< Ufunuo 18 >

1 Baada ya haya nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, akiwa na mamlaka makuu na dunia ikamulikiwa na mngʼao wake.
After these things I saw another angel coming down from Heaven, armed with great power. The earth shone with his splendor,
2 Naye akalia kwa nguvu kwa sauti kubwa, akisema: “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu! Umekuwa makao ya mashetani na makazi ya kila pepo mchafu, makazi ya kila ndege na kila mnyama achukizaye.
and with a mighty voice he cried out, saying, "Great Babylon has fallen, has fallen, and has become a home for demons and a stronghold for every kind of foul spirit and for every kind of foul and hateful bird.
3 Kwa maana mataifa yote yamekunywa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake. Nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi nao, nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.”
For all the nations have drunk the wine of the anger provoked by her fornication, and the kings of the earth have committed fornication with her, and the merchants of the earth have grown rich through her excessive luxury."
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: “Tokeni katikati yake, enyi watu wangu, ili msije mkashiriki dhambi zake, ili msije mkapatwa na pigo lake lolote;
Then I heard another voice from Heaven, which said, "Come out of her, My people, that you may not become partakers in her sins, nor receive a share of her plagues.
5 kwa kuwa dhambi zake zimelundikana hadi mbinguni, naye Mungu ameukumbuka uhalifu wake.
For her sins are piled up to the sky, and God has called to mind her unrighteous deeds.
6 Mtendee kama yeye alivyotenda; umlipe mara mbili kwa ajili ya yale aliyotenda. Katika kikombe chake mchanganyie mara mbili ya kile alichochanganya.
Give back to her as she has given; repay her in accordance with her doings, twice as much; in the bowl that she has mixed, mix twice as much for her.
7 Mpatie mateso na huzuni nyingi sawa na utukufu na anasa alizojipatia. Kwa kuwa moyoni mwake hujivuna, akisema, ‘Mimi ninatawala kama malkia; mimi si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.’
She has freely glorified herself and revelled in luxury; equally freely administer torment to her, and woe. For in her heart she boasts, saying, 'I sit enthroned as Queen: no widow am I: I shall never know sorrow.'
8 Kwa hiyo mapigo yatampata kwa siku moja: mauti, maombolezo na njaa. Naye atateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana Mungu amhukumuye ana nguvu.
"For this reason calamities shall come thick upon her on a single day--death and sorrow and famine--and she shall be burned to the ground. For strong is the Lord God who has judged her.
9 “Wafalme wa dunia waliozini naye na kushiriki anasa zake watakapoona moshi wa kuungua kwake, watamlilia na kumwombolezea.
The kings of the earth who have committed fornication with her, and have revelled in luxury, shall weep aloud and lament over her when they see the smoke of her burning,
10 Kwa hofu kubwa ya mateso yake, watasimama mbali na kulia na wakisema: “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, ee Babeli mji wenye nguvu! Hukumu yako imekuja katika saa moja!’
while they stand afar off because of their terror at her heavy punishment, and say, 'Alas, alas, thou great city, O Babylon, the mighty city! For in one short hour thy doom has come!'
11 “Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumwomboleza kwa sababu hakuna anunuaye bidhaa zao tena:
And the merchants of the earth weep aloud and lament over her, because now there is no sale for their cargoes--
12 Bidhaa za dhahabu, za fedha, za vito vya thamani na vya lulu, kitani safi, nguo za rangi ya zambarau, hariri, nguo nyekundu, aina zote za miti ya udi, na vifaa vyote vya pembe za ndovu, vifaa vyote vya miti yenye thamani kuliko yote, shaba, chuma na marmar,
cargoes of gold and silver, of jewels and pearls, of fine linen, purple and silk, and of scarlet stuff; all kinds of rare woods, and all kinds of goods in ivory and in very costly wood, in bronze, steel and marble.
13 bidhaa za mdalasini, vikolezi, za uvumba, manemane, na uvumba wenye harufu nzuri, za divai, na mafuta ya zeituni, za unga mzuri na ngano; ngʼombe na kondoo; farasi na magari; na miili na roho za wanadamu.
