< Hesabu 19 >

1 Bwana akamwambia Mose na Aroni:
I PAN powiedział do Mojżesza i Aarona:
2 “Hivi ndivyo sheria ambayo Bwana ameagiza itakavyo: Waambie Waisraeli wakuletee mtamba mwekundu asiye na dosari wala waa, na ambaye hajapata kufungwa nira.
To jest ustawa prawa, którą nadał PAN: Powiedz synom Izraela, aby przyprowadzili do ciebie czerwoną jałówkę, zdrową i bez skazy, na której jeszcze nie było jarzma.
3 Mpeni kuhani Eleazari huyo mtamba; naye atatolewa nje ya kambi na kuchinjwa mbele yake huyo kuhani.
Oddacie ją kapłanowi Eleazarowi, który ją wyprowadzi poza obóz, i zostanie przed nim zabita.
4 Kisha kuhani Eleazari atachukua baadhi ya damu yake kwenye kidole chake na kuinyunyiza mara saba kuelekea upande wa mbele ya Hema la Kukutania.
A kapłan Eleazar weźmie nieco z jej krwi na swój palec i pokropi nią siedem razy na wprost przed Namiotem Zgromadzenia.
5 Wakati angali akitazama, mtamba huyo atateketezwa: ngozi yake, nyama yake, damu na sehemu zake za ndani.
Potem każe spalić jałówkę na swoich oczach: spali jej skórę, mięso, krew wraz z jej odchodami.
6 Kuhani atachukua kuni za mti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu, na kuvitupa kwenye huyo mtamba anayeungua.
I kapłan weźmie drewno cedrowe, hizop i karmazyn i wrzuci to do ognia, w którym płonie jałówka.
7 Baada ya hayo, kuhani lazima afue nguo zake, na aoge mwili wake kwa maji. Kisha anaweza kurudi kambini, lakini atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni.
Wtedy kapłan wypierze swoje szaty i umyje swoje ciało wodą; potem wejdzie do obozu i będzie nieczysty do wieczora.
8 Mtu amchomaye huyo mtamba lazima naye pia afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye pia atakuwa najisi mpaka jioni.
Również ten, który ją będzie palić, wypierze swoje szaty w wodzie i umyje swoje ciało wodą, i będzie nieczysty do wieczora.
9 “Mtu ambaye ni safi atakusanya majivu ya mtamba huyo na kuyaweka mahali ambapo ni safi nje ya kambi kwa taratibu za kiibada. Yatahifadhiwa na jumuiya ya Kiisraeli kwa matumizi katika maji ya utakaso; ni kwa ajili ya kutakasa kutoka dhambini.
Człowiek czysty zbierze popiół tej jałówki i złoży go poza obozem na miejscu czystym; będzie on przechowywany dla zgromadzenia synów Izraela do wody oczyszczenia; jest to ofiara za grzech.
10 Mtu akusanyaye majivu ya huyo mtamba ni lazima pia afue nguo zake, kadhalika naye pia atakuwa najisi hadi jioni. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa Waisraeli na kwa wageni wanaoishi miongoni mwao.
Ten, który zbierał popiół jałówki, wypierze swoje szaty i będzie nieczysty do wieczora. Będzie to ustawa wieczysta dla synów Izraela i dla przybysza mieszkającego wśród was.
11 “Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba.
Kto dotknie jakiegokolwiek ludzkiego trupa, będzie nieczysty przez siedem dni.
12 Ni lazima ajitakase mwenyewe kwa maji katika siku ya tatu na siku ya saba, ndipo atakuwa safi. Lakini kama hatajitakasa mwenyewe katika siku ya tatu na ya saba, hatakuwa safi.
Taki oczyści się tą [wodą] w trzecim i siódmym dniu i będzie czysty. Jeśli jednak nie oczyści się w trzecim i siódmym dniu, będzie nieczysty.
13 Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote na kushindwa kujitakasa mwenyewe hunajisi Maskani ya Bwana. Mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na Israeli. Kwa sababu hajanyunyiziwa maji ya utakaso, yeye ni najisi; unajisi wake unabaki juu yake.
