< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Segne, Jehovah, meine Seele! Jehovah, mein Gott, Du bist sehr groß. Majestät und Ehre hast Du angezogen!
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Er umhüllt Sich mit Licht wie mit einem Gewand, Er spannt die Himmel aus wie einen Teppich.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Er zimmert mit Wassern Seine Söller, setzt dichte Wolken zu Seinem Wagen und geht auf den Flügeln des Windes einher.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Er macht zu Seinen Boten die Winde, zu Seinen Dienern flammend Feuer.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Er hat die Erde auf ihre Grundlagen gegründet, daß sie nicht wankt in Ewigkeit und immerfort.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Mit dem Abgrund hast Du sie bedeckt, wie mit einem Anzug; die Wasser stehen auf den Bergen.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
Vor Deinem Drohen fliehen sie, enteilen vor der Stimme Deines Donners.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Die Berge steigen auf, die Talgründe sinken hernieder zum Ort, den Du für sie gegründet hast.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Du setztest eine Grenze, die sie nicht überschreiten; sie kehren nicht zurück, die Erde zu bedecken.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Er sendet Quellen in die Bachtäler; zwischen den Bergen gehen sie.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Sie tränken alle wilden Tiere des Gefildes; Waldesel löschen ihren Durst.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Des Himmels Gevögel wohnen an ihnen, aus dem Gezweig geben sie ihre Stimme hervor.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Von Seinen Söllern aus tränkt Er die Berge, von Seiner Werke Frucht wird satt die Erde;
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Er läßt Gras sprossen für das Vieh und Kraut zum Dienst des Menschen, damit er Brot herausbringe aus der Erde.
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
Und Wein macht fröhlich des Menschen Herz; daß von Öl sein Antlitz glänze und Brot das Herz des Menschen labe.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Jehovahs Bäume werden satt, die Zedern Libanons, die Er gepflanzt.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Daselbst nisten die Vögel; der Storch hat sein Haus auf Tannen.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Die hohen Berge sind der Gemsen, der Kaninchen Schirm die Felsenklippen.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Er hat den Mond gemacht für die bestimmten Festzeiten, die Sonne weiß ihren Niedergang.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Du setzest Finsternis und es wird Nacht; da kriechen hervor alle wilden Tiere des Waldes.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Die jungen Löwen brüllen nach dem Zerfleischen, und suchen von Gott ihre Speise.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Die Sonne geht auf, sie sammeln sich und lagern sich in ihren Wohnstätten.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Der Mensch geht aus an sein Werk, und zu seinem Dienst bis an den Abend.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Wie viel sind Deiner Werke, o Jehovah, sie alle hast mit Weisheit Du gemacht. Voll ist die Erde Deines Besitztums.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Da ist das Meer, groß und weit zu beiden Händen, dort sind Kriechtiere auch ohne Zahl, kleine Getiere und große.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Da gehen Schiffe, der Leviathan, den Du gebildet, um darin zu scherzen.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Sie alle warten auf Dich, daß Du ihnen ihre Speise gebest zu seiner Zeit.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Du gibst ihnen, sie lesen auf, Du tust Deine Hand auf, sie werden mit Gutem gesättigt.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Du verbirgst Dein Angesicht, sie sind bestürzt, Du raffst ihren Geist weg, sie verscheiden und kehren zu ihrem Staub zurück.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Sendest Du Deinen Geist aus, sind sie geschaffen, und Du erneuerst das Angesicht des Bodens.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
Jehovahs Herrlichkeit sei in Ewigkeit. Es sei fröhlich Jehovah in Seinen Werken.
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Er blickt zur Erde, und sie bebt. Er rührt die Berge an, und sie rauchen.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
In meinem Leben will ich Jehovah singen, will Psalmen singen meinem Gott, weil ich bin.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Es möge Ihm genehm sein mein Nachsinnen! Ich will fröhlich sein in Jehovah.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Möchten die Sünder ein Ende nehmen von der Erde, und die Ungerechten nicht mehr sein! Segne Jehovah, meine Seele! Hallelujah!

< Zaburi 104 >