< Zaburi 109 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
למנצח לדוד מזמור אלהי תהלתי אל תחרש׃
2 kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
כי פי רשע ופי מרמה עלי פתחו דברו אתי לשון שקר׃
3 Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
ודברי שנאה סבבוני וילחמוני חנם׃
4 Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
תחת אהבתי ישטנוני ואני תפלה׃
5 Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
וישימו עלי רעה תחת טובה ושנאה תחת אהבתי׃
6 Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
הפקד עליו רשע ושטן יעמד על ימינו׃
7 Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
בהשפטו יצא רשע ותפלתו תהיה לחטאה׃
8 Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
יהיו ימיו מעטים פקדתו יקח אחר׃
9 Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
יהיו בניו יתומים ואשתו אלמנה׃
10 Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
ונוע ינועו בניו ושאלו ודרשו מחרבותיהם׃
11 Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
ינקש נושה לכל אשר לו ויבזו זרים יגיעו׃
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
אל יהי לו משך חסד ואל יהי חונן ליתומיו׃
13 Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
יהי אחריתו להכרית בדור אחר ימח שמם׃
14 Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
יזכר עון אבתיו אל יהוה וחטאת אמו אל תמח׃
15 Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
יהיו נגד יהוה תמיד ויכרת מארץ זכרם׃
16 Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
יען אשר לא זכר עשות חסד וירדף איש עני ואביון ונכאה לבב למותת׃
17 Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
ויאהב קללה ותבואהו ולא חפץ בברכה ותרחק ממנו׃
18 Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
וילבש קללה כמדו ותבא כמים בקרבו וכשמן בעצמותיו׃
19 Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
תהי לו כבגד יעטה ולמזח תמיד יחגרה׃
20 Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
זאת פעלת שטני מאת יהוה והדברים רע על נפשי׃
21 Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
ואתה יהוה אדני עשה אתי למען שמך כי טוב חסדך הצילני׃
22 Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
כי עני ואביון אנכי ולבי חלל בקרבי׃
23 Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
כצל כנטותו נהלכתי ננערתי כארבה׃
24 Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
ברכי כשלו מצום ובשרי כחש משמן׃
25 Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
ואני הייתי חרפה להם יראוני יניעון ראשם׃
26 Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
עזרני יהוה אלהי הושיעני כחסדך׃
27 Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
וידעו כי ידך זאת אתה יהוה עשיתה׃
28 Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
יקללו המה ואתה תברך קמו ויבשו ועבדך ישמח׃
29 Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
ילבשו שוטני כלמה ויעטו כמעיל בשתם׃
30 Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
אודה יהוה מאד בפי ובתוך רבים אהללנו׃
31 Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.
כי יעמד לימין אביון להושיע משפטי נפשו׃

< Zaburi 109 >