< Marko 4 >

1 Yesu akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Umati wa watu uliokuwa umekusanyika kumzunguka ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba ilimbidi Yesu aingie kwenye mashua iliyokuwa baharini na kuketi humo, nao watu wote walikuwa ufuoni mwa bahari.
Once more He began to teach by the side of the Lake, and a vast multitude of people came together to listen to Him. He therefore went on board the boat and sat there, a little way from the land; and all the people were on the shore close to the water.
2 Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, naye katika mafundisho yake akasema:
Then He proceeded to teach them many lessons in figurative language; and in His teaching He said,
3 “Sikilizeni! Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
"Listen: the sower goes out to sow.
4 Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
As he sows, some of the seed falls by the way-side, and the birds come and peck it up.
5 Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
Some falls on the rocky ground where it finds but little earth, and it shoots up quickly because it has no depth of soil;
6 Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
but when the sun is risen, it is scorched, and through having no root it withers away.
7 Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea, hivyo haikutoa mazao.
Some, again, falls among the thorns; and the thorns spring up and stifle it, so that it yields no crop.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri, zikaota vizuri na kukua, zikatoa mazao, moja mara thelathini, nyingine mara sitini, na nyingine mara mia moja.”
But some of the seed falls into good ground, and gives a return: it comes up and increases, and yields thirty, sixty, or a hundred-fold."
9 Kisha Yesu akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
"Listen," He added, "every one who has ears to listen with!"
10 Alipokuwa peke yake, watu waliokuwepo naye pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili wakamuuliza kuhusu mifano yake.
When He was alone, the Twelve and the others who were about Him requested Him to explain His figurative language.
11 Naye akawaambia, “Ninyi mmepewa kujua siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kwa wale walioko nje, kila kitu husemwa kwao kwa mifano,
"To you," He replied, "has been entrusted the secret truth concerning the Kingdom of God; but to those others outside your number all this is spoken in figurative language;
12 ili, “‘daima waone lakini wasitambue, daima wasikie lakini wasielewe; wasije wakageuka, wakatubu na kusamehewa!’”
that "'They may look and look but not see, and listen and listen but not understand, lest perchance they should return and be pardoned.'"
13 Kisha Yesu akawauliza, “Hamwelewi maana ya mfano huu? Basi mtaelewaje mifano mingine?
"Do you all miss the meaning of this parable?" He added; "how then will you understand the rest of my parables?"
14 Yule mpanzi hupanda neno.
"What the sower sows is the Message.
15 Hawa ndio wale walio kando ya njia ambako neno lilipandwa. Walisikiapo neno, Shetani huja mara na kulinyakua lile neno lililopandwa ndani yao.
Those who receive the seed by the way-side are those in whom the Message is sown, but, when they have heard it, Satan comes at once and carries away the Message sown in them.
16 Nazo zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo wenye miamba, ni wale wanaolisikia neno, na mara hulipokea kwa furaha.
In the same way those who receive the seed on the rocky places are those who, when they have heard the Message, at once accept it joyfully,
17 Lakini kwa kuwa hawana mizizi, wao hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, mara wao huiacha imani.
but they have no root within them. They last for a time; then, when suffering or persecution comes because of the Message, they are immediately overthrown.
18 Lakini wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye miiba, hulisikia lile neno;
Others there are who receive the seed among the thorns: these are they who have heard the Message,
19 lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae. (aiōn g165)
but worldly cares and the deceitfulness of wealth and the excessive pursuit of other objects come in and stifle the Message, and it becomes unfruitful. (aiōn g165)
20 Wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri, hulisikia lile neno, wakalipokea na kuzaa mazao. Wao huzaa mara thelathini, au mara sitini, au mara mia ya mbegu iliyopandwa.”
Those, on the other hand, who have received the seed on the good ground, are all who hear the Message and welcome it, and yield a return of thirty, sixty, or a hundred fold."
21 Akawaambia, “Je, taa huwashwa na kufunikwa chini ya kikapu au mvunguni mwa kitanda? Je, haiwashwi na kuwekwa juu ya kinara chake?
He went on to say, "Is the lamp brought in in order to be put under the bushel or under the bed? Is it not rather in order that it may be placed on the lampstand?