Kto dotknie zwłok człowieka zmarłego, a nie oczyści się, ten zanieczyści przybytek PANA; ta dusza będzie wykluczona z Izraela. Człowiek ten nie został bowiem pokropiony wodą oczyszczenia; będzie nieczysty, a jego nieczystość pozostanie na nim.
14 “Hii ndiyo sheria itumikayo wakati mtu amekufa ndani ya hema: Yeyote aingiaye ndani ya hema hilo na yeyote aliye ndani yake watakuwa najisi kwa muda wa siku saba,
Taka [jest] ustawa, gdy człowiek umrze w namiocie: ktokolwiek wejdzie do tego namiotu i cokolwiek [znajduje się] w tym namiocie będzie nieczyste przez siedem dni.
15 nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.
Każde naczynie odkryte, które nie ma przymocowanej pokrywy, będzie nieczyste.
16 “Mtu yeyote aliyeko nje mahali pa wazi agusaye mtu aliyeuawa kwa upanga au mtu aliyekufa kwa kifo cha kawaida, au mtu yeyote agusaye mfupa wa mtu aliyekufa au kaburi, atakuwa najisi kwa siku saba.
Kto dotknie na polu zabitego mieczem lub umarłego, lub kości ludzkich, lub grobu będzie nieczysty przez siedem dni.
17 “Kwa mtu aliye najisi, weka majivu ya sadaka ya utakaso wa dhambi ndani ya chombo, umimine maji safi juu yao.
Wezmą dla [tego] nieczystego nieco popiołu [jałówki] spalonej za grzech i na to wleją do naczynia źródlanej wody.
18 Kisha mtu aliye safi kwa kawaida za kiibada atachukua hisopo, achovye ndani ya maji, na kunyunyizia hema na vifaa vyote pamoja na watu ambao walikuwamo. Pia ni lazima amnyunyizie mtu yeyote ambaye amegusa mfupa wa mtu aliyekufa, au kaburi, au mtu ambaye ameuawa, au mtu ambaye amekufa kifo cha kawaida.
Człowiek czysty weźmie hizop, zmoczy go w tej wodzie i pokropi namiot oraz wszystkie naczynia i wszystkich ludzi, którzy tam byli, także tego, który dotknął kości lub zabitego, lub zmarłego, lub grobu.
19 Mtu ambaye ni safi ndiye atakayemnyunyizia yeyote ambaye ni najisi siku ya tatu na siku ya saba, na katika siku ya saba atamtakasa mtu huyo. Mtu ambaye ametakaswa lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, na jioni ile atakuwa safi.
[Człowiek] czysty pokropi nieczystego w trzecim i siódmym dniu, a gdy go oczyści w siódmym dniu, wypierze on swoje szaty i umyje się wodą, i wieczorem będzie czysty.
20 Lakini ikiwa mtu ambaye ni najisi hakujitakasa mwenyewe, ni lazima akatiliwe mbali na jumuiya, kwa sababu ameinajisi Maskani ya Bwana. Maji ya utakaso hayajanyunyizwa juu yake, naye ni najisi.
A człowiek, który stał się nieczysty, a nie oczyścił się, zostanie wykluczony spośród zgromadzenia, gdyż ta dusza zbezcześciła świątynię PANA. Człowiek ten nie został pokropiony wodą oczyszczenia i jest nieczysty.
21 Hii ni sheria ya kudumu kwao. “Mtu yeyote ambaye ananyunyiza yale maji ya utakaso lazima pia afue nguo zake, na yeyote ambaye hugusa maji ya utakaso atakuwa najisi mpaka jioni.
Będzie to dla nich ustawą wieczystą: kto skrapia wodą oczyszczenia, wypierze swoje szaty, a kto dotknie tej wody oczyszczenia, będzie nieczysty do wieczora.
22 Kitu chochote anachogusa mtu aliye najisi kitakuwa najisi, na yeyote akigusaye huwa najisi mpaka jioni.”
Czegokolwiek dotknie nieczysty, będzie nieczyste; również człowiek, który [tego] dotknie, będzie nieczysty do wieczora.

< Hesabu 19 >