Also cinnamon and amomum; odors to burn as incense or for perfume; frankincense, wine, oil; fine flour, wheat, cattle and sheep; horses and carriages and slaves; and the lives of men.
14 “Watasema, ‘Yale matunda ambayo roho yako iliyatamani yamekoma. Utajiri wako wote na fahari yako vimetoweka, wala haviwezi kupatikana tena kamwe!’
The dainties that thy soul longed for are gone from thee, and all thine elegance and splendor have perished, and never again shall they be found.
15 Wale wafanyabiashara waliotajirika kwa bidhaa hizo kutoka kwake watasimama mbali naye kwa hofu kubwa ya mateso yanayompata. Watalia na kuomboleza wakipiga kelele wakisema:
Those who traded in these things, who grew wealthy through her, will stand afar off, struck with terror at her punishment,
16 “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, uliyekuwa umevikwa mavazi ya kitani safi, ya rangi ya zambarau na nyekundu, ukimetameta kwa dhahabu, vito vya thamani na lulu!
weeping aloud and sorrowing, and saying, 'Alas, alas, for this great city, which was brilliantly arrayed in fine linen, and purple and scarlet stuff, and beautified with gold, jewels and pearls;
17 Katika muda wa saa moja utajiri wote mkubwa kama huu umeangamia!’ “Kila nahodha, na wote wasafirio kwa meli, na wote wapatao kipato chao kutokana na bahari, watasimama mbali.
because in one short hour all this great wealth has been laid waste!' And every shipmaster and every passenger by sea and the crews and all who ply their trade on the sea,
18 Watakapouona moshi wa kuungua kwake watalia wakisema, ‘Je, kulipata kuwako mji mkubwa kama huu?’
stood afar off, and cried aloud when they saw the smoke of her burning. And they said, 'What city is like this great city?'
19 Nao watajirushia mavumbi vichwani mwao, huku wakilia na kuomboleza, wakisema: “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, mji ambao wote wenye meli baharini walitajirika kupitia kwa mali zake! Katika saa moja tu ameangamizwa!
And they threw dust upon their heads, and cried out, weeping aloud and sorrowing. 'Alas, alas,' they said, 'for this great city, in which, through her vast wealth, the owners of all the ships on the sea have grown rich; because in one short hour she has been laid waste!'
20 Furahia kwa ajili yake, ee mbingu! Furahini watakatifu, mitume na manabii! Mungu amemhukumu kwa vile alivyowatendea ninyi.’”
Rejoice over her, O Heaven, and you saints and Apostles and Prophets; for God has taken vengeance upon her because of you."
21 Kisha malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe kubwa kama la kusagia akalitupa baharini akisema: “Hivyo ndivyo mji mkubwa Babeli utakavyotupwa chini kwa nguvu wala hautaonekana tena.
Then a single angel of great strength took a stone which resembled a huge millstone, and hurled it into the sea, saying, "So shall Babylon, that great city, be violently hurled down and never again be found.
22 Nyimbo za wapiga vinubi na waimbaji, wapiga filimbi na wapiga tarumbeta kamwe hazitasikika tena ndani yako. Ndani yako kamwe hataonekana tena fundi mwenye ujuzi wa aina yoyote. Wala sauti ya jiwe la kusagia kamwe haitasikika tena.
No harp or song, no flute or trumpet, shall ever again be heard in thee; no craftsman of any kind shall ever again be found in thee; nor shall the grinding of the mill ever again be heard in thee.
23 Mwanga wa taa hautaangaza ndani yako tena. Sauti ya bwana arusi na bibi arusi kamwe haitasikika ndani yako tena. Wafanyabiashara wako walikuwa watu maarufu wa dunia. Mataifa yote yalipotoshwa kwa uchawi wako.
Never again shall the light of a lamp shine in thee, and never again shall the voice of a bridegroom or of a bride be heard in thee. For thy merchants were the great men of the earth, and with the magic which thou didst practise all nations were led astray.
24 Ndani yake ilionekana damu ya manabii na ya watakatifu na wote waliouawa duniani.”
And in her was found the blood of Prophets and of God's people and of all who had been put to death on the earth."

< Ufunuo 18 >