< Zaburi 78 >

1 Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Pieśń pouczająca. Asafa. Słuchaj, mój ludu, mego prawa, nakłońcie uszu ku słowom moich ust.
2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
Otworzę moje usta do przypowieści, opowiem starodawne tajemnice;
3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
Cośmy słyszeli i poznali i [co] nam opowiadali nasi ojcowie.
4 Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
Nie zataimy [tego] przed ich synami, opowiemy przyszłemu pokoleniu o chwale PANA, o jego mocy i cudach, które czynił.
5 Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
Ustanowił bowiem świadectwo w Jakubie, nadał prawo w Izraelu i nakazał naszym ojcom, aby je oznajmiali swoim synom;
6 ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
Aby poznało przyszłe pokolenie, synowie, którzy się urodzą; aby powstawszy, przekazywali [je] swoim synom;
7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
Żeby pokładali w Bogu nadzieję i nie zapominali o dziełach Boga, lecz strzegli jego przykazań;
8 Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
Żeby nie byli, jak ich ojcowie, pokoleniem opornym i nieposłusznym; pokoleniem, które nie przygotowało swego serca i którego duch nie był wierny Bogu.
9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
Synowie Efraima, uzbrojeni i wyposażeni w łuki, w dniu bitwy wycofali się.
10 Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
[Bo] nie strzegli przymierza Boga i nie chcieli postępować według jego prawa.
11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
Zapomnieli o jego dziełach i cudach, które im ukazał.
12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
Przed ich ojcami czynił cuda w ziemi Egiptu, na polu Soanu.
13 Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
Rozdzielił morze i przeprowadził ich, i sprawił, że wody stanęły jak wał.
14 Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
Prowadził ich w obłoku za dnia, a całą noc w blasku ognia.
15 Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
Rozszczepił skały na pustyni i napoił ich jakby z wielkich głębin.
16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
Wydobył strumienie ze skały i sprawił, że wody płynęły jak rzeki.
17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
Lecz [oni] jeszcze więcej grzeszyli przeciwko niemu i pobudzili do gniewu Najwyższego na pustyni;
18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
I wystawiali Boga na próbę w swych sercach, żądając pokarmu według swego pragnienia.
19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
I mówili przeciwko Bogu tymi słowy: Czy Bóg może zastawić stół na tej pustyni?
20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
Oto uderzył w skałę i wypłynęły wody, i wezbrały strumienie; czy będzie mógł też dać chleb? Czy przygotuje mięso swemu ludowi?
21 Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
Gdy PAN [to] usłyszał, rozgniewał się i ogień zapłonął przeciw Jakubowi, i gniew wybuchnął przeciw Izraelowi;
22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
Bo nie uwierzyli Bogu i nie zaufali jego zbawieniu;
23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
Choć rozkazał chmurom w górze i bramy nieba otworzył.
24 akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
I zesłał im [jak] deszcz mannę do jedzenia, i zboże z nieba im dał.
25 Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
Człowiek jadł chleb anielski; zesłał im pokarm do syta.
26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
Wzbudził na niebie wiatr ze wschodu i sprowadził swą mocą wiatr południowy.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
Zesłał im mięso jak pył i ptactwo skrzydlate jak piasek morski.
28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
Spadło ono pośrodku ich obozu, wokół ich namiotów.
29 Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
Jedli i w pełni się nasycili; dał im, czego pragnęli.
30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
[A gdy] jeszcze nie zaspokoili swego pragnienia, [gdy] jeszcze pokarm był w ich ustach;
31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
Spadł na nich gniew Boży i zabił ich tłustych, a znakomitszych z Izraela powalił.
32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
Mimo to nadal grzeszyli i nie wierzyli jego cudom;
33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
Dlatego sprawił, że ich dni przemijały w marności, a ich lata – w trwodze.
34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
Gdy ich zabijał, szukali go; nawracali się i o świcie szukali Boga;
35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
Przypominali sobie, że Bóg [jest] ich skałą, że Bóg Najwyższy – ich Odkupicielem;
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
Pochlebiali mu jednak swoimi ustami i okłamywali go swym językiem;
37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
A ich serce nie było przed nim szczere i nie byli wierni jego przymierzu.
