< 1 Nyakati 11 >

1 Kisha Waisraeli wote walikuja Hebroni kwa Daudi na kusema, “Angalia, sisi ni nyama na mifupa yako.
Then all Israel came to David at Hebron and said, “Look, we are your flesh and bone.
2 Katika wakati uliopita, Sauli alipoo kuwa mfalme juu yetu, ni wewe uliye ongoza jeshi la Israeli. Yahweh Mungu wako alisema kwako, 'utawachunga watu wangu wa Isaraeli, na utakuwa mtawala wa watu wangu wa Israeli”'.
In the recent past, when Saul was king over us, it was you who led the Israelite army. Yahweh your God said to you, 'You will shepherd my people Israel, and you will become a ruler over my people Israel.'”
3 Kwaiyo wazee wote wa Israeli wakamjia mfalme huko Hebroni, na Daudi akafanya agano nao mbele ya Yahweh. Wakampaka mafuta Daudi kuwa mfalme wa Israeli. Kwa namna hii, neno la Yahweh lilo nenwa na Samweli likawa kweli.
So all the elders of Israel came to the king at Hebron, and David made a covenant with them before Yahweh. They anointed David king over Israel. In this way, the word of Yahweh that had been declared by Samuel came true.
4 Daudi na Israeli yote wakaenda Yerusalemu (yani, Yebusi). Sasa Wayebusi, wakazi wa nchi, walikuwa pale.
David and all Israel went to Jerusalem (that is, Jebus). Now the Jebusites, the inhabitants of the land, were there.
5 Wakazi wa yebusi wakamwabia Daudi, “Hautakuja humu.” Lakini Daudi alichukuwa ngome ya Sayuni, mji wa Daudi.
The inhabitants of Jebus said to David, “You will not come in here.” But David took the stronghold of Zion, that is, the city of David.
6 Daudi alisema, “Yeyote atakaye washambulia Wayebusi wa kwanza atakuwa mkuu wa jeshi” kwaiyo Yoabu mwana wa Zeruia akashambulia wa kwanza, hivyo akafanywa mkuu wa jeshi.
David had said, “Whoever attacks the Jebusites first will become chief and commander.” So Joab son of Zeruiah attacked first, so he was made the chief.
7 Daudi akaanza kuishi katika hiyo ngome. Kwaiyo wakaiita mji wa Daudi.
Then David began to live in the stronghold. So they called it the city of David.
8 Akaimarisha mji kutoka Milo na hadi mpaka ukuta unao zunguka. Yoabu akaimairisha mji wote uliyo baki.
He built the city all around from the Millo and back to the surrounding wall. Joab restored the rest of the city.
9 Daudi akawa mkuu na mkuu kwa sababu Yahweh wa Majeshi alikuwa naye.
David became greater and greater because Yahweh of hosts was with him.
10 Hawa walikuwa viongozi Daudi aliyo kuwa nao, waliyo jionyesha imara katika ufalme wake, pamoja na Israeli, kumfanya mfalme, kutii neno la Yahweh kuhusu Israeli.
These were the leaders David had, who showed themselves strong with him in his kingdom, together with all Israel, to make him king, obeying the word of Yahweh concerning Israel.
11 Hii ni orodha ya wanajeshi shupavu wa Daudi. Yashobeami, mwana wa Mhakimoni, alikuwa mkuu wa kikosi cha thelathini. Aliwaua wanaume mia tatu na mkuki wake katika sehemu moja.
This is a list of David's mighty men: Jashobeam, the son of a Hachmonite, was commander of the officers. He killed three hundred men with his spear on one occasion.
12 Baada ya yeye alikuwa Eleazari mwana wa Dodo, Mahohi, aliyekuwa mmoja wa wanaume watatu hodari.
After him was Eleazar son of Dodo, the Ahohite, who was one of the three mighty men.
13 Alikuwa na Daudi huko Pasidamimu, na pale Wafilisti wakakusanyika pamoja kwa mapambano, ambapo palikuwa na uwanja wa ngano na jeshi liliwakimbia Wafilisti.
He was with David at Pas Dammim, and there the Philistines assembled together for battle, where there was a barley field and the army fled from the Philistines.
14 Walisimama katikati ya uwanja. Wakautetea na kuwakata Wafilisti na Yahweh akawaokoa na ushindi mkubwa.
They stood in the middle of the field. They defended it and cut down the Philistines and Yahweh rescued them with a great victory.
15 Kisha watatu wa viongozi thelathini wakashuka chini kwenye mwamba wa Daudi, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti walieka kambi katika bonde la Refaim.
Then three of the thirty leaders went down to the rock to David, to the cave of Adullam. The army of the Philistines was camped in the Valley of Rephaim.
16 Kwa wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, Wafilisti walikita kambi yao Bethilehemu.
At that time David was in his stronghold, a cave, while the Philistines had established their camp at Bethlehem.
17 Daudi alikuwa na kiu ya maji na akasema, “Laiti mtu akanipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho Bethilehemu, kisima kilicho pembeni mwa lango!”
David was longing for water and said, “If only someone would give me water to drink from the well at Bethlehem, the well that is by the gate!”
18 Hawa wanaume hodari watatu wakatoboa kupita jeshi la Wafilisti na kuchota maji kwenye kisima cha Bethilehemu, kisima pembeni mwa lango. Wakachukuwa maji na kumletea Daudi, lakini alikataa kunywa. Badala yake, akamwaga chini kwa Yahweh.
So these three mighty men broke through the army of the Philistines and drew water out of the well of Bethlehem, the well at the gate. They took the water and brought it to David, but he refused to drink it. Instead, he poured it out to Yahweh.
