< Ufunuo 6 >

1 Kisha nikaangalia wakati Mwana-Kondoo akivunja ile lakiri ya kwanza miongoni mwa zile saba. Ndipo nikasikia mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akisema kwa sauti kama ya radi: “Njoo!”
And when the Lamb broke one of the seven seals I saw it, and I heard one of the four living creatures say, as if in a voice of thunder, "Come."
2 Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mweupe! Yeye aliyempanda alikuwa na upinde, naye akapewa taji, akampanda akatoka akiwa kama mshindi aelekeaye katika kushinda.
And I looked and a white horse appeared, and its rider carried a bow; and a victor's wreath was given to him; and he went out conquering and in order to conquer.
3 Alipoivunja ile lakiri ya pili, nikamsikia yule kiumbe wa pili mwenye uhai akisema, “Njoo!”
And when the Lamb broke the second seal, I heard the second living creature say, "Come."
4 Ndipo akatokea farasi mwingine mwekundu sana. Yeye aliyempanda akapewa uwezo wa kuondoa amani duniani na kuwafanya watu wauane. Yeye akapewa upanga mkubwa.
And another horse came out--a fiery-red one; and power was given to its rider to take peace from the earth, and to cause men to kill one another; and a great sword was given to him.
5 Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tatu, nikamsikia yule kiumbe wa tatu mwenye uhai akisema, “Njoo!” Nikatazama, na mbele yangu alikuwepo farasi mweusi! Yeye aliyempanda alikuwa na mizani mkononi mwake.
When the Lamb broke the third seal, I heard the third living creature say, "Come." I looked, and a black horse appeared, its rider carrying a balance in his hand.
6 Ndipo nikasikia kile kilichokuwa kama sauti katikati ya wale viumbe wanne wenye uhai ikisema, “Kipimo kimoja cha ngano kwa mshahara wa kibarua wa siku moja, na vipimo vitatu vya shayiri kwa mshahara wa kibarua cha siku moja. Lakini usiharibu mafuta wala divai!”
And I heard what seemed to be a voice speaking in the midst of the four living creatures, and saying, "A quart of wheat for a shilling, and three quarts of barley for a shilling; but do not injure either the oil or the wine."
7 Alipovunja ile lakiri ya nne, nikasikia sauti ya yule kiumbe wa nne mwenye uhai ikisema, “Njoo!”
When the Lamb broke the fourth seal I heard the voice of the fourth living creature say, "Come."
8 Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mwenye rangi ya kijivujivu! Yeye aliyempanda aliitwa Mauti, naye Kuzimu alikuwa akimfuata nyuma yake kwa karibu. Wakapewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia. (Hadēs g86)
I looked and a pale-colored horse appeared. Its rider's name was Death, and Hades came close behind him; and authority was given to them over the fourth part of the earth, to kill with the sword or with famine or pestilence or by means of the wild beasts of the earth. (Hadēs g86)
9 Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tano, nikaona chini ya madhabahu, roho za wale waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu na kwa ajili ya ushuhuda walioutunza.
When the Lamb broke the fifth seal, I saw at the foot of the altar the souls of those whose lives had been sacrificed because of the word of God and of the testimony which they had given.
10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, “Hata lini, Ee Bwana Mwenyezi, uliye mtakatifu na mwaminifu, hutawahukumu na kulipiza kisasi juu ya watu waishio duniani kwa ajili ya damu yetu?”
And now in loud voices they cried out, saying, "How long, O Sovereign Lord, the holy One and the true, dost Thou delay judgment and the taking of vengeance upon the inhabitants of the earth for our blood?"
11 Kisha kila mmoja wao akapewa joho jeupe na wakaambiwa wangoje kwa muda kidogo zaidi, mpaka idadi ya ndugu zao na watumishi wenzao watakaouawa kama wao walivyouawa, itakapotimia.
And there was given to each of them a long white robe, and they were bidden to wait patiently for a short time longer, until the full number of their fellow bondservants should also complete--namely of their brethren who were soon to be killed just as they had been.
12 Nikatazama akiivunja ile lakiri ya sita. Pakatokea tetemeko kuu la nchi, na jua likawa jeusi kama nguo ya gunia iliyotengenezwa kwa singa za mbuzi, na mwezi wote ukawa mwekundu kama damu.
When the Lamb broke the sixth seal I looked, and there was a great earthquake, and the sun became as dark as sackcloth, and the whole disc of the moon became like blood.
13 Nyota zilizo angani zikaanguka ardhini kama vile matunda ya mtini yasiyokomaa yaangukavyo wakati mti wake unapotikiswa na upepo mkali.
The stars in the sky also fell to the earth, as when a fig-tree, upon being shaken by a gale of wind, casts its unripe figs to the ground.
14 Anga ikatoweka kama vile karatasi isokotwavyo, na kila mlima na kila kisiwa kikaondolewa mahali pake.
The sky too passed away, as if a scroll were being rolled up, and every mountain and island was removed from its place.
15 Ndipo wafalme wa dunia, wakuu wote, majemadari, matajiri, wenye nguvu na kila mtu, mtumwa na mtu huru, wakajificha katika mapango na kwenye miamba ya milima.
The kings of the earth and the great men, the military chiefs, the wealthy and the powerful--all, whether slaves or free men--hid themselves in the caves and in the rocks of the mountains,
16 Wakaiita milima na miamba wakisema, “Tuangukieni, mkatufiche na uso wake yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na mkatuepushe na ghadhabu ya Mwana-Kondoo!
while they called to the mountains and the rocks, saying, "Fall on us and hide us from the presence of Him who sits on the throne and from the anger of the Lamb;
17 Kwa maana siku ile kuu ya ghadhabu yao imewadia. Je, ni nani awezaye kustahimili?”
for the day of His anger--that great day--has come, and who is able to stand?"

< Ufunuo 6 >