< Warumi 8 >

1 Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu ya adhabu kwa wale walio ndani ya Kristo Yesu, wale ambao hawaenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.
There is therefore now no condemnation to those who are in Christ Jesus;
2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima katika Kristo Yesu imeniweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti.
for the Spirit's Law-- telling of Life in Christ Jesus--has set me free from the Law that deals only with sin and death.
3 Kwa maana kile ambacho sheria haikuwa na uwezo wa kufanya, kwa vile ilivyokuwa dhaifu katika mwili, Mungu kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe kwa mfano wa mwanadamu mwenye mwili ulio wa dhambi na kwa ajili ya dhambi, yeye aliihukumu dhambi katika mwili,
For what was impossible to the Law--powerless as it was because it acted through frail humanity--God effected. Sending His own Son in a body like that of sinful human nature and as a sacrifice for sin, He pronounced sentence upon sin in human nature;
4 ili kwamba haki ipatikanayo kwa sheria itimizwe ndani yetu sisi, ambao hatuenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.
in order that in our case the requirements of the Law might be fully met. For our lives are regulated not by our earthly, but by our spiritual natures.
5 Kwa maana wale wanaoishi kwa kuufuata mwili huziweka nia zao katika vitu vya mwili, lakini wale wanaoishi kwa kufuata Roho, huziweka nia zao katika mambo ya Roho.
For if men are controlled by their earthly natures, they give their minds to earthly things. If they are controlled by their spiritual natures, they give their minds to spiritual things.
6 Kwa maana kuwa na nia ya mwili ni mauti, bali kuwa na nia inayoongozwa na Roho ni uzima na amani.
Because for the mind to be given up to earthly things means death; but for it to be given up to spiritual things means Life and peace.
7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui na Mungu, kwa maana haiitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
Abandonment to earthly things is a state of enmity to God. Such a mind does not submit to God's Law, and indeed cannot do so.
8 Wale wanaotawaliwa na mwili, hawawezi kumpendeza Mungu.
And those whose hearts are absorbed in earthly things cannot please God.
9 Lakini ninyi, hamtawaliwi na mwili, bali na Roho, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Mtu yeyote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo.
You, however, are not devoted to earthly, but to spiritual things, if the Spirit of God is really dwelling in you; whereas if any man has not the Spirit of Christ, such a one does not belong to Him.
10 Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, miili yenu imekufa kwa sababu ya dhambi, lakini roho zenu zi hai kwa sababu ya haki.
But if Christ is in you, though your body must die because of sin, yet your spirit has Life because of righteousness.
11 Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
And if the Spirit of Him who raised up Jesus from the dead is dwelling in you, He who raised up Christ from the dead will give Life also to your mortal bodies because of His Spirit who dwells in you.
12 Kwa hiyo ndugu zangu, sisi tu wadeni, si wa mwili, ili tuishi kwa kuufuata mwili,
Therefore, brethren, it is not to our lower natures that we are under obligation that we should live by their rule.
13 kwa maana mkiishi kwa kuufuata mwili, mtakufa, lakini kama mkiyaua matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.
For if you so live, death is near; but if, through being under the sway of the spirit, you are putting your old bodily habits to death, you will live.
14 Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio watoto wa Mungu.
For those who are led by God's Spirit are, all of them, God's sons.
15 Kwa maana hamkupokea roho ya utumwa iwaleteayo tena hofu, bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambaye kwa yeye twalia, “Abba, yaani, Baba,”
You have not for the second time acquired the consciousness of being--a consciousness which fills you with terror. But you have acquired a deep inward conviction of having been adopted as sons--a conviction which prompts us to cry aloud, "Abba! our Father!"
16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kwamba sisi tu watoto wa Mungu.
The Spirit Himself bears witness, along with our own spirits, to the fact that we are children of God;
17 Hivyo, ikiwa sisi ni watoto, basi tu warithi, warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo, naam, tukiteswa pamoja naye tupate pia kutukuzwa pamoja naye.
and if children, then heirs too--heirs of God and co-heirs with Christ; if indeed we are sharers in Christ's sufferings, in order that we may also be sharers in His glory.
18 Nayahesabu mateso yetu ya wakati huu kuwa si kitu kulinganisha na utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
Why, what we now suffer I count as nothing in comparison with the glory which is soon to be manifested in us.
19 Kwa maana viumbe vyote vinangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa watoto wa Mungu.
For all creation, gazing eagerly as if with outstretched neck, is waiting and longing to see the manifestation of the sons of God.
20 Kwa kuwa viumbe vyote viliwekwa chini ya ubatili, si kwa chaguo lao, bali kwa mapenzi yake yeye aliyevitiisha katika tumaini,
For the Creation fell into subjection to failure and unreality (not of its own choice, but by the will of Him who so subjected it).