22 Kwa kuwa hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa, wala hakuna jambo lolote la siri ambalo halitaletwa nuruni.
Why, there is nothing hidden except with a view to its being ultimately disclosed, nor has anything been made a secret but that it may at last come to light.
23 Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
Listen, every one who has ears to listen with!"
24 Naye akawaambia, “Kuweni waangalifu na yale mnayosikia. Kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa ninyi, hata na zaidi.
He also said to them, "Take care what you hear. With what measure you measure, it will be measured to you, and that with interest.
25 Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.”
For those who have will have more given them; and from those who have not, even what they have will be taken away."
26 Pia akawaambia, “Ufalme wa Mungu unafanana na mtu apandaye mbegu shambani.
Another saying of His was this: "The Kingdom of God is as if a man scattered seed over the ground:
27 Akiisha kuzipanda, usiku na mchana, akiwa amelala au ameamka, mbegu huota na kukua pasipo yeye kujua ikuavyo.
he spends days and nights, now awake, now asleep, while the seed sprouts and grows tall, he knows not how.
28 Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke.
Of itself the land produces the crop-- first the blade, then the ear; afterwards the perfect grain is seen in the ear.
29 Lakini nafaka inapokuwa imekomaa, mara mkulima huingia shambani na mundu wa kuvunia, maana mavuno yamekuwa tayari.”
But no sooner is the crop ripe, than he sends the reapers, because the time of harvest has come."
30 Akawaambia tena, “Tuufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Au tutumie mfano gani ili kuueleza?
Another saying of His was this: "How are we to picture the Kingdom of God? or by what figure of speech shall we represent it?
31 Ni kama punje ya haradali, ambayo ni mbegu ndogo sana kuliko mbegu zote zinazopandwa ardhini.
It is like a mustard-seed, which, when sown in the earth, is the smallest of all the seeds in the world;
32 Lakini ikishaota, hukua ikawa mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, ikawa na matawi makubwa hata ndege wa angani wanaweza kujenga viota kwenye matawi yake.”
yet when sown it springs up and becomes larger than all the herbs, and throws out great branches, so that the birds build under its shadow."
33 Kwa mifano mingine mingi kama hii Yesu alinena nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulielewa.
With many such parables He used to speak the Message to them according to their capacity for receiving it.
34 Hakusema nao neno lolote pasipo mfano. Lakini alipokuwa na wanafunzi wake, aliwafafanulia kila kitu.
But except in figurative language He spoke nothing to them; while to His own disciples He expounded everything, in private.
35 Siku hiyo ilipokaribia jioni, aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo.”
The same day, in the evening, He said to them, "Let us cross to the other side."
36 Wakauacha ule umati wa watu, na wakamchukua vile alivyokuwa kwenye mashua. Palikuwa pia na mashua nyingine nyingi pamoja naye.
So they got away from the crowd, and took Him--as He was--in the boat; and other boats accompanied Him.
37 Kukawa na dhoruba kali, nayo mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikawa karibu kujaa maji.
But a heavy squall came on, and the waves were now dashing into the boat, so that it was fast filling.
38 Yesu alikuwa katika shetri, akiwa analala juu ya mto. Wanafunzi wake wakamwamsha, wakamwambia, “Mwalimu, hujali kama tunazama?”
But He Himself was in the stern asleep, with His head on the cushion: so they woke Him. "Rabbi," they cried, "is it nothing to you that we are drowning?"
39 Akaamka, akaukemea ule upepo, akayaambia yale mawimbi, “Uwe kimya! Tulia!” Ule upepo ukatulia, kukawa shwari kabisa.
So He roused Himself and rebuked the wind, and said to the waves, "Silence! Be still!" The wind sank, and a perfect calm set in.
40 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa nini mnaogopa hivyo? Je, bado hamna imani?”
"Why are you so timid?" He asked; "have you still no faith?"
41 Nao wakawa wameogopa sana, wakaulizana, “Ni nani huyu ambaye hata upepo na mawimbi vinamtii?”
Then they were filled with terror, and began to say to one another, "Who is this, then? For even wind and sea obey Him."

< Marko 4 >