< Nehemia 12 >

1 Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
A oto kapłani i Lewici, którzy przybyli z Zorobabelem, synem Szealtiela, i z Jeszuą: Serajasz, Jeremiasz, Ezdrasz;
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
Amariasz, Malluk, Chattusz;
3 Shekania, Rehumu, Meremothi,
Szekaniasz, Rechum, Meremot;
4 Ido, Ginethoni, Abiya,
Iddo, Ginneton, Abiasz;
5 Miyamini, Moadia, Bilga,
Mijamin, Maadiasz, Bilga;
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
Szemajasz, Jojarib, Jedajasz;
7 Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
Sallu, Amok, Chilkiasz, Jedajasz. To [byli] przedniejsi z kapłanów i ze swoich braci za dni Jeszuy.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
A Lewici: Jeszua, Binnuj, Kadmiel, Szerebiasz, Juda i Mattaniasz, który wraz z braćmi kierował śpiewem [pieśni dziękczynnych].
9 Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
A Bakbukiasz i Unni, ich bracia, [stali] naprzeciw nich w [swoich] służbach.
10 Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
Jeszua spłodził Jojakima, a Jojakim spłodził Eliasziba, a Eliaszib spłodził Jojadę;
11 Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
Jojada spłodził Jonatana, a Jonatan spłodził Jadduę.
12 Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
A za dni Jojakima naczelnikami rodu byli [następujący] kapłani: z Serajasza – Merajasz, z Jeremiasza – Chananiasz;
13 wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
Z Ezdrasza – Meszullam, z Amariasza – Jehochanan;
14 wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
Z Malluki – Jonatan, z Szebaniasza – Józef;
15 wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
Z Charima – Adna, z Merajota – Chelkaj;
16 wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
Z Iddo – Zachariasz, z Ginneto – Meszullam;
17 wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
Z Abiasza – Zikri, z Miniamina i Moadiasza – Piltaj;
18 wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
Z Bilgi – Szammua, z Szemajasza – Jonatan;
19 wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
A z Jojariba – Mattenaj, z Jedajasza – Uzzi;
20 wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
Z Sallaj – Kallaj, z Amoka – Eber;
21 wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
Z Chilkiasza – Chaszabiasz, z Jedajasza – Netanaeel.
22 Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
Za dni Eliasziba, Jojady, Jochanana i Jadduy Lewici zostali spisani jako naczelnicy rodów, a także kapłani, aż do panowania Dariusza Persa.
23 Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
Synowie Lewiego, naczelnicy rodów, [zostali] spisani w księdze kronik aż do dni Jochanana, syna Eliasziba.
24 Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
Naczelnikami Lewitów [byli]: Chaszabiasz, Szerebiasz, Jeszua, syn Kadmiela, i ich bracia, którzy stali naprzeciw nich, straż przy straży, aby chwalić i dziękować, według rozkazu Dawida, męża Bożego.
25 Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
Mattaniasz i Bakbukiasz, Obadiasz, Meszullam, Talmon i Akkub [jako] odźwierni trzymali straż przy składnicach u bram.
26 Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
Ci [żyli] za dni Jojakima, syna Jeszuy, syna Jocadaka, i za dni namiestnika Nehemiasza i Ezdrasza, kapłana i uczonego w Piśmie.
27 Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
I na poświęcanie muru Jerozolimy odszukano Lewitów ze wszystkich ich miejsc, aby ich przyprowadzić do Jerozolimy, by mogli obchodzić poświęcenie z radością, dziękczynieniem, przy śpiewaniu, cymbałach, cytrach i harfach.
28 Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
Zgromadzili się więc synowie śpiewaków, z równin wokół Jerozolimy i ze wsi Netofatytów;
29 kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
Także z domu Gilgal, z pól Geba i z Azmawet. Śpiewacy bowiem zbudowali sobie wsie wokół Jerozolimy.
30 Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
Wtedy kapłani i Lewici oczyścili się, po czym oczyścili też lud, bramy i mur.
31 Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
Następnie kazałem przełożonym Judy wstąpić na mur i ustawiłem dwa wielkie zespoły dziękczynne, z których [jeden] szedł po murze na prawo, w kierunku Bramy Gnojnej.
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
Za nim szedł Hoszajasz i połowa przełożonych Judy;
33 pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
Także Azariasz, Ezdrasz i Meszullam;
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
Juda, Beniamin, Szemajasz i Jeremiasz;
35 pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
Potem [szli] z trąbami niektórzy z synów kapłanów, [mianowicie]: Zachariasz, syn Jonatana, syna Szemajasza, syna Mattaniasza, syna Michajasza, syna Zakkura, syna Asafa;
36 pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
I jego bracia: Szemajasz, Azarel, Milalaj, Gilalaj, Maaj, Netaneel, Juda, Chanani z instrumentami muzycznymi Dawida, męża Bożego, a Ezdrasz, uczony w Piśmie, [szedł] przed nimi.
37 Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
Następnie przy Bramie Źródlanej, która [była] naprzeciw nich, szli po schodach miasta Dawida, które prowadzą na mur, znad domu Dawida aż do Bramy Wodnej na wschodzie.
38 Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
A drugi zespół dziękczynny, a ja za nim, szedł po murze w lewo z drugą połową [przełożonych], od Wieży Pieców aż do Muru Szerokiego;
39 juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
I znad Bramy Efraima, nad Bramą Starą, nad Bramą Rybną, obok Wieży Chananeela i Wieży Mea, aż do Bramy Owczej. I stanęli u Bramy Więziennej.
40 Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
A tak stanęły oba zespoły dziękczynne w domu Bożym, a wraz z nimi ja i połowa przełożonych ze mną.
41 na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
Także kapłani: Eliakim, Maasejasz, Miniamin, Michajasz, Elioenaj, Zachariasz, Chananiasz, z trąbami;
42 na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
I Maasejasz, Szemajasz, Eleazar, Uzzi, Jehochanan, Malkiasz, Elam i Ezer. Śpiewacy głośno śpiewali, a Jizrachiasz był [ich] kierownikiem.
43 Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
Tego dnia składali także wielkie ofiary i radowali się. Bóg bowiem dał im wielką radość. Również kobiety i dzieci radowały się, a radość Jerozolimy słychać było z daleka.
44 Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
W tym czasie ustanowiono mężczyzn nad składnicami dla skarbów, ofiar, pierwocin i dziesięcin, aby w nich zgromadzono dla kapłanów i Lewitów udziały przyznane im przez Prawo z pól miejskich. Juda bowiem cieszył się z powodu kapłanów i Lewitów pełniących służbę;
45 Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
I śpiewacy i odźwierni pełnili służbę dla swego Boga i służbę oczyszczenia, według rozkazu Dawida [i] jego syna Salomona.
46 Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
Już bowiem dawno, za dni Dawida i Asafa, [byli ustanowieni] przełożeni nad śpiewakami oraz [były ustalone] pieśni pochwalne i dziękczynienia dla Boga.
47 Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.
Cały Izrael więc za dni Zorobabela i za dni Nehemiasza dawał porcje śpiewakom i odźwiernym na codzienne utrzymanie. Oddawali Lewitom to, co poświęcili, Lewici zaś oddawali [to] synom Aarona.

< Nehemia 12 >