< Wimbo wa Sulemani 4 >

1 Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu! Ee, jinsi ulivyo mzuri! Macho yako nyuma ya shela yako ni kama ya hua. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi zikishuka kutoka Mlima Gileadi.
O jaka ty jesteś piękna, moja umiłowana! O jaka ty jesteś piękna! Twoje oczy między twymi kędziorkami są [jak oczy] gołębicy; twoje włosy są jak stado kóz, które widać na górze Gileadu.
2 Meno yako ni kama kundi la kondoo waliokatwa manyoya sasa hivi, watokao kuogeshwa. Kila mmoja ana pacha lake, hakuna hata mmoja aliye peke yake.
Twoje zęby są jak stado strzyżonych [owiec], gdy wychodzą z kąpieli; wszystkie mają bliźnięta i nie ma żadnej niepłodnej wśród nich.
3 Midomo yako ni kama uzi mwekundu, kinywa chako kinapendeza. Mashavu yako nyuma ya shela yako ni kama vipande viwili vya komamanga.
Twoje wargi [są] jak nić purpurowa, a twoja wymowa pełna wdzięku. Twoje skronie [są] jak połówki granatu między twymi kędziorkami.
4 Shingo yako ni kama mnara wa Daudi, uliojengwa kwa madaha, juu yake zimetundikwa ngao elfu, zote ni ngao za mashujaa.
Twoja szyja [jest] jak wieża Dawida, zbudowana na zbrojownię, na której tysiąc puklerzy zawieszono, wszystko to tarcze dzielnych wojowników.
5 Matiti yako mawili ni kama wana-paa wawili, kama wana-paa mapacha wajilishao katikati ya yungiyungi.
Twoje piersi są jak dwoje bliźniaczych sarniąt, które pasą się między liliami.
6 Hata kupambazuke na vivuli vikimbie, nitakwenda kwenye mlima wa manemane na kwenye kilima cha uvumba.
Nim zaświta dzień i znikną cienie, wejdę na górę mirry i na pagórek kadzidła.
7 Wewe ni mzuri kote, mpenzi wangu, hakuna hitilafu ndani yako.
Cała [jesteś] piękna, moja umiłowana, i nie ma w tobie żadnej skazy.
8 Enda nami kutoka Lebanoni, bibi arusi wangu, enda nami kutoka Lebanoni. Shuka kutoka ncha ya Amana, kutoka juu ya Seniri, kilele cha Hermoni, kutoka mapango ya simba na kutoka mlima wapendapo kukaa chui.
Przyjdź ze mną z Libanu, [moja] oblubienico, [przyjdź] ze mną z Libanu. Spójrz ze szczytu [góry] Amana, ze szczytu [góry] Senir i Hermon, z jaskiń lwów i z gór lampartów.
9 Umeiba moyo wangu, dada yangu, bibi arusi wangu; umeiba moyo wangu kwa mtazamo mmoja wa macho yako, kwa kito kimoja cha mkufu wako.
Zachwyciłaś moje serce, moja siostro, [moja] oblubienico! Zachwyciłaś moje serce jednym twoim okiem i jednym łańcuszkiem na twojej szyi.
10 Tazama jinsi pendo lako linavyofurahisha, dada yangu, bibi arusi wangu! Pendo lako linafurahisha aje zaidi ya divai, na harufu ya manukato yako zaidi ya kikolezo chochote!
Jakże piękna jest twoja miłość, moja siostro, [moja] oblubienico! Jak daleko lepsza jest twoja miłość od wina, a woń twoich olejków od wszystkich innych wonności!
11 Midomo yako inadondosha utamu kama sega la asali, bibi arusi wangu; maziwa na asali viko chini ya ulimi wako. Harufu nzuri ya mavazi yako ni kama ile ya Lebanoni.
Z twoich warg ocieka miód [jak] z plastrów, [moja] oblubienico! Miód i mleko pod twoim językiem, a woń twoich szat jest jak woń Libanu.
12 Wewe ni bustani iliyofungwa, dada yangu, bibi arusi wangu; wewe ni chanzo cha maji kilichozungushiwa kabisa, chemchemi yangu peke yangu.
[Jesteś] zamkniętym ogrodem, moja siostro, [moja] oblubienico; źródłem zamkniętym, zdrojem zapieczętowanym.
13 Mimea yako ni bustani ya mikomamanga yenye matunda mazuri sana, yenye hina na nardo,
Twoje pędy to sad [drzew] granatu z wybornym owocem cyprysu i nardu;
14 nardo na zafarani, mchai na mdalasini, pamoja na kila aina ya mti wa uvumba, manemane na udi, na aina zote za vikolezo bora kuliko vyote.
Nard i szafran, tatarak i cynamon, ze wszelkimi drzewami, kadzidło, mirra i aloes, ze wszelkimi wybornymi wonnościami.
15 Wewe ni chemchemi ya bustani, kisima cha maji yatiririkayo, yakitiririka kutoka Lebanoni.
Źródło ogrodów, zdrój żywych wód, które płyną z Libanu!
16 Amka, upepo wa kaskazini, na uje, upepo wa kusini! Vuma juu ya bustani yangu, ili harufu yake nzuri iweze kuenea mpaka ngʼambo. Mpendwa wangu na aje bustanini mwake na kuonja matunda mazuri sana.
Powstań, wietrze północny, i przyjdź, wietrze z południa, powiej przez mój ogród, by się rozpłynęły jego wonności. Niech przyjdzie mój umiłowany do swego ogrodu i niech je swoje rozkoszne owoce.

< Wimbo wa Sulemani 4 >