< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
Een psalm van David, bij zijn vlucht voor zijn zoon Absalom. Jahweh, hoe talrijk zijn mijn belagers, Hoe talrijk, die tegen mij opstaan;
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Hoe velen, die van mij zeggen: Voor hem geen heil bij zijn God!
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
Toch zijt Gij, Jahweh, het schild dat mij dekt, Mijn glorie en trots!
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
Ik behoef maar tot Jahweh te roepen, Dan verhoort Hij mij van zijn heilige berg.
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
Ik leg mij neer, slaap rustig in, Ontwaak, want Jahweh beschut mij.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
Zo vrees ik de duizenden niet, Die van alle kant mij omringen.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Sta op dan, Jahweh; Red mij, mijn God! Want Gij slaat al mijn vijanden in het gezicht, Stoot de bozen hun tanden stuk.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Bij U, Jahweh, is redding; Op uw volk rust uw zegen.

< Zaburi 3 >