< Ufunuo 21 >

1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza vimekwisha kupita, wala hapakuwepo na bahari tena.
And I saw a new Heaven and a new earth; for the first Heaven and the first earth were gone, and the sea no longer exists.
2 Nikaona Mji Mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa umeandaliwa kama bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
And I saw the holy city, the new Jerusalem, coming down out of Heaven from God and made ready like a bride attired to meet her husband.
3 Nami nikasikia sauti kubwa kutoka kile kiti cha enzi ikisema, “Sasa makao ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao. Yeye atakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wake, naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
And I heard a loud voice, which came from the throne, say, "God's dwelling place is among men and He will dwell among them and they shall be His peoples. Yes, God Himself will be among them.
4 Atafuta kila chozi kutoka macho yao. Mauti haitakuwepo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu, kwa maana mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”
He will wipe every tear from their eyes. Death shall be no more; nor sorrow, nor wail of woe, nor pain; for the first things have passed away."
5 Naye yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi akasema, “Tazama, nayafanya mambo yote kuwa mapya!” Kisha akasema, “Andika haya, maana maneno haya ni ya kuaminika tena ni kweli.”
Then He who was seated on the throne said, "I am re-creating all things." And He added, "Write down these words, for they are trustworthy and true."
6 Akaniambia, “Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Yeye aonaye kiu nitampa kunywa kutoka chemchemi ya maji ya uzima bila gharama yoyote.
He also said, "They have now been fulfilled. I am the Alpha and the Omega, the Beginning and the End. To those who are thirsty I will give the privilege of drinking from the well of the Water of Life without payment.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya yote, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
All this shall be the heritage of him who overcomes, and I will be his God and he shall be one of My sons.
8 Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr g3041 g4442)
But as for cowards and the unfaithful, and the polluted, and murderers, fornicators, and those who practise magic or worship idols, and all liars--the portion allotted to them shall be in the Lake which burns with fire and sulphur. This is the Second Death." (Limnē Pyr g3041 g4442)
9 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba ya hayo mapigo saba ya mwisho akaja akaniambia, “Njoo, nami nitakuonyesha bibi arusi, yaani, mke wa Mwana-Kondoo.”
Then there came one of the seven angels who were carrying the seven bowls full of the seven last plagues. "Come with me," he said, "and I will show you the Bride, the Lamb's wife."
10 Naye akanichukua katika Roho hadi kwenye mlima mkubwa na mrefu, akanionyesha ule Mji Mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu.
So in the Spirit he carried me to the top of a vast, lofty mountain, and showed me the holy city, Jerusalem, coming down out of Heaven from God,
11 Ulikuwa ukingʼaa kwa utukufu wa Mungu kama kito chenye thamani sana, kama yaspi, safi kama kioo.
and bringing with it the glory of God. It shone with a radiance like that of a very precious stone--such as a jasper, bright and transparent.
12 Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye malango kumi na mawili, pakiwa na malaika kumi na wawili kwenye hayo malango. Kwenye malango hayo yaliandikwa majina ya yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
It has a wall, massive and high, with twelve large gates, and in charge of the gates were twelve angels. And overhead, above the gates, names were inscribed which are those of the twelve tribes of the descendants of Israel.
13 Kulikuwa na malango matatu upande wa mashariki, matatu upande wa kaskazini, matatu upande wa kusini na matatu upande wa magharibi.
There were three gates on the east, three on the north, three on the south, and three on the west.
14 Ukuta wa huo mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake yaliandikwa majina ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.
The wall of the city had twelve foundation stones, and engraved upon them were twelve names--the names of the twelve Apostles of the Lamb.
15 Huyo malaika aliyesema nami alikuwa na ufito wa dhahabu wa kupimia huo mji, malango yake na kuta zake.
Now he who was speaking to me had a measuring-rod of gold, with which to measure the city and its gates and its wall.
16 Mji huo ulikuwa mraba, urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Akaupima huo mji kwa huo ufito akakuta una kama kilomita 2,200; urefu wake na upana wake na kwenda juu kwake vilikuwa sawa.
The plan of the city is a square, the length being the same as the breadth; and he measured the city furlong by furlong, with his measuring rod--it is twelve hundred miles long, and the length and the breadth and the height of it are equal.
17 Akaupima ukuta wake, ulikuwa na unene wa dhiraa 144 kwa kipimo cha kibinadamu ambacho huyo malaika alikuwa akikitumia.
And he measured the wall of it--a wall of a hundred and forty-four cubits, according to human measure, which was also that of the angel.
18 Ukuta huo ulijengwa kwa yaspi hali mji wenyewe ulijengwa kwa dhahabu safi, ikingʼaa kama kioo.
The solid fabric of the wall was jasper; and the city itself was made of gold, resembling transparent glass.
19 Misingi ya kuta za mji huo zilipambwa kwa kila aina ya kito cha thamani. Msingi wa kwanza ulikuwa wa yaspi, wa pili yakuti samawi, wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi,
As for the foundation-stones of the city wall, which were beautified with various kinds of precious stones, the first was jasper, the second sapphire, the third chalcedony, the fourth emerald, the fifth sardonyx, the sixth sardius,
20 wa tano sardoniki, wa sita akiki, wa saba krisolitho, wa nane zabarajadi, wa tisa yakuti manjano, wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hiakintho, wa kumi na mbili amethisto.
the seventh chrysolite, the eighth beryl, the ninth topaz, the tenth chrysoprase, the eleventh jacinth, the twelfth amethyst.
21 Yale malango kumi na mbili yalikuwa ni lulu kumi na mbili, kila lango lilikuwa limetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji huo ilikuwa ya dhahabu safi ingʼaayo kama kioo.
And the twelve gates were twelve pearls; each of them consisting of a single pearl. And the main street of the city was made of pure gold, resembling transparent glass.
22 Sikuona Hekalu ndani ya huo mji kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio hekalu lake.
I saw no sanctuary in the city, for the Lord God, the Ruler of all, is its Sanctuary, and so is the Lamb.
23 Ule mji hauhitaji jua wala mwezi kuuangazia, kwa sababu utukufu wa Mungu ndio nuru yake na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.
Nor has the city any need of the sun or of the moon, to give it light; for the glory of God has shone upon it and its lamp is the Lamb.
24 Mataifa yatatembea yakiangaziwa na nuru yake na wafalme wa duniani wataleta fahari yao ndani yake.
The nations will live their lives by its light; and the kings of the earth are to bring their glory into it.
25 Malango yake hayatafungwa kamwe, kwa maana hakutakuwa na usiku humo.
And in the daytime (for there will be no night there) the gates will never be closed;
26 Utukufu na heshima za mataifa zitaletwa humo.
and the glory and honor of the nations shall be brought into it.
27 Lakini kitu kichafu hakitaingia humo kamwe, wala mtu yeyote atendaye mambo ya aibu au ya udanganyifu. Bali watakaoingia humo ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.
And no unclean thing shall ever enter it, nor any one who is guilty of base conduct or tells lies, but only they whose names stand recorded in the Lamb's Book of Life.

< Ufunuo 21 >