< Zaburi 30 >

1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
A psalm; a song at the dedication of the temple. A psalm of David. I will exalt you, Yahweh, for you have raised me up and have not allowed my enemies to rejoice over me.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
Yahweh my God, I cried to you for help, and you healed me.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
Yahweh, you have brought up my soul from Sheol; you have kept me alive from going down to the grave. (Sheol h7585)
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Sing praises to Yahweh, you his faithful people! Give thanks when you remember his holiness.
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
For his anger is only for a moment; but his favor is for a lifetime. Weeping comes for a night, but joy comes in the morning.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
In confidence I said, “I will never be shaken.”
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
Yahweh, by your favor you established me as a strong mountain; but when you hid your face, I was troubled.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
I cried to you, Yahweh, and sought favor from my Lord!
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
What advantage is there in my death, if I go down to the grave? Will the dust praise you? Will it declare your trustworthiness?
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
Hear, Yahweh, and have mercy on me! Yahweh, be my helper.
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
You have turned my mourning into dancing; you have removed my sackcloth and clothed me with gladness.
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
So now my glory will sing praise to you and not be silent; Yahweh my God, I will give thanks to you forever!

< Zaburi 30 >