< Mathayo 22 >

1 Yesu akasema nao tena kwa mifano, akawaambia,
Again Jesus spoke to them in figurative language.
2 “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme mmoja aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi.
"The Kingdom of the Heavens," He said, "may be compared to a king who celebrated the marriage of his son,
3 Akawatuma watumishi wake kuwaita wale waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini wakakataa kuja.
and sent his servants to call the invited guests to the wedding, but they were unwilling to come.
4 “Kisha akawatuma watumishi wengine akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba nimeandaa chakula. Nimekwisha kuchinja mafahali wangu na vinono, karamu iko tayari. Karibuni kwa karamu ya arusi.’
"Again he sent other servants with a message to those who were invited. "'My breakfast is now ready," he said, 'my bullocks and fat cattle are killed, and every preparation is made: come to the wedding.'
5 “Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao: huyu shambani mwake na mwingine kwenye biashara zake.
"They however gave no heed, but went, one to his home in the country, another to his business;
6 Wengine wao wakawakamata wale watumishi wake, wakawatesa na kuwaua.
and the rest seized the king's servants, maltreated them, and murdered them.
7 Yule mfalme akakasirika sana, akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
So the king's anger was stirred, and he sent his troops and destroyed those murderers and burnt their city.
8 “Kisha akawaambia watumishi wake, ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale niliowaalika hawakustahili kuja.
Then he said to his servants, "'The wedding banquet is ready, but those who were invited were unworthy of it.
9 Kwa hiyo nendeni katika njia panda mkamwalike karamuni yeyote mtakayemwona.’
Go out therefore to the crossroads, and everybody you meet invite to the wedding.'
10 Wale watumishi wakaenda barabarani, wakawakusanya watu wote waliowaona, wema na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
"So they went out into the roads and gathered together all they could find, both bad and good, and the banqueting hall was filled with guests.
11 “Lakini mfalme alipoingia ndani ili kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi.
"Now the king came in to see the guests; and among them he discovered one who was not wearing a wedding-robe.
12 Mfalme akamuuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
"'My friend,' he said, 'how is it that you came in here without a wedding robe?'
13 “Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.’
"The man stood speechless. Then the king said to the servants, "'Bind him hand and foot and fling him into the darkness outside: there will be the weeping aloud and the gnashing of teeth.'
14 “Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini walioteuliwa ni wachache.”
"For there are many called, but few chosen."
15 Ndipo Mafarisayo wakatoka nje wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika maneno yake.
Then the Pharisees went and consulted together how they might entrap Him in His conversation.
16 Wakatuma wanafunzi wao kwake pamoja na Maherode. Nao wakasema, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika kweli bila kuyumbishwa na mtu wala kuonyesha upendeleo.
So they sent to Him their disciples together with the Herodians; who said, "Teacher, we know that you are truthful and that you faithfully teach God's truth; and that no fear of man misleads you, for you are not biased by men's wealth or rank.
17 Tuambie basi, wewe unaonaje? Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Give us your judgement therefore: is it allowable for us to pay a poll-tax to Caesar, or not?"
18 Lakini Yesu, akijua makusudi yao mabaya, akawaambia, “Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu kunitega?
Perceiving their wickedness, Jesus replied, "Why are you hypocrites trying to ensnare me?
19 Nionyesheni hiyo sarafu inayotumika kwa kulipia kodi.” Wakamletea dinari.
Show me the tribute coin." And they brought Him a shilling.
20 Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?”
"Whose likeness and inscription," He asked, "is this?"
21 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Basi Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
"Caesar's," they replied. "Pay therefore," He rejoined, "what is Caesar's to Caesar; and what is God's to God."
22 Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo wakamwacha, wakaenda zao.
They heard this, and were astonished; then left Him, and went their way.
23 Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza swali, wakisema,
On the same day a party of Sadducees came to Him, contending that there is no resurrection. And they put this case to Him.
24 “Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila kuwa na watoto, ndugu yake inampasa amwoe huyo mjane ili ampatie watoto huyo nduguye aliyekufa.’
"Teacher," they said, "Moses enjoined, 'If a man die childless, his brother shall marry his widow, and raise up a family for him.'
25 Basi palikuwa na ndugu saba miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa, na kwa kuwa hakuwa na watoto, akamwachia nduguye yule mjane.
Now we had among us seven brothers. The eldest of them married, but died childless, leaving his wife to his brother.
26 Ikatokea vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili, na wa tatu, hadi wote saba.
So also did the second and the third, down to the seventh,
27 Hatimaye, yule mwanamke naye akafa.
till the woman also died, after surviving them all.
28 Sasa basi, siku ya ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa wamemwoa huyo mwanamke?”
At the Resurrection, therefore, whose wife of the seven will she be? for they all married her."
29 Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui Maandiko wala uweza wa Mungu.
The reply of Jesus was, "You are in error, through ignorance of the Scriptures and of the power of God.
30 Wakati wa ufufuo, watu hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
For in the Resurrection, men neither marry nor are women given in marriage, but they are like angels in Heaven.
31 Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia, kwamba,
But as to the Resurrection of the dead, have you never read what God says to you,
32 ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo’? Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
'I am the God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob'? He is not the God of dead, but of living men."
33 Ule umati wa watu uliposikia hayo, ulishangaa sana kwa mafundisho yake.
All the crowd heard this, and were filled with amazement at His teaching.
34 Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, Mafarisayo wakakusanyika pamoja.
Now the Pharisees came up when they heard that He had silenced the Sadducees,
35 Mmoja wao, mtaalamu wa sheria, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema,
and one of them, an expounder of the Law, asked Him as a test question,
36 “Mwalimu, ni amri ipi katika Sheria iliyo kuu kuliko zote?”
"Teacher, which is the greatest Commandment in the Law?"
37 Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’
"'Thou shalt love the Lord thy God,'" He answered, "'with thy whole heart, thy whole soul, thy whole mind.'
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
This is the greatest and foremost Commandment.
39 Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’
And the second is similar to it: 'Thou shalt love thy fellow man as much as thyself.'
40 Amri hizi mbili ndizo msingi wa Sheria na Manabii.”
The whole of the Law and the Prophets is summed up in these two Commandments."
41 Wakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza,
While the Pharisees were still assembled there, Jesus put a question to them.
42 “Mnaonaje kuhusu Kristo? Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.”
"What think you about the Christ," He said, "whose son is He?" "David's," they replied.
43 Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Kristo ‘Bwana’? Kwa maana asema,
"How then," He asked, "does David, taught by the Spirit, call Him Lord, when he says,
44 “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
"'The Lord said to my Lord, sit at My right hand until I have put thy foes beneath thy feet'?
45 Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
"If therefore David calls Him Lord, how can He be his son?"
46 Hakuna mtu aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku hiyo hakuna aliyethubutu kumuuliza tena maswali.
No one could say a word in reply, nor from that day did any one venture again to put a question to Him.

< Mathayo 22 >