< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Pieśń i psalm dla synów Korego. Wielki jest PAN i godzien wielkiej chwały w mieście naszego Boga, na swej świętej górze.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Pięknie wzniesiona, radością całej ziemi [jest] góra Syjon na krańcach północy, miasto wielkiego Króla.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Bóg w pałacach jego jest uznany za twierdzę.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Bo oto zgromadzili się królowie i razem ruszyli.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Gdy zobaczyli, zdumieli się, przerazili się i uciekli.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Strach ich tam ogarnął i ból, jak rodzącą kobietę.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Wiatrem wschodnim rozbijasz okręty Tarszisz.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
To, co słyszeliśmy, [to] zobaczyliśmy w mieście PANA zastępów, w mieście naszego Boga; Bóg je ugruntuje na wieki. (Sela)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Rozważamy, o Boże, twoje miłosierdzie we wnętrzu twej świątyni.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Jak twoje imię, Boże, tak i chwała twoja [sięga] aż po krańce ziemi; twoja prawica pełna jest sprawiedliwości.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Niech się weseli góra Syjon, niech się radują córki Judy z powodu twoich sądów.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Okrążcie Syjon i obejdźcie go, policzcie jego wieże.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Przyjrzyjcie się jego wałom obronnym, oglądajcie jego pałace, abyście mogli opowiadać przyszłemu pokoleniu.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Bo ten Bóg jest naszym Bogiem na wieki wieków, on będzie nas prowadził aż do śmierci.

< Zaburi 48 >