron, and the Levites;
5 Kutoka uzao wa Kohathi, palikuwa na Urieli kiongozi na ndugu zake, wanaume 120.
Of the sons of Kohath: Uriel the chief, and his brothers, a hundred and twenty;
6 Kutoka uzao wa Merari, palikuwa na Asaia kiongozi na ndugu zake, wanaume 220.
Of the sons of Merari: Asaiah the chief, and his brothers, two hundred and twenty;
7 Kutoka uzao wa Gerishomu, palikuwa na Yoeli kiongozi na ndugu zake, wanaume 130.
Of the sons of Gershom: Joel the chief, and his brothers, a hundred and thirty;
8 Kutoka uzao wa Elizafani, palikuwa na Shemaia kiongozi na ndugu zake, wanaume 200.
Of the sons of Elizaphan: Shemaiah the chief, and his brothers, two hundred;
9 Kutoka uzao wa Hebroni, palikuwa na Elieli kiongozi na ndugu zake, wanaume themanini.
Of the sons of Hebron: Eliel the chief, and his brothers, eighty;
10 Kutoka uzao wa Uzieli, palikuwa na Aminadabu kiongozi na ndugu zake, wanaume 112.
Of the sons of Uzziel: Amminadab the chief, and his brothers, a hundred and twelve.
11 Daudi akaagiza Zadoki kuitwa na Abiathari kuhuani, na Walawi Urieli, Asaia, Yoeli, Shemaia, Elieli, na Aminadabu.
And David sent for Zadok and Abiathar the priests, and for the Levites, Uriel, Asaiah and Joel, Shemaiah and Eliel and Amminadab,
12 Akasema, “Nyinyi ni viongozi wa familia za Kilawi. Jiwekeni wakfu, nyie na ndugu zenu, ilikwamba mlete sanduku la Yahweh, Mungu wa Israeli, kwenye sehemu niliyo iandaa.
And said to them, You are the heads of the families of the Levites: make yourselves holy, you and your brothers, so that you may take the ark of the Lord, the God of Israel, to the place which I have made ready for it.
13 Mara ya kwanza hamkubeba. Ndio maana Yahweh Mungu wetu akawa na hasira kwetu, kwa kuwa hatuku mtafuta wala kutii amri yake.”
For because you did not take it at the first, the Lord our God sent punishment on us, because we did not get directions from him in the right way.
14 Hivyo makuhani na Walawi waka jiweka wakfu iliwaweze kuleta sanduku la Yahweh, Mungu wa Israeli.
So the priests and the Levites made themselves holy to take up the ark of the Lord, the God of Israel.
15 Walawi wakabeba sanduku la Mungu katika mabega yao na nguzo, kama Musa alivyo amuru-kwa kufuata sheria zilizo tolewa na Yahweh.
And the sons of the Levites took up the ark of God, lifting it by its rods, as the Lord had said to Moses.
16 Daudi akazungumza na viongozi wa Walawi kuwapangia ndugu zao kuwa wana muziki wenye vyombo vya muziki, vyombo vya uzi, vinubi na upatu, kwa kupiga kwa sauti na furaha wakipaza sauti zao.
And David gave orders to the chief of the Levites to put their brothers the music-makers in position, with instruments of music, corded instruments and brass, with glad voices making sounds of joy.
17 Hivyo Walawi wakamchagua Hemani mwana wa Yoeli na mmoja wa kaka zake, Asafu mwana wa Berekia. Pia walimchagua ndugu wa uzao wa Merari na Ethani mwana wa Kushaia.
So Heman, the son of Joel, and, of his brothers, Asaph, the son of Berechiah; and of the sons of Merari their brothers, Ethan, the son of Kushaiah, were put in position by the Levites;
18 Pamoja nao walikuwa ndugu wa daraja la pili: Zekarai, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaia, Maasaeia, Matithia, Elifelehu, Mikineaia, Obedi Edomu, na Yeieli, mlinzi wa lango.
And with them their brothers of the second order, Zechariah, Bani and Jaaziel and Shemiramoth and Jehiel and Unni, Eliab and Benaiah and Maaseiah and Mattithiah and Eliphelehu and Mikneiah, and Obed-edom and Jeiel, the door-keepers.
19 Wanamuziki Hemani, Asafu, na Ethani walichaguliwa kupiga upatu wa shaba.
So those who made melody, Heman, Asaph, and Ethan, were put in position, with brass instruments, sounding loudly;
20 Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni Eliabu, Maaseia, na Benaia walicheza vyombo vya uzi.
And Zechariah and Aziel and Shemiramoth and Jehiel, Unni and Eliab and Maaseiah and Benaiah, with corded instruments put to Alamoth.
21 Matithia, Elifelehu, Mikineia, Obedi Edomu, Yeieli, na Azazia waliongoza njia na vinubi.
And Mattithiah and Eliphelehu and Mikneiah and Obed-edom and Jeiel and Azaziah, with corded instruments on the octave, to give the first note of the song.
22 Kenania, kiongozi wa Walawi, aliongoza uimbaji sababu alikuwa mwalimu wa muziki.
And Chenaniah, chief of the Levites, was master of the music: he gave directions about the song, because he was expert.
23 Berekia na Elikana walikuwa walinzi wa sanduku.
And Berechiah and Elkanah were door-keepers for the ark.
24 Shebania, Yoshafati, Nethanieli, Amasai, Zekaria, Benaia, na Eliezeri, makuhani, walikuwa wa kupuliza matarumbeta mbele ya sanduku la Mungu. Obedi Edomu na Yehia walikuwa walinzi wa sanduku.
And Shebaniah and Joshaphat and Nethanel and Amasai and Zechariah and Benaiah and Eliezer, the priests, made music on the horns before the ark of God; and Obed-edom and Jehiah were door-keepers for the ark.
25 Hivyo Daudi, wazee wa Israeli, na wakuu wa maelfu wakaenda kuchukua sanduku la agano la Yahweh kutoka nyumba ya Obedi Edomu kwa shangwe.
So David, and the responsible men of Israel, and the captains over thousands, went with joy to get the ark of the agreement of the Lord out of the house of Obed-edom.
26 Wakati Mungu alipo wasaidia Walawi kubeba sanduku la agano la Yahweh, walitoa ng'ombe saba na mbuzi
And when God gave help to the Levites who were lifting up the ark of the agreement of the Lord, they made an offering of seven oxen and seven sheep.
27 Daudi alivishwa joho safi la maridadi, pamoja na Walawi walio beba sanduku, waimbaji, na Kenania, kiongozi wa nyimbo na waimbaji. Daudi alivaa juu ya joho lake naivera.
And David was clothed with a robe of fair linen, as were all the Levites who took up the ark, and those who made melody, and Chenaniah the master of those who made melody; and David had on a linen ephod;
28 Hivyo Israeli yote wakaleta sanduku la agano la Yahweh na kelele za shangwe, na sauti za tarumbeta, ngoma za saani, na vyombo vya uzi na vinubi.
So all Israel took up the ark of the agreement of the Lord, with loud cries and with horns and brass and corded instruments sounding loudly.
29 Lakini sanduku la Yahweh lilivyokuja kwa mji wa Daudi, Mikali binti wa Sauli, alitazama nje ya dirisha, Akamuona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea. Kisha akamdharau moyoni mwake.
And when the ark of the agreement of the Lord came into the town of David, Michal, the daughter of Saul, looking out of the window, saw King David dancing and playing; and to her mind he seemed foolish.

< 1 Nyakati 15 >