< Marko 12 >

1 Yesu akaanza kusema nao kwa mifano, akawaambia: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akachimba shimo ndani yake kwa ajili ya shinikizo la kusindika divai, na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha shamba hilo la mizabibu kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwenda nchi nyingine.
Then He began to speak to them in figurative language. "There was once a man," He said, "who planted a vineyard, fenced it round, dug a pit for the wine-tank, and built a strong lodge. Then he let the place to vine-dressers and went abroad.
2 Wakati wa mavuno ulipofika, mwenye shamba akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili kuchukua sehemu yake ya mavuno ya shamba la mizabibu kutoka kwa hao wapangaji.
At vintage-time he sent one of his servants to receive from the vine-dressers a share of the grapes.
3 Lakini wale wakulima walimkamata yule mtumishi, wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
But they seized him, beat him cruelly and sent him away empty-handed.
4 Kisha yule mwenye shamba akamtuma mtumishi mwingine kwao; nao wale wakulima wakampiga kichwani na kumfanyia mambo ya aibu.
Again he sent to them another servant: and as for him, they wounded him in the head and treated him shamefully.
5 Kisha akamtuma mtumishi mwingine, naye huyo wakamuua. Akawatuma wengine wengi; baadhi yao wakawapiga, na wengine wakawaua.
Yet a third he sent, and him they killed. And he sent many besides, and them also they ill-treated, beating some and killing others.
6 “Mwenye shamba alikuwa bado na mmoja wa kumtuma, mwanawe aliyempenda. Hatimaye akamtuma akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
He had still one left whom he could send, a dearly-loved son: him last of all he sent, saying, "'They will treat my son with respect.'
7 “Lakini wale wapangaji wakasemezana pamoja, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, nao urithi utakuwa wetu.’
"But those men--the vine-dressers--said to one another, "'Here is the heir: come, let us kill him, and then the property will one day be ours.'
8 Hivyo wakamchukua na kumuua, wakamtupa nje ya lile shamba la mizabibu.
"So they took him and killed him, and flung his body outside the vineyard.
9 “Sasa basi yule mwenye shamba atafanya nini? Atakuja na kuwaua hao wapangaji, kisha atawapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.
What, therefore, will the owner of the vineyard do?" "He will come and put the vine-dressers to death," they said; "and will give the vineyard to others."
10 Je, hamjasoma Andiko hili: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni;
"Have you not read even this passage," He added, "'The stone which the builders rejected has become the Cornerstone:
11 Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni ajabu machoni petu’?”
this Cornerstone came from the Lord, and is wonderful in our esteem?'"
12 Walipotambua kuwa amesema mfano huo kwa ajili yao, wakataka kumkamata, lakini wakaogopa ule umati wa watu. Wakamwacha, wakaondoka, wakaenda zao.
And they kept looking out for an opportunity to seize Him, but were afraid of the people; for they saw that in this parable He had referred to them. So they left Him and went away.
13 Baadaye wakawatuma baadhi ya Mafarisayo na Maherode ili kwenda kumtega Yesu katika yale anayosema.
Their next step was to send to Him some of the Pharisees and of Herod's partisans to entrap Him in conversation.
14 Wakamjia, wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu. Wewe huyumbishwi na wanadamu, kwa kuwa huna upendeleo. Lakini wewe huifundisha njia ya Mungu katika kweli. Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?
So they came to Him. "Rabbi," they said, "we know that you are a truthful man and you do not fear any one; for you do not recognize human distinctions, but teach God's way truly. Is it allowable to pay poll-tax to Caesar, or not?
15 Je, tulipe kodi au tusilipe?” Lakini Yesu alijua unafiki wao. Akawauliza “Mbona mnajaribu kunitega? Nileteeni hiyo dinariniione.”
Shall we pay, or shall we refuse to pay?" But He, knowing their hypocrisy, replied, "Why try to ensnare me? Bring me a shilling for me to look at."
16 Wakamletea hiyo sarafu. Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?” Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.”
They brought one; and He asked them, "Whose is this likeness and this inscription?" "Caesar's," they replied.
17 Ndipo Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.” Nao wakamstaajabia sana.
"What is Caesar's," replied Jesus, "pay to Caesar--and what is God's, pay to God." And they wondered exceedingly at Him.
18 Kisha Masadukayo, wale wasemao kuwa hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu,
Then came to Him a party of Sadducees, a sect which denies that there is any Resurrection; and they proceeded to question Him.
19 wakasema, “Mwalimu, Mose alituandikia kuwa kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
"Rabbi," they said, "Moses made it a law for us: 'If a man's brother should die and leave a wife, but no child, the man shall marry the widow and raise up a family for his brother.'
