< Zaburi 12 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
in finem pro octava psalmus David salvum me fac Domine quoniam defecit sanctus quoniam deminutae sunt veritates a filiis hominum
2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
vana locuti sunt unusquisque ad proximum suum labia dolosa in corde et corde locuti sunt
3 Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila na kila ulimi uliojaa majivuno,
disperdat Dominus universa labia dolosa linguam magniloquam
4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
qui dixerunt linguam nostram magnificabimus labia nostra a nobis sunt quis noster dominus est
5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge na kulia kwa uchungu kwa wahitaji, nitainuka sasa,” asema Bwana. “Nitawalinda kutokana na wale wenye nia mbaya juu yao.”
propter miseriam inopum et gemitum pauperum nunc exsurgam dicit Dominus ponam in salutari fiducialiter agam in eo
6 Maneno ya Bwana ni safi, kama fedha iliyosafishwa katika tanuru, iliyosafishwa mara saba.
eloquia Domini eloquia casta argentum igne examinatum probatum terrae purgatum septuplum
7 Ee Bwana, utatuweka salama na kutulinda na kizazi hiki milele.
tu Domine servabis nos et custodies nos a generatione hac et in aeternum
8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali wakati ambapo yule aliye mbaya sana ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
in circuitu impii ambulant secundum altitudinem tuam multiplicasti filios hominum

< Zaburi 12 >