38 Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
On jednak, będąc miłosiernym, przebaczał ich nieprawości i nie wytracał [ich]; często odwracał swój gniew i nie pobudzał całej swej zapalczywości;
39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
Bo pamiętał, że są ciałem; wiatrem, który ulatuje i nie wraca.
40 Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
Jak często pobudzali go do gniewu na pustyni [i] zasmucali go na pustkowiu!
41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
Odwracali się i wystawiali Boga na próbę, i stawiali granice Świętemu Izraela.
42 Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
Nie pamiętali jego ręki [ani] dnia, w którym ich wybawił z utrapienia;
43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
Gdy czynił swe znaki w Egipcie i swe cuda na polu Soanu;
44 Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
Gdy zamienił w krew ich rzeki i ich strumienie, tak że nie mogli [z nich] pić.
45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
Zesłał na nich rozmaite muchy, aby ich kąsały, i żaby, aby ich niszczyły;
46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
I dał robactwu ich plony, a ich pracę szarańczy.
47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
Zniszczył gradem ich winorośle, a sykomory szronem.
48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
Ich bydło wydał na pastwę gradu, a ich stada [na pastwę] błyskawic.
49 Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
Wylał na nich żar swojego gniewu, zapalczywość, oburzenie i udrękę, zesławszy na nich złych aniołów.
50 Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
Otworzył drogę dla swego gniewu, nie zachował ich duszy od śmierci, a ich życie wydał zarazie;
51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
Wytracił wszystko pierworodne w Egipcie, pierwociny [ich] mocy w namiotach Chama;
52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
Ale swój lud wyprowadził jak owce i wiódł ich po pustyni jak stado.
53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
Prowadził ich bezpiecznie, tak że się nie lękali, a ich wrogów przykryło morze;
54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
I przyprowadził ich do swej świętej granicy; do góry, którą nabyła jego prawica.
55 Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
Wypędził przed nimi narody, sznurem wyznaczył im dziedzictwo, żeby pokolenia Izraela mieszkały w swoich namiotach.
56 Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
Oni jednak wystawiali na próbę i pobudzali do gniewu Boga Najwyższego, i nie strzegli jego świadectw.
57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
Lecz odwrócili się i postępowali przewrotnie jak ich ojcowie, schodzili z drogi jak łuk zawodny.
58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
Pobudzali go bowiem do gniewu przez swe wyżyny i rzeźbionymi posągami wzbudzali jego zazdrość.
59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
Gdy Bóg [to] usłyszał, rozgniewał się i wielce wzgardził Izraelem.
60 Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
I opuścił przybytek w Szilo; namiot, [który] rozbił wśród ludzi;
61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
I oddał w niewolę swoją moc i swoją chwałę w ręce wroga.
62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
Wydał swój lud pod miecz i rozgniewał się na swoje dziedzictwo.
63 Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Ich młodzieńców pochłonął ogień, a ich dziewic nie wydano za mąż.
64 makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
Ich kapłani padli od miecza, a ich wdowy nie lamentowały.
65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
Lecz potem Pan ocknął się jak ze snu, jak mocarz wykrzykujący od wina.
66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
I uderzył na tyły swoich wrogów, okrył ich wieczną hańbą.
67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
Ale choć wzgardził namiotem Józefa i pokolenia Efraima nie wybrał;
68 lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
Jednak wybrał pokolenie Judy, górę Syjon, którą umiłował.
69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
I zbudował swoją świątynię jak wysoki [pałac]; jak ziemię, którą ugruntował na wieki.
70 Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
Wybrał też Dawida, swego sługę; wziął go z owczych zagród;
71 Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
Przywołał go, gdy chodził za karmiącymi [owcami], aby pasł Jakuba, jego lud, i Izraela, jego dziedzictwo.
72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.
A on ich pasł w prawości swego serca i prowadził ich roztropną ręką.

< Zaburi 78 >