< Mathayo 4 >

1 Kisha Yesu akaongozwa na Roho Mtakatifu kwenda nyikani ili akajaribiwe na ibilisi.
At that time Jesus was led up by the Spirit into the Desert in order to be tempted by the Devil.
2 Baada ya kufunga siku arobaini usiku na mchana, hatimaye akaona njaa.
There He fasted for forty days and nights; and after that He suffered from hunger.
3 Mjaribu akamjia na kumwambia, “Ikiwa wewe ndiye Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.”
So the Tempter came and said, "If you are the Son of God, command these stones to turn into loaves."
4 Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.’”
"It is written," replied Jesus, "'It is not on bread alone that a man shall live, but on whatsoever God shall appoint.'"
5 Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji mtakatifu na kumweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu,
Then the Devil took Him to the Holy City and caused Him to stand on the roof of the Temple,
6 akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini. Kwa kuwa imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake, nao watakuchukua mikononi mwao ili usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
and said, "If you are God's Son, throw yourself down; for it is written, "'To His angels He will give orders concerning thee, and on their hands they shall bear thee up, lest at any moment thou shouldst strike thy foot against a stone.'"
7 Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa: ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
"Again it is written," replied Jesus, "'Thou shalt not put the Lord thy God to the proof.'"
8 Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari zake,
Then the Devil took Him to the top of an exceedingly lofty mountain, from which he caused Him to see all the Kingdoms of the world and their splendour,
9 kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote kama ukinisujudia na kuniabudu.”
and said to Him, "All this I will give you, if you will kneel down and do me homage."
10 Yesu akamwambia, “Ondoka mbele yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”
"Begone, Satan!" Jesus replied; "for it is written, 'To the Lord thy God thou shalt do homage, and to Him alone shalt thou render worship.'"
11 Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika wakaja na kumhudumia.
Thereupon the Devil left Him, and angels at once came and ministered to Him.
12 Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
Now when Jesus heard that John was thrown into prison, He withdrew into Galilee,
13 Akaondoka Nazareti akaenda kuishi Kapernaumu, mji ulioko karibu na bahari, katika mipaka ya nchi ya Zabuloni na Naftali,
and leaving Nazareth He went and settled at Capernaum, a town by the Lake on the frontiers of Zebulun and Naphtali,
14 ili kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama alivyosema:
in order that these words, spoken through the Prophet Isaiah, might be fulfilled,
15 “Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kwenye njia ya kuelekea baharini, ngʼambo ya Yordani, Galilaya ya watu wa Mataifa:
"Zebulun's land and Naphtali's land; the road by the Lake; the country beyond the Jordan; Galilee of the Nations!
16 watu wale waliokaa gizani wameona nuru kuu; nao wale walioishi katika nchi ya uvuli wa mauti, nuru imewazukia.”
The people who were dwelling in darkness have seen a brilliant light; and on those who were dwelling in the region of the shadow of death, on them light has dawned."
17 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.”
From that time Jesus began to preach. "Repent," He said, "for the Kingdom of the Heavens is now close at hand."
18 Yesu alipokuwa anatembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake. Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
And walking along the shore of the Lake of Galilee He saw two brothers--Simon called Peter and his brother Andrew--throwing a drag-net into the Lake; for they were fishers.
19 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
And He said to them, "Come and follow me, and I will make you fishers of men."
20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
So they immediately left their nets and followed Him. As He went further on,
21 Alipoendelea mbele kutoka pale, akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.
He saw two other brothers, James the son of Zabdi and his brother John, in the boat with their father Zabdi mending their nets; and He called them.
22 Nao mara wakaiacha mashua yao, pamoja na baba yao, wakamfuata.
And they at once left the boat and their father, and followed Him.
23 Yesu akapita katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri habari njema za Ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni mwa watu.
Then Jesus travelled through all Galilee, teaching in their synagogues and proclaiming the Good News of the Kingdom, and curing every kind of disease and infirmity among the people.
24 Kwa hiyo sifa zake zikaenea sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na maumivu, waliopagawa na pepo wachafu, wenye kifafa na waliopooza, naye akawaponya.
Thus His fame spread through all Syria; and they brought all the sick to Him, the people who were suffering from various diseases and pains--demoniacs, epileptics, paralytics; and He cured them.
25 Makutano makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na kutoka ngʼambo ya Mto Yordani.
And great crowds followed Him, coming from Galilee, from the Ten Towns, from Jerusalem, and from beyond the district on the other side of the Jordan.

< Mathayo 4 >