< Mathayo 2 >

1 Baada ya Yesu kuzaliwa katika mji wa Bethlehemu huko Uyahudi, wakati wa utawala wa Mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu
Now after the birth of Jesus, which took place at Bethlehem in Judaea in the reign of King Herod, excitement was produced in Jerusalem by the arrival of certain Magi from the east,
2 wakiuliza, “Yuko wapi huyo aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tumeona nyota yake ikitokea mashariki, nasi tumekuja kumwabudu.”
inquiring, "Where is the newly born king of the Jews? For we have seen his Star in the east, and have come here to do him homage."
3 Mfalme Herode aliposikia jambo hili aliingiwa na hofu sana pamoja na watu wote wa Yerusalemu.
Reports of this soon reached the king, and greatly agitated not only him but all the people of Jerusalem.
4 Herode akawaita pamoja viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, akawauliza ni mahali gani ambapo Kristo angezaliwa.
So he assembled all the High Priests and Scribes of the people, and anxiously asked them where the Christ was to be born.
5 Nao wakamwambia, “Katika Bethlehemu ya Uyahudi, kwa maana hivyo ndivyo ilivyoandikwa na nabii:
"At Bethlehem in Judaea," they replied; "for so it stands written in the words of the Prophet,
6 “‘Nawe, Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si mdogo miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana kutoka kwako atakuja mtawala atakayekuwa mchungaji wa watu wangu Israeli.’”
"'And thou, Bethlehem in the land of Judah, by no means the least honorable art thou among princely places in Judah! For from thee shall come a prince--one who shall be the Shepherd of My People Israel.'"
7 Ndipo Herode akawaita wale wataalamu wa nyota kwa siri na kutaka kujua kutoka kwao uhakika kamili wa wakati ile nyota ilionekana.
Thereupon Herod sent privately for the Magi and ascertained from them the exact time of the star's appearing.
8 Kisha akawatuma waende Bethlehemu akiwaambia, “Nendeni mkamtafute kwa bidii huyo mtoto. Nanyi mara mtakapomwona, mniletee habari ili na mimi niweze kwenda kumwabudu.”
He then directed them to go to Bethlehem, adding, "Go and make careful inquiry about the child, and when you have found him, bring me word, that I too may come and do him homage."
9 Baada ya kumsikia mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaenda zao, nayo ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama mahali pale alipokuwa mtoto.
After hearing what the king said, they went to Bethlehem, while, strange to say, the star they had seen in the east led them on until it came and stood over the place where the babe was.
10 Walipoiona ile nyota wakajawa na furaha kubwa mno.
When they saw the star, the sight filled them with intense joy.
11 Walipoingia ndani ya ile nyumba, wakamwona mtoto pamoja na Maria mama yake, wakamsujudu na kumwabudu yule mtoto Yesu. Ndipo wakafungua hazina zao, wakamtolea zawadi za dhahabu, uvumba na manemane.
So they entered the house; and when they saw the babe with His mother Mary, they prostrated themselves and did Him homage, and opening their treasure-chests offered gifts to Him--gold, frankincense, and myrrh.
12 Nao wakiisha kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Herode, wakarudi kwenda katika nchi yao kwa njia nyingine.
But being forbidden by God in a dream to return to Herod, they went back to their own country by a different route.
13 Walipokwisha kwenda zao, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kumtafuta huyu mtoto ili amuue.”
When they were gone, and angel of the Lord appeared to Joseph in a dream and said, "Rise: take the babe and His mother and escape to Egypt, and remain there till I bring you word. For Herod is about to make search for the child in order to destroy Him."
14 Kisha Yosefu akaondoka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake wakati wa usiku, nao wakaenda Misri
So Joseph roused himself and took the babe and His mother by night and departed into Egypt.
15 ambako walikaa mpaka Herode alipofariki. Hili lilifanyika ili litimie lile lililonenwa na Bwana kwa kinywa cha nabii kusema: “Nilimwita mwanangu kutoka Misri.”
There he remained till Herod's death, that what the Lord had said through the Prophet might be fulfilled, "Out of Egypt I called My Son."
16 Herode alipongʼamua kwamba wale wataalamu wa nyota wamemshinda kwa akili, alikasirika sana, naye akatoa amri ya kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kurudi chini katika mji wa Bethlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda alioambiwa na wale wataalamu wa nyota.
Then Herod, finding that the Magi had trifled with him, was furious, and sent and massacred all the boys under two years of age, in Bethlehem and all its neighbourhood, according to the date he had so carefully ascertained from the Magi.
17 Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia.
Then were these words, spoken by the Prophet Jeremiah, fulfilled,
18 “Sauti ilisikika huko Rama, maombolezo na kilio kikubwa, Raheli akilia kwa ajili ya wanawe, akikataa kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”
"A voice was heard in Ramah, wailing and bitter lamentation: It was Rachel bewailing her children, and she refused to be comforted because there were no more."
19 Baada ya Herode kufa, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto huko Misri
But after Herod's death an angel of the Lord appeared in a dream to Joseph in Egypt, and said to him,
20 na kusema, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mwende, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliokuwa wanatafuta uhai wa mtoto wamekufa.”
"Rise from sleep, and take the child and His mother, and go into the land of Israel, for those who were seeking the child's life are dead."
21 Basi Yosefu, akaondoka akamchukua mtoto na mama yake wakaenda mpaka nchi ya Israeli.
So he roused himself and took the child and His mother and came into the land of Israel.
22 Lakini aliposikia kwamba Arkelao alikuwa anatawala huko Uyahudi mahali pa Herode baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye akiisha kuonywa katika ndoto, akaenda zake sehemu za Galilaya,
But hearing that Archelaus had succeeded his father Herod on the throne of Judaea, he was afraid to go there; and being instructed by God in a dream he withdrew into Galilee,
23 akaenda akaishi katika mji ulioitwa Nazareti. Hivyo likawa limetimia neno lililonenwa na manabii, “Ataitwa Mnazarayo.”
and went and settled in a town called Nazareth, in order that these words spoken through the Prophets might be fulfilled, "He shall be called a Nazarene."

< Mathayo 2 >