21 ili kwamba viumbe vyote vipate kuwekwa huru kutoka kwa utumwa wa kuharibika na kupewa uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
Yet there was always the hope that at last the Creation itself would also be set free from the thraldom of decay so as to enjoy the liberty that will attend the glory of the children of God.
22 Kwa maana twajua ya kuwa hata sasa viumbe vyote vimekuwa vikilia kwa maumivu kama utungu wa mwanamke wakati wa kuzaa.
For we know that the whole of Creation is groaning together in the pains of childbirth until this hour.
23 Wala si hivyo viumbe peke yao, bali hata sisi ambao ndio matunda ya kwanza ya Roho, kwa ndani tunalia kwa uchungu tukisubiri kwa shauku kufanywa wana wa Mungu, yaani, ukombozi wa miili yetu.
And more than that, we ourselves, though we possess the Spirit as a foretaste and pledge of the glorious future, yet we ourselves inwardly sigh, as we wait and long for open recognition as sons through the deliverance of our bodies.
24 Kwa kuwa tuliokolewa kwa tumaini hili. Lakini kama kinachotumainiwa kikionekana hakiwi tumaini tena. Je, kuna mtu anayetumaini kupata kitu alicho nacho tayari?
It is in hope that we have been saved. But an object of hope is such no longer when it is present to view; for when a man has a thing before his eyes, how can he be said to hope for it?
25 Lakini tunapotumaini kupata kitu ambacho hatuna, basi twakingojea kwa saburi.
But if we hope for something which we do not see, then we eagerly and patiently wait for it.
26 Vivyo hivyo, Roho hutusaidia katika udhaifu wetu, kwa sababu hatujui kuomba ipasavyo. Lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa uchungu usioweza kutamkwa.
In the same way the Spirit also helps us in our weakness; for we do not know what prayers to offer nor in what way to offer them. But the Spirit Himself pleads for us in yearnings that can find no words,
27 Naye Mungu aichunguzaye mioyo, anaijua nia ya Roho, kwa sababu Roho huwaombea watakatifu sawasawa na mapenzi ya Mungu.
and the Searcher of hearts knows what the Spirit's meaning is, because His intercessions for God's people are in harmony with God's will.
28 Nasi tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja na wote wampendao, katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
Now we know that for those who love God all things are working together for good--for those, I mean, whom with deliberate purpose He has called.
29 Maana wale Mungu aliowajua tangu mwanzo, pia aliwachagua tangu mwanzo, wapate kufanana na mfano wa Mwanawe, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
For those whom He has known beforehand He has also pre-destined to bear the likeness of His Son, that He might be the Eldest in a vast family of brothers;
30 Nao wale Mungu aliotangulia kuwachagua, akawaita, wale aliowaita pia akawahesabia haki, nao wale aliowahesabia haki, pia akawatukuza.
and those whom He has pre-destined He also has called; and those whom He has called He has also declared free from guilt; and those whom He has declared free from guilt He has also crowned with glory.
31 Tuseme nini basi kuhusu haya? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, ni nani awezaye kuwa kinyume chetu?
What then shall we say to this? If God is on our side, who is there to appear against us?
32 Ikiwa Mungu hakumhurumia Mwanawe, bali alimtoa kwa ajili yetu sote, atakosaje basi kutupatia vitu vyote kwa ukarimu pamoja naye?
He who did not withhold even His own Son, but gave Him up for all of us, will He not also with Him freely give us all things?
33 Ni nani atakayewashtaki wale ambao Mungu amewateua? Ni Mungu mwenyewe ndiye mwenye kuwahesabia haki.
Who shall impeach those whom God has chosen? God declares them free from guilt.
34 Ni nani basi atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu aliyekufa, naam, zaidi ya hayo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yuko mkono wa kuume wa Mungu, naye pia anatuombea.
Who is there to condemn them? Christ Jesus died, or rather has risen to life again. He is also at the right hand of God, and is interceding for us.
35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni shida au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga?
Who shall separate us from Christ's love? Shall affliction or distress, persecution or hunger, nakedness or danger or the sword?
36 Kama ilivyoandikwa: “Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”
As it stands written in the Scripture, "For Thy sake they are, all day long, trying to kill us. We have been looked upon as sheep destined for slaughter."
37 Lakini katika mambo haya yote tunashinda, naam na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.
Yet amid all these things we are more than conquerors through Him who has loved us.
38 Kwa maana nimekwisha kujua kwa hakika ya kuwa sio mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuja, wala wenye uwezo,
For I am convinced that neither death nor life, neither the lower ranks of evil angels nor the higher, neither things present nor things future, nor the forces of nature,
39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine chochote zitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu, Bwana wetu.
nor height nor depth, nor any other created thing, will be able to separate us from the love of God which rests upon us in Christ Jesus our Lord.

< Warumi 8 >