< Zekaria 10 >

1 Mwombeni Bwana mvua wakati wa vuli; ndiye Bwana atengenezaye mawingu ya tufani. Huwapa watu manyunyu ya mvua, pia mimea ya shambani kwa ajili ya kila mtu.
Proście PANA o deszcz w późnej porze [deszczowej], a PAN stworzy chmury burzowe i da wam obfity deszcz i każdemu trawę na polu.
2 Sanamu huzungumza udanganyifu, waaguzi huona maono ya uongo; husimulia ndoto ambazo si za kweli, wanatoa faraja batili. Kwa hiyo watu wanatangatanga kama kondoo walioonewa kwa kukosa mchungaji.
Bożki wypowiadają bowiem [słowa] próżności, a wróżbici prorokują kłamstwo i opowiadają zmyślone sny, daremnie pocieszają. Dlatego błąkali się jak trzoda, byli utrapieni, bo nie było pasterza.
3 “Hasira yangu inawaka dhidi ya wachungaji, nami nitawaadhibu viongozi; kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote atalichunga kundi lake, nyumba ya Yuda, naye atawafanya kuwa kama farasi mwenye kiburi akiwa vitani.
Mój gniew zapłonął przeciwko tym pasterzom i ukarałem te kozły, ale PAN zastępów nawiedzi swoją trzodę, dom Judy, i uczyni z niej wspaniałego konia do boju.
4 Kutoka Yuda litatokea Jiwe la pembeni, kutoka kwake vitatoka vigingi vya hema, kutoka kwake utatoka upinde wa vita, kutoka kwake atatoka kila mtawala.
Od niego wywodzi się kamień węgielny, od niego gwóźdź, od niego łuk wojenny, od niego także wszelki poborca.
5 Kwa pamoja watakuwa kama mashujaa wanaokanyaga barabara za matope wakati wa vita. Kwa sababu Bwana yu pamoja nao, watapigana na kuwashinda wapanda farasi.
I będą jak mocarze, którzy wdeptują wroga w błoto uliczne podczas bitwy. I będą walczyć, bo PAN [jest] z nimi; a zawstydzą jeźdźców konnych.
6 “Nitaiimarisha nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yosefu. Nitawarejesha kwa sababu nina huruma juu yao. Watakuwa kama watu ambao sijawahi kuwakataa kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wao, nami nitawajibu.
Umocnię dom Judy, wybawię dom Józefa i sprowadzę ich z powrotem w pokoju, bo zlituję się nad nimi. I będą [takimi], jak gdybym ich nie odrzucił. Ja bowiem jestem PAN, ich Bóg, i wysłucham ich.
7 Waefraimu watakuwa kama mashujaa, mioyo yao itafurahi kana kwamba ni kwa divai. Watoto wao wataona na kufurahi, mioyo yao itashangilia katika Bwana.
Efraimici będą jak mocarz, ich serce rozweseli się jak od wina. Ich synowie to zobaczą i będą się cieszyć, a ich serce rozraduje się w PANU.
8 Nitawaashiria na kuwakusanya ndani. Hakika nitawakomboa, nao watakuwa wengi kama walivyokuwa mwanzoni.
Zaświstam na nich i zgromadzę ich, bo ich odkupiłem; i będą tak liczni, jak byli [dawniej].
9 Ijapokuwa niliwatawanya miongoni mwa mataifa, hata hivyo wakiwa katika nchi za mbali watanikumbuka mimi. Wao na watoto wao watanusurika katika hatari nao watarudi.
I rozsieję ich wśród narodów, aby w dalekich krajach przypomnieli sobie o mnie, a żyjąc tam ze swoimi dziećmi, nawrócą się.
10 Nitawarudisha kutoka Misri na kuwakusanya toka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni, na hapo hapatakuwa na nafasi ya kuwatosha.
Wyprowadzę ich znowu z ziemi Egiptu i zgromadzę ich z Asyrii, zaprowadzę do ziemi Gilead i do Libanu, ale nie starczy dla nich [miejsca].
11 Watapita katika bahari ya mateso; bahari iliyochafuka itatulizwa na vilindi vyote vya Mto Naili vitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa, nayo fimbo ya utawala ya Misri itatoweka.
Przejdzie przez morze ucisku, rozbije fale na morzu i wyschną wszystkie głębie rzeki. Wtedy pycha Asyrii będzie poniżona, a berło Egiptu zniknie.
12 Nitawaimarisha katika Bwana, na katika jina lake watatembea,” asema Bwana.
Umocnię ich też w PANU i będą chodzić w jego imię, mówi PAN.

< Zekaria 10 >