< Nahumu 1 >

1 Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.
The declaration about Nineveh. The book of the vision of Nahum, the Elkoshite.
2 Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi; Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu. Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake, naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.
Yahweh is a jealous God and avenges; Yahweh avenges and is full of wrath; Yahweh takes vengeance on his adversaries, and he continues his anger for his enemies.
3 Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu, Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia. Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni vumbi la miguu yake.
Yahweh is slow to anger and great in power; he will not allow the wicked to go unpunished. Yahweh makes his way in the whirlwind and the storm, and the clouds are the dust of his feet.
4 Anakemea bahari na kuikausha, anafanya mito yote kukauka. Bashani na Karmeli zinanyauka na maua ya Lebanoni hukauka.
He rebukes the sea and makes it dry; he dries up all the rivers. Bashan is weak, and Carmel also; the flowers of Lebanon are weak.
5 Milima hutikisika mbele yake na vilima huyeyuka. Nchi hutetemeka mbele yake, dunia na wote waishio ndani yake.
The mountains shake in his presence, and the hills melt; the earth collapses in his presence, indeed, the world and all people who live in it.
6 Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu? Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali? Ghadhabu yake imemiminwa kama moto, na miamba inapasuka mbele zake.
Who can stand before his wrath? Who can resist the fierceness of his anger? His wrath is poured out like fire, and the rocks are broken apart by him.
7 Bwana ni Mwema, kimbilio wakati wa taabu. Huwatunza wale wanaomtegemea,
Yahweh is good, a stronghold in the day of trouble; and he is faithful to those who take refuge in him.
8 lakini kwa mafuriko makubwa, ataangamiza Ninawi; atafuatilia adui zake hadi gizani.
But he will make a full end to his enemies with an overwhelming flood; he will pursue them into darkness.
9 Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana yeye atalikomesha; taabu haitatokea mara ya pili.
What are you people plotting against Yahweh? He will make a full end to it; trouble will not rise up a second time.
10 Watasongwa katikati ya miiba na kulewa kwa mvinyo wao. Watateketezwa kama mabua makavu.
For they will become tangled up like thornbushes; they will be saturated in their own drink; they will be completely devoured by fire like dry stubble.
11 Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja, ambaye anapanga shauri baya dhidi ya Bwana na kushauri uovu.
Someone arose among you, Nineveh, who planned evil against Yahweh, someone who promoted wickedness.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Ingawa wana muungano nao ni wengi sana, watakatiliwa mbali na kuangamia. Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda, sitakutesa tena.
This is what Yahweh says, “Even if they are at their full strength and full numbers, they will nevertheless be sheared; their people will be no more. But you, Judah: Though I have afflicted you, I will afflict you no more.
13 Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako, nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”
Now will I break that people's yoke from off you; I will break your chains.”
14 Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi: “Hutakuwa na wazao watakaoendeleza jina lako. Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu. Nitaandaa kaburi lako, kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”
Yahweh has given a command about you, Nineveh: “There will be no more descendants bearing your name. I will cut off the carved figures and the cast metal figures from the houses of your gods. I will dig your graves, for you are contemptible.”
15 Tazama, huko juu milimani, miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema, ambaye anatangaza amani! Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako, nawe utimize nadhiri zako. Waovu hawatakuvamia tena; wataangamizwa kabisa.
Look, on the mountains there are the feet of someone who is bringing good news, who is announcing peace! Celebrate your festivals, Judah, and keep your vows, for the wicked one will invade you no more; he is completely cut off.

< Nahumu 1 >