< Hesabu 31 >

1 Bwana akamwambia Mose,
The LORD spoke to Moses, saying,
2 “Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
“Avenge the children of Israel on the Midianites. Afterward you shall be gathered to your people.”
3 Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
Moses spoke to the people, saying, “Arm men from amongst you for war, that they may go against Midian, to execute the LORD’s vengeance on Midian.
4 Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
You shall send one thousand out of every tribe, throughout all the tribes of Israel, to the war.”
5 Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
So there were delivered, out of the thousands of Israel, a thousand from every tribe, twelve thousand armed for war.
6 Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
Moses sent them, one thousand of every tribe, to the war with Phinehas the son of Eleazar the priest, to the war, with the vessels of the sanctuary and the shofars for the alarm in his hand.
7 Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
They fought against Midian, as the LORD commanded Moses. They killed every male.
8 Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
They killed the kings of Midian with the rest of their slain: Evi, Rekem, Zur, Hur, and Reba, the five kings of Midian. They also killed Balaam the son of Beor with the sword.
9 Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
The children of Israel took the women of Midian captive with their little ones; and all their livestock, all their flocks, and all their goods, they took as plunder.
10 Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
All their cities in the places in which they lived, and all their encampments, they burnt with fire.
11 Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
They took all the captives, and all the plunder, both of man and of animal.
12 nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
They brought the captives with the prey and the plunder, to Moses, and to Eleazar the priest, and to the congregation of the children of Israel, to the camp at the plains of Moab, which are by the Jordan at Jericho.
13 Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
Moses and Eleazar the priest, with all the princes of the congregation, went out to meet them outside of the camp.
14 Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
Moses was angry with the officers of the army, the captains of thousands and the captains of hundreds, who came from the service of the war.
15 Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
Moses said to them, “Have you saved all the women alive?
16 “Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
Behold, these caused the children of Israel, through the counsel of Balaam, to commit trespass against the LORD in the matter of Peor, and so the plague was amongst the congregation of the LORD.
17 Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
Now therefore kill every male amongst the little ones, and kill every woman who has known man by lying with him.
18 lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
But all the girls, who have not known man by lying with him, keep alive for yourselves.
19 “Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
“Encamp outside of the camp for seven days. Whoever has killed any person, and whoever has touched any slain, purify yourselves on the third day and on the seventh day, you and your captives.
20 Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
You shall purify every garment, and all that is made of skin, and all work of goats’ hair, and all things made of wood.”
21 Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
Eleazar the priest said to the men of war who went to the battle, “This is the statute of the law which the LORD has commanded Moses.
22 Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
However the gold, and the silver, the bronze, the iron, the tin, and the lead,
23 na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
everything that may withstand the fire, you shall make to go through the fire, and it shall be clean; nevertheless it shall be purified with the water for impurity. All that doesn’t withstand the fire you shall make to go through the water.
24 Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
You shall wash your clothes on the seventh day, and you shall be clean. Afterward you shall come into the camp.”
25 Bwana akamwambia Mose,
The LORD spoke to Moses, saying,
26 “Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
“Count the plunder that was taken, both of man and of animal, you, and Eleazar the priest, and the heads of the fathers’ households of the congregation;
27 Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
and divide the plunder into two parts: between the men skilled in war, who went out to battle, and all the congregation.
28 Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
Levy a tribute to the LORD of the men of war who went out to battle: one soul of five hundred; of the persons, of the cattle, of the donkeys, and of the flocks.
29 Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
Take it from their half, and give it to Eleazar the priest, for the LORD’s wave offering.
30 Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
Of the children of Israel’s half, you shall take one drawn out of every fifty, of the persons, of the cattle, of the donkeys, and of the flocks, of all the livestock, and give them to the Levites, who perform the duty of the LORD’s tabernacle.”
31 Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Moses and Eleazar the priest did as the LORD commanded Moses.
32 Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
Now the plunder, over and above the booty which the men of war took, was six hundred and seventy-five thousand sheep,
33 ngʼombe 72,000,
seventy-two thousand head of cattle,
34 punda 61,000,
sixty-one thousand donkeys,
35 na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
and thirty-two thousand persons in all, of the women who had not known man by lying with him.
36 Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
The half, which was the portion of those who went out to war, was in number three hundred and thirty-seven thousand and five hundred sheep;
37 ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
and the LORD’s tribute of the sheep was six hundred and seventy-five.
38 ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
The cattle were thirty-six thousand, of which the LORD’s tribute was seventy-two.
39 punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
The donkeys were thirty thousand and five hundred, of which the LORD’s tribute was sixty-one.
40 Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
The persons were sixteen thousand, of whom the LORD’s tribute was thirty-two persons.
41 Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Moses gave the tribute, which was the LORD’s wave offering, to Eleazar the priest, as the LORD commanded Moses.
42 Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
Of the children of Israel’s half, which Moses divided off from the men who fought
43 nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
(now the congregation’s half was three hundred and thirty-seven thousand and five hundred sheep,
44 ngʼombe 36,000,
thirty-six thousand head of cattle,
45 punda 30,500,
thirty thousand and five hundred donkeys,
46 na wanadamu 16,000.
and sixteen thousand persons),
47 Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
even of the children of Israel’s half, Moses took one drawn out of every fifty, both of man and of animal, and gave them to the Levites, who performed the duty of the LORD’s tabernacle, as the LORD commanded Moses.
48 Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
The officers who were over the thousands of the army, the captains of thousands, and the captains of hundreds, came near to Moses.
49 na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
They said to Moses, “Your servants have taken the sum of the men of war who are under our command, and there lacks not one man of us.
50 Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
We have brought the LORD’s offering, what every man found: gold ornaments, armlets, bracelets, signet rings, earrings, and necklaces, to make atonement for our souls before the LORD.”
51 Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
Moses and Eleazar the priest took their gold, even all worked jewels.
52 Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
All the gold of the wave offering that they offered up to the LORD, of the captains of thousands, and of the captains of hundreds, was sixteen thousand and seven hundred and fifty shekels.
53 Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
The men of war had taken booty, every man for himself.
54 Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.
Moses and Eleazar the priest took the gold of the captains of thousands and of hundreds, and brought it into the Tent of Meeting for a memorial for the children of Israel before the LORD.

< Hesabu 31 >