< Hesabu 1 >

1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
IL Signore parlò ancora a Mosè, nel deserto di Sinai, nel Tabernacolo della convenenza, nel primo giorno del secondo mese, nell'anno secondo da che [i figliuoli d'Israele] furono usciti fuor del paese di Egitto, dicendo:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
Levate la somma di tutta la raunanza de' figliuoli d'Israele, secondo le lor nazioni, [e] le famiglie de' padri loro, contando per nome, a testa a testa, ogni maschio,
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
di età da vent'anni in su, tutti coloro che possono andare alla guerra in Israele; annoverateli, tu, ed Aaronne, per le loro schiere.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
E siavi con voi un uomo di ciascuna tribù, che sia capo della sua casa paterna.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
E questi [sono] i nomi di coloro che saranno presenti con voi: Di Ruben, Elisur, figliuolo di Sedeur;
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
Di Simeone, Selumiel, figliuolo di Surisaddai;
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
Di Giuda, Naasson, figliuolo di Amminadab;
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
D'Issacar, Natanael, figliuolo di Suar;
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
Di Zabulon, Eliab, figliuolo di Helon;
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
De' figliuoli di Giuseppe: di Efraim, Elisama, figliuoli di Ammiud; di Manasse, Gamliel, figliuolo di Pedasur;
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
Di Beniamino, Abidan, figliuolo di Ghidoni;
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
Di Dan, Ahiezer, figliuolo di Ammisaddai;
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
Di Aser, Paghiel, figliuolo di Ocran;
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
Di Gad, Eliasaf, figliuolo di Deuel;
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
Di Neftali, Ahira, figliuolo di Enan.
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
Costoro [erano] quelli che si chiamavano alla raunanza, principali delle tribù loro paterne, e capi delle migliaia d'Israele.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
Mosè adunque ed Aaronne presero seco questi uomini, ch'erano stati nominati per li nomi [loro].
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
E, a' calendi del secondo mese, adunarono tutta la raunanza; e le generazioni [de' figliuoli d'Israele] furono descritte per le lor nazioni, e per le famiglie loro paterne, contandoli per nome dall'età di vent'anni in su, a testa a testa.
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Come il Signore avea comandato a Mosè, egli li annoverò nel deserto di Sinai.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
E delle generazioni de' figliuoli di Ruben, primogenito d'Israele, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome, a testa a testa, d'infra tutti i maschi, dall'età di vent'anni in su, tutti quelli che potevano andare alla guerra;
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
gli annoverati della tribù di Ruben [furono] quarantaseimila cinquecento.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Simeone, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome, a testa a testa, d'infra tutti i maschi, dall'età di vent'anni in su, tutti quelli che potevano andare alla guerra;
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
gli annoverati della tribù di Simeone [furono] cinquantanovemila trecento.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Gad, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
gli annoverati della tribù di Gad [furono] quarantacinquemila seicencinquanta.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Giuda, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
gli annoverati della tribù di Giuda [furono] settantaquattromila seicento.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli d'Issacar, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
gli annoverati della tribù d'Issacar [furono] cinquantaquattromila quattrocento.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Zabulon, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
gli annoverati della tribù di Zabulon [furono] cinquantasettemila quattrocento.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De' figliuoli di Giuseppe; delle generazioni de' figliuoli di Efraim, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
gli annoverati della tribù di Efraim [furono] quarantamila cinquecento.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Manasse, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
gli annoverati della tribù di Manasse [furono] trentaduemila dugento.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Beniaminio, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
gli annoverati della tribù di Beniamino [furono] trentacinquemila quattrocento.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Dan, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
gli annoverati della tribù di Dan [furono] sessantaduemila settecento.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Aser, per le lor nazioni, e famiglie paterne; contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
gli annoverati della tribù di Aser [furono] quarantunmila cinquecento.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Delle generazioni de' figliuoli di Neftali, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
gli annoverati della tribù di Neftali [furono] cinquantatremila quattrocento.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
Questi [furono] gli annoverati, i quali Mosè ed Aaronne annoverarono, insieme co' principali d'Israele, [ch'] erano dodici uomini, uno per familglia paterna.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Così, tutti gli annoverati d'infra i figliuoli d'Israele, per le lor famiglie paterne, dall'età di vent'anni in su, che potevano andare alla guerra,
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
furono seicentotremila cinquecencinquanta.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Ma i Leviti non furono annoverati fra loro secondo la lor tribù paterna;
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
perciocchè il Signore avea detto a Mosè:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
Sol non annoverar la tribù di Levi, e non levarne la somma per mezzo i figliuoli d'Iraele.
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
Ma ordina i Leviti sopra il Tabernacolo della Testimonianza, e sopra tutti i suoi arredi; e sopra tutte le cose ad esso [appartenenti]; e portino essi il Tabernacolo e tutti i suoi arredi; e facciano i servigi di esso, e accampinvisi attorno.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
E quando il Tabernacolo si dipartirà, mettanlo giù i Leviti; quando altresì si accamperà, rizzinlo i Leviti; e se alcuno straniere vi si appressa, sia fatto morire.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
Or accampinsi i figliuoli d'Israele, ciascuno nel suo quartiere, e ciascuno presso alla sua bandiera, per le loro schiere.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Ma accampinsi i Leviti intorno al Tabernacolo della Testimonianza; acciocchè non vi sia ira contro alla raunanza de' figliuoli d'Israele; e facciano i Leviti la funzione del Tabernacolo della Testimonianza.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
E i figliuoli d'Israele fecero interamente come il Signore avea comandato.

< Hesabu 1 >