< Zaburi 120 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
(Sang til Festrejserne.) Jeg råbte til HERREN i Nød, og han svarede mig.
2 Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
HERRE, udfri min Sjæl fra Løgnelæber, fra den falske Tunge!
3 Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
Der ramme dig dette og hint, du falske Tunge!
4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
Den stærkes Pile er hvæsset ved glødende Gyvel.
5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
Ve mig, at jeg må leve som fremmed i Mesjek, bo iblandt Kedars Telte!
6 Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
Min Sjæl har længe nok boet blandt Folk, som hader Fred.
7 Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.
Jeg vil Fred; men taler jeg, vil de Krig!

< Zaburi 120 >