< Ufunuo 14 >

1 Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao.
Then I looked, and I saw the Lamb standing upon Mount Zion, and with Him 144,000 people, having His name and His Father's name written on their foreheads.
2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao.
And I heard music from Heaven which resembled the sound of many waters and the roar of loud thunder; and the music which I heard was like that of harpists playing upon their harps.
3 Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani.
And they were singing what seemed to be a new song, in front of the throne and in the presence of the four living creatures and the Elders; and no one was able to learn that song except the 144,000 people who had been redeemed out of the world.
4 Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
These are those who had not defiled themselves with women: they are as pure as virgins. They follow the Lamb wherever He goes. They have been redeemed from among men, as firstfruits to God and to the Lamb.
5 Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.
And no lie has ever been found upon their lips: they are faultless.
6 Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. (aiōnios g166)
And I saw another angel flying across the sky, carrying the Good News of the Ages to tell to every nation, tribe, language and people, among those who live on the earth. (aiōnios g166)
7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”
He said in a loud voice, "Fear God and give Him glory, because the time of His judgment has come; and worship Him who made sky and earth, the sea and the water-springs."
8 Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”
And another, a second angel, followed, exclaiming, "Great Babylon has fallen, has fallen--she who made all the nations drink the wine of the anger provoked by her fornication."
9 Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake,
And another, a third angel, followed them, exclaiming in a loud voice, "If any one worships the Wild Beast and his statue, and receives a mark on his forehead or on his hand,
10 yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo.
he shall drink the wine of God's anger which stands ready, undiluted, in the cup of His fury, and he shall be tormented with fire and sulphur in the presence of the holy angels and of the Lamb.
11 Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” (aiōn g165)
And the smoke of their torment goes up until the Ages of the Ages; and the worshipers of the Wild Beast and his statue have no rest day or night, nor has any one who receives the mark of his name. (aiōn g165)
12 Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.
Here is an opportunity for endurance on the part of God's people, who carefully keep His commandments and the faith of Jesus!"
13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”
And I heard a voice speaking from Heaven. It said, "Write as follows: "'Blessed are the dead who die in the Lord from this time onward. Yes, says the Spirit, let them rest from their sorrowful labours; for what they have done goes with them.'"
14 Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake.
Then I looked, and a white cloud appeared, and sitting on the cloud was some One resembling the Son of Man, having a wreath of gold upon His head and in His hand a sharp sickle.
15 Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.”
And another, an angel, came out of the sanctuary, calling in a loud voice to Him who sat on the cloud, and saying, "Use your sickle and reap the harvest, for the hour for reaping it has come: the harvest of the earth is over-ripe."
16 Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.
Then He who sat on the cloud flung His sickle on the earth, and the earth had its harvest reaped.
17 Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali.
And another angel came out from the sanctuary in Heaven, and he too carried a sharp sickle.
18 Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”
And another angel came out from the altar--he who had power over fire--and he spoke in a loud voice to him who had the sharp sickle, saying, "Use your sharp sickle, and gather the bunches from the vine of the earth, for its grapes are now quite ripe."
19 Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
And the angel flung his sickle down to the earth, and reaped the vine of the earth and threw the grapes into the great winepress of God's anger.
20 Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi, kwa umbali wa maili 200.
And the winepress was trodden outside the city, and out of it came blood reaching the horses' bridles for a distance of 200 miles.

< Ufunuo 14 >