< Ufunuo 2 >

1 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika: “Haya ndiyo maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu.
"To the minister of the Church in Ephesus write as follows: "'This is what He who holds the seven stars in the grasp of His right hand says--He who walks to and fro among the seven lampstands of gold.
2 Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo.
I know your doings and your toil and patient suffering. And I know that you cannot tolerate wicked men, but have put to the test those who say that they themselves are Apostles but are not, and you have found them to be liars.
3 Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.
And you endure patiently and have borne burdens for My sake and have never grown weary.
4 “Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza.
Yet I have this against you--that you no longer love Me as you did at first.
5 Kumbuka basi ni wapi ulikoangukia! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake.
Be mindful, therefore, of the height from which you have fallen. Repent at once, and act as you did at first, or else I will surely come and remove your lampstand out of its place--unless you repent.
6 Lakini una jambo hili kwa upande wako: Unayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo nami pia nayachukia.
Yet this you have in your favor: you hate the doings of the Nicolaitans, which I also hate.
7 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa haki ya kula matunda toka kwa mti wa uzima, ambao uko katika paradisoya Mungu.
"'Let all who have ears give heed to what the Spirit is saying to the Churches. To him who overcomes I will give the privilege of eating the fruit of the Tree of Life, which is in the Paradise of God.'
8 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye wa Kwanza na wa Mwisho, aliyekufa kisha akafufuka.
"To the minister of the Church at Smyrna write as follows: "'This is what the First and the Last says--He who died and has returned to life.
9 Naijua dhiki yako na umaskini wako, lakini wewe ni tajiri! Nayajua masingizio ya wale wasemao kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali wao ni sinagogi la Shetani.
Your sufferings I know, and your poverty--but you are rich--and the evil name given you by those who say that they themselves are Jews, and are not, but are Satan's synagogue.
10 Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia ibilisi atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.
Dismiss your fears concerning all that you are about to suffer. I tell you that the Devil is about to throw some of you into prison that you may be put to the test, and for ten days you will have to endure persecution. Be faithful to the End, even if you have to die, and then I will give you the victor's Wreath of Life.
11 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatadhuriwa kamwe na mauti ya pili.
"'Let all who have ears give heed to what the Spirit is saying to the Churches. He who overcomes shall be in no way hurt by the Second Death.'
12 “Kwa malaika wa Kanisa lililoko Pergamo andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili.
"To the minister of the Church at Pergamum write as follows: "'This is what He who has the sharp, two-edged sword says. I know where you dwell.
13 Ninajua unakoishi, ni kule ambako Shetani ana kiti chake cha enzi. Lakini umelishika Jina langu. Wala hukuikana imani yako kwangu hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji mkuu wenu, ambako ndiko anakoishi Shetani.
Satan's throne is there; and yet you are true to Me, and did not deny your faith in Me, even in the days of Antipas My witness and faithful friend, who was put to death among you, in the place where Satan dwells.
14 “Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako: Unao watu wafuatao mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki kuwashawishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa kafara kwa sanamu na kufanya uasherati.
Yet I have a few things against you, because you have with you some that cling to the teaching of Balaam, who taught Balak to put a stumbling-block in the way of the descendants of Israel--to eat what had been sacrificed to idols, and commit fornication.
15 Vivyo hivyo unao wale wayashikayo mafundisho ya Wanikolai.
So even you have some that cling in the same way to the teaching of the Nicolaitans.
16 Basi tubu! Ama sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga wa kinywa changu.
Repent, at once; or else I will come to you quickly, and will make war upon them with the sword which is in My mouth.
17 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa. Nitampa pia jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea.
"'Let all who have ears give heed to what the Spirit is saying to the Churches. He who overcomes--to him I will give some of the hidden Manna, and a white stone; and--written upon the stone and known only to him who receives it-- a new name.'
18 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika: “Haya ndiyo maneno ya Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto na ambaye miguu yake ni kama shaba iliyosuguliwa sana.
"To the minister of the Church at Thyateira write as follows: "'This is what the Son of God says--He who has eyes like a flame of fire, and feet resembling silver-bronze.
19 Nayajua matendo yako, upendo wako na imani yako, huduma na saburi yako na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya kwanza.
I know your doings, your love, your faith, your service, and your patient endurance; and that of late you have toiled harder than you did at first.
20 “Hata hivyo, nina neno dhidi yako: Unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu ili wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa kafara kwa sanamu.
Yet I have this against you, that you tolerate the woman Jezebel, who calls herself a prophetess and by her teaching leads astray My servants, so that they commit fornication and eat what has been sacrificed to idols.
21 Nimempa muda ili atubu kwa ajili ya uasherati wake, lakini hataki.
I have given her time to repent, but she is determined not to repent of her fornication.
22 Kwa hiyo nitamtupa kwenye kitanda cha mateso, na nitawafanya hao wanaozini naye kupata mateso makali wasipotubia njia zake.
I tell you that I am about to cast her upon a bed of sickness, and I will severely afflict those who commit adultery with her, unless they repent of conduct such as hers.
23 Nami nitawaua watoto wake. Nayo makanisa yote yatajua kwamba Mimi ndiye nichunguzaye mioyo na nia, na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
Her children too shall surely die; and all the Churches shall come to know that I am He who searches into men's inmost thoughts; and to each of you I will give a requital which shall be in accordance with what your conduct has been.
24 Basi nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamyafuati mafundisho ya Yezebeli, wala hamkujifunza hayo yanayoitwa mambo ya ndani sana ya Shetani (sitaweka mzigo mwingine wowote juu yenu):
But to you, the rest of you in Thyateira, all who do not hold this teaching and are not the people who have learnt the "deep things," as they call them (the deep things of Satan!) --to you I say that I lay no other burden on you.
25 Lakini shikeni sana mlicho nacho, mpaka nitakapokuja.
Only that which you already possess, cling to until I come.
26 “Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa:
"'And to him who overcomes and obeys My commands to the very end, I will give authority over the nations of the earth.
27 “‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma, atawavunja vipande vipande kama chombo cha udongo’: kama vile mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu.
And he shall be their shepherd, ruling them with a rod of iron, just as earthenware jars are broken to pieces; and his power over them shall be like that which I Myself have received from My Father;
28 Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi.
and I will give him the Morning Star.
29 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
Let all who have ears give heed to what the Spirit is saying to the Churches.'

< Ufunuo 2 >