< Mathayo 11 >

1 Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
When Jesus had concluded His instructions to His twelve disciples, He left in order to teach and to proclaim His Message in the neighbouring towns.
2 Yohana aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Kristo alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake
Now John had heard in prison about the Christ's doings, and he sent some of his disciples to inquire:
3 ili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
"Are you the Coming One, or is it a different person that we are to expect?"
4 Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona:
"Go and report to John what you see and hear," replied Jesus;
5 Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
"blind eyes receive sight, and cripples walk; lepers are cleansed, and deaf ears hear; the dead are raised to life, and the poor have the Good News proclaimed to them;
6 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
and blessed is every one who does not stumble and fall because of my claims."
7 Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa wanaondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
When the messengers had taken their leave, Jesus proceeded to say to the multitude concerning John, "What did you go out into the Desert to gaze at? A reed waving in the wind?
8 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari wako katika majumba ya wafalme.
But what did you go out to see? A man luxuriously dressed? Those who wear luxurious clothes are to be found in kings' palaces.
9 Basi mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
But why did you go out? To see a prophet? Yes, I tell you, and far more than a prophet.
10 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
This is he of whom it is written, "'See I am sending My messenger before Thy face, and he will make Thy road ready before Thee.'
11 Amin, nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni ni mkuu kuliko Yohana.
"I solemnly tell you that among all of woman born no greater has ever been raised up than John the Baptist; yet one who is of lower rank in the Kingdom of the Heavens is greater than he.
12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wanauteka.
But from the time of John the Baptist till now, the Kingdom of the Heavens has been suffering violent assault, and the violent have been seizing it by force.
13 Kwa maana manabii wote na Sheria walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
For all the Prophets and the Law taught until John.
14 Ikiwa mko tayari kukubali hilo, yeye ndiye yule Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema angekuja.
And (if you are willing to receive it) he is the Elijah who was to come.
15 Yeye aliye na masikio, na asikie.
Listen, every one who has ears!
16 “Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini? Kinafanana na watoto waliokaa sokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia,
"But to what shall I compare the present generation? It is like children sitting in the open places, who call to their playmates.
17 “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkuomboleza.’
"'We have played the flute to you,' they say, 'and you have not danced: we have sung dirges, and you have not beaten your breasts.'
18 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali wala hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
"For John came neither eating nor drinking, and they say, 'He has a demon.'
19 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nao wanasema, ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’ Lakini hekima huthibitishwa kuwa kweli kwa matendo yake.”
The Son of Man came eating and drinking, and they exclaim, 'See this man! --given to gluttony and tippling, and a friend of tax-gatherers and notorious sinners!' And yet Wisdom is vindicated by her actions."
20 Ndipo Yesu akaanza kushutumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu.
Then began He to upbraid the towns where most of His mighty works had been done--because they had not repented.
21 “Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
"Alas for thee, Chorazin!" He cried. "Alas for thee, Bethsaida! For had the mighty works been done in Tyre and Sidon which have been done in both of you, they would long ere now have repented, covered with sackcloth and ashes.
22 Lakini nawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
Only I tell you that it will be more endurable for Tyre and Sidon on the day of Judgement than for you.
23 Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. (Hadēs g86)
And thou, Capernaum, shalt thou be exalted even to Heaven? Even to Hades shalt thou descend. For had the mighty works been done in Sodom which have been done in thee, it would have remained until now. (Hadēs g86)
24 Lakini nakuambia kwamba, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ya hukumu kuliko wewe.”
Only I tell you all, that it will be more endurable for the land of Sodom on the day of Judgement than for thee."
25 Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo.
About that time Jesus exclaimed, "I heartily praise Thee, Father, Lord of Heaven and of earth, that Thou hast hidden these things from sages and men of discernment, and hast unveiled them to babes.
26 Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
Yes, Father, for such has been Thy gracious will.
27 “Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.
"All things have been handed over to me by my Father, and no one fully knows the Son except the Father, nor does any one fully know the Father except the Son and all to whom the Son chooses to reveal Him.
28 “Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
"Come to me, all you toiling and burdened ones, and I will give you rest.
29 Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu.
Take my yoke upon you and learn from me; for I am gentle and lowly in heart, and you will find rest for your souls.
30 Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”
For it is good to bear my yoke, and my burden is light."

< Mathayo 11 >