19 Kisha akasema, “Yahweh, iwe mbali na mimi, kwamba ni yanywe haya maji. Je ninywe damu ya wanaume walio hatarisha maisha yao?” Kwa sababu wameeka maisha ya hatarini, akakataa kunywa. Haya ni mambo wanaume hodari watatu walio fanya.
Then he said, “May it be that I should never do this! Should I drink the blood of these men who have risked their lives?” Because they had put their lives at risk, David refused to drink it. These were the deeds of the three mighty men.
20 Abishai kaka wa Yoabu, alikuwa kiongozi wa watatu. Alitumia mkuki wake dhidi ya watu mia tatu na kuwaua. Ametajwa pamoja na wale watatu.
Abishai brother of Joab was captain over the Three. He once used his spear against three hundred and killed them. He is mentioned along with the Three.
21 Kati ya wale watatu, yeye alipewa heshima mara mbili na akawa kiongozi wao. Japo hakuwa mmoja wa miongoni mwao.
Of the Three, he was given double honor and became their captain, even though he was not one of them.
22 Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwanaume mwenye nguvu aliye fanya mambo makuu. Aliua wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka chini ya shimo na kumuua simba wakati theluji ikianguka.
Benaiah son of Jehoiada was a brave warrior from Kabzeel, who did great deeds. He killed the two sons of Ariel of Moab. He also went down into a pit and killed a lion on a day when the snow was falling.
23 Alimua hadi Mmisri, mwanaume mwenye mita mbili na theluthi moja. Mmisri alikuwa na mkuki kama gongo la mshonaji, lakini alimfuata chini na fimbo tu. Akakamata mkuki katika mkono wa Mmisri na kumuua na mkuki wake.
He even killed an Egyptian, a man five cubits tall. The Egyptian had a spear like a weaver's beam, but he went down to him with only a staff. He seized the spear out of the Egyptian's hand and killed him with his own spear.
24 Benaia mwana wa Yehoiada alifanya haya matukio, na akatajwa miongoni mwa wale wanaume hodari watatu.
Benaiah son of Jehoiada did these feats, and he was named alongside the three mighty men.
25 Alisifika zaidi ya wale wanajeshi thelathini kwa ujumla, lakini hakuwa pewa hadhi ya wale wanajeshi watatu hodari. Daudi alimueka kiongozi wa walinzi wake.
He was more highly regarded than the thirty soldiers in general, but he was not regarded quite as highly as the three mighty men. Yet David put him in charge of his bodyguard.
26 Wanaume hodari walikuwa Asaheli kaka wa Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Bethilehemu,
The mighty men were Asahel brother of Joab, Elhanan son of Dodo of Bethlehem,
27 Shamothi Mherori, Helezi Mpeloni,
Shammoth the Harorite, Helez the Pelonite,
28 Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi, Abi Eza Manathothi,
Ira son of Ikkesh the Tekoite, Abiezer the Anathothite,
29 Sibekai Mhushathite, Ilai Mahohite,
Sibbekai the Hushathite, Ilai the Ahohite,
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana Mnetofathite,
Maharai the Netophathite, Heled son of Baanah the Netophathite,
31 Itai mwana wa Ribai wa Gibea uzao wa Benjamini, Benaia Mpirathoni,
Ithai son of Ribai of Gibeah of Benjamin's descendants, Benaiah the Pirathonite,
32 Hurai wa mabonde ya Gaashi, Abieli Marbathi,
Hurai of the valleys of Gaash, Abiel the Arbathite,
33 Azmavethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Azmaveth the Baharumite, Eliahba the Shaalbonite,
34 Mwana wa Hashemu Mgizoni, Yonathani mwana wa Shagee Mhararite,
the sons of Hashem the Gizonite, Jonathan son of Shagee the Hararite,
35 Ahiamu mwana wa Sacari Mhararite, Elifali mwana wa Uri,
Ahiam son of Sakar the Hararite, Eliphal son of Ur,
36 Hefa Mmekarathi, Ahija Mpeloni,
Hepher the Mekerathite, Ahijah the Pelonite,
37 Hezro Mcarmeli, Maarai mwana wa Ezibai,
Hezro the Carmelite, Naarai son of Ezbai,
38 Yoeli kaka wa Nathani, Mibhari mwana wa Hagiri,
Joel brother of Nathan, Mibhar son of Hagri,
39 Zeleki Mamoni, Naharai Mberothi ( mbeba ngao ya Yoabu mwana wa Zeruia),
Zelek the Ammonite, Naharai the Berothite (the armor bearer of Joab son of Zeruiah),
40 Ira Mithire, Garebu Mithire,
Ira the Ithrite, Gareb the Ithrite,
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Ahlai,
Uriah the Hittite, Zabad son of Ahlai,
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni ( kiongozi wa Wareubeni) na thelathini pamoja nae,
Adina son of Shiza the Reubenite (a chief of the Reubenites) and thirty with him,
43 Hanani mwana wa Maaka, na Yoshafati Mmithini,
Hanan son of Maacah, and Joshaphat the Mithnite,
44 Uzia Mashiterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Waaroeri,
Uzzia the Ashterathite, Shama and Jeiel sons of Hotham the Aroerite,
45 Jediaeli mwana wa Shimri, Joha ( kaka yake Mtize),
Jediael son of Shimri, Joha (his brother the Tizite),
46 Elieli Mmahavi, Yeribai na Yoshavia mwana wa Elnaamu, Ithima Mmoabi,
Eliel the Mahavite, Jeribai and Joshaviah sons of Elnaam, Ithmah the Moabite,
47 Elieli, Obedi, na Yaasieli Wamezobai.
Eliel, Obed, and Jaasiel the Mezobaite.

< 1 Nyakati 11 >