< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Wysławiajcie PANA, bo [jest] dobry, bo jego miłosierdzie [trwa] na wieki.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Niech [to] mówią odkupieni przez PANA, ci, których odkupił z ręki wroga;
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
I zgromadził z ziem, ze wschodu i zachodu, z północy i południa.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Błądzili po pustyni, po bezdrożnym pustkowiu, nie znajdując miasta, gdzie mogliby zamieszkać.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
[Byli] głodni i spragnieni, aż omdlewała w nich dusza.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
A gdy zawołali do PANA w swoim utrapieniu, uwolnił ich z ucisku;
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
I prowadził ich prostą drogą, aby doszli do miasta, w którym mogliby zamieszkać.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Niech wysławiają PANA [za] jego miłosierdzie i cudowne dzieła [wobec] synów ludzkich;
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Bo napoił spragnioną duszę, a głodną duszę napełnił dobrami.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Siedzieli w ciemności i w cieniu śmierci, spętani nędzą i żelazem;
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
Bo buntowali się przeciw słowom Boga i pogardzili radą Najwyższego.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Dlatego upokorzył ich serce trudem, upadli, a nie było nikogo, kto by im pomógł.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
A [gdy] wołali do PANA w swoim utrapieniu, wybawił ich z ucisku;
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
Wyprowadził ich z ciemności i z cienia śmierci, a ich pęta rozerwał.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Niech wysławiają PANA [za] jego miłosierdzie i za cudowne dzieła [wobec] synów ludzkich.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Bo skruszył bramy spiżowe i połamał żelazne rygle.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Głupcy z powodu swej występnej drogi i nieprawości doznają utrapień.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Ich dusza brzydzi się wszelkim pokarmem i zbliżają się do bram śmierci.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
A gdy wołają do PANA w swoim utrapieniu, wybawia ich z udręczeń.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Posłał swoje słowo i uzdrowił ich, i wybawił ich z grobu.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Niech wysławiają PANA [za] jego miłosierdzie i cudowne dzieła [wobec] synów ludzkich;
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
I niech składają ofiary dziękczynienia, i głoszą z radością jego dzieła.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Ci, którzy na statkach wyruszają w morze, handlujący na wielkich wodach;
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
Widzą dzieła PANA i jego cuda w głębinach.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
Gdy daje rozkaz, powstaje wicher i podnoszą się fale morskie.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Oni wstępują aż [do] nieba i zstępują w głębiny, tak że ich dusza mdleje w niebezpieczeństwie.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
Chwieją się i zataczają jak pijany, a cała ich mądrość zanika.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Gdy wołają do PANA w swoim utrapieniu, wybawia ich z udręczeń.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
Zamienia burzę w ciszę, tak że uspokajają się jej fale.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Wtedy oni weselą się, że ucichły; i tak przyprowadza ich do upragnionego portu.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Niech wysławiają PANA [za] jego miłosierdzie i cudowne dzieła [wobec] synów ludzkich.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Niech go wywyższają w zgromadzeniu ludu i w radzie starszych niech go chwalą.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
Zamienia rzeki w pustynię, a źródła wód w suchą ziemię;
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
Ziemię urodzajną [zamienia] w jałową z powodu niegodziwości tych, którzy w niej mieszkają.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
Pustynię zamienia w jezioro, a suchą ziemię w źródła wód.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
I osadza tam głodnych, aby zakładali miasta do zamieszkania;
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
I obsiewali pole, sadzili winnice i zbierali obfity plon.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Błogosławi im tak, że bardzo się rozmnażają, i nie zmniejsza [liczebności] ich bydła.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Ale potem maleje ich liczba i upokorzeni są uciskiem, nędzą i utrapieniem;
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
On wylewa wzgardę na władców i sprawia, że błądzą po bezdrożach pustkowia.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Lecz podnosi nędznego z utrapienia i rozmnaża [jego] rodzinę jak stado.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Widząc to, prawi rozweselą się, a wszelka nieprawość zamknie swe usta.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Kto jest tak mądry, aby tego upatrywał i rozumiał litość PANA?

< Zaburi 107 >