20 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa pasipo kuwa na mtoto yeyote.
There were once seven brothers, the eldest of whom married a wife, but at his death left no family.
21 Wa pili akamwoa yule mjane, lakini naye akafa bila kuacha mtoto yeyote. Ikawa vivyo hivyo kwa yule wa tatu.
The second married her, and died, leaving no family; and the third did the same.
22 Hakuna hata mmojawapo wa hao ndugu wote saba aliyeacha mtoto. Hatimaye yule mwanamke naye akafa.
And so did the rest of the seven, all dying childless. Finally the woman also died.
23 Kwa hiyo wakati wa ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
At the Resurrection whose wife will she be? For they all seven married her."
24 Yesu akawajibu, “Je, hampotoki kwa sababu hamfahamu Maandiko wala uweza wa Mungu?
"Is not this the cause of your error," replied Jesus--"your ignorance alike of the Scriptures and of the power of God?
25 Wafu watakapofufuka, hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
For when they have risen from among the dead, men do not marry and women are not given in marriage, but they are as angels are in Heaven.
26 Basi kuhusu wafu kufufuliwa, je hamjasoma katika Kitabu cha Mose jinsi Mungu alivyosema na Mose kutoka kile kichaka akisema, ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, na Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo?’
But as to the dead, that they rise to life, have you never read in the Book of Moses, in the passage about the Bush, how God said to him, 'I am the God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob?'
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai. Kwa hiyo mmekosea kabisa.”
He is not the God of dead, but of living men. You are in grave error."
28 Mwalimu mmoja wa sheria akaja, akawasikia wakijadiliana. Akiona kwamba Yesu amewajibu vyema, naye akamuuliza, “Katika amri zote, ni ipi iliyo kuu?”
Then one of the Scribes, who had heard them disputing and well knew that Jesus had given them an answer to the point, and a forcible one, came forward and asked Him, "Which is the chief of all the Commandments?"
29 Yesu akajibu, “Amri iliyo kuu ndiyo hii: ‘Sikia ee Israeli. Bwana Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
"The chief Commandment," replied Jesus, "is this: 'Hear, O Israel! The Lord our God is one Lord;
30 Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.’
and thou shalt love the Lord thy God with thy whole heart, thy whole soul, thy whole mind, and thy whole strength.'
31 Ya pili ndiyo hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.”
"The second is this: 'Thou shalt love thy fellow man as thou lovest thyself.' "Other Commandment greater than these there is none."
32 Yule mwalimu wa sheria akamwambia Yesu, “Mwalimu, umejibu vyema kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye.
So the Scribe said to Him, "Rightly, in very truth, Rabbi, have you said that He stands alone, and there is none but He;
33 Kumpenda Mungu kwa moyo wote na kwa akili zote na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama mtu anavyojipenda mwenyewe ni bora zaidi kuliko kutoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu zote.”
and To love Him with all one's heart, with all one's understanding, and with all one's strength, and to love one's fellow man no less than oneself, is far better than all our whole burnt-offerings and sacrifices."
34 Yesu alipoona kwamba amejibu kwa busara, akamwambia, “Wewe hauko mbali na Ufalme wa Mungu.” Tangu wakati huo, hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
Perceiving that the Scribe had answered wisely Jesus said to him, "You are not far from the Kingdom of God." No one from that time forward ventured to put any question to Him.
35 Yesu alipokuwa akifundisha Hekaluni, akauliza, “Imekuwaje walimu wa sheria wanasema kwamba Kristoni Mwana wa Daudi?
But, while teaching in the Temple, Jesus asked, "How is it the Scribes say that the Christ is a son of David?
36 Kwa maana Daudi mwenyewe, akinena kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu, alisema: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
David himself said, taught by the Holy Spirit, "'The Lord said to my Lord, Sit at My right hand, until I have made thy foes a footstool under thy feet.'
37 Kwa hiyo Daudi mwenyewe anamwita ‘Bwana.’ Awezaje basi yeye kuwa mwanawe?” Ule umati wote wa watu wakamsikiliza kwa furaha.
"David himself calls Him 'Lord:' how then can He be his son?" And the mass of people found pleasure in listening to Jesus.
38 Alipokuwa akifundisha, Yesu alisema, “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni.
Moreover in the course of His teaching He said, "Be on your guard against the Scribes who like to walk about in long robes and to be bowed to in places of public resort,
39 Pia wao hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kupewa nafasi za heshima katika karamu.
and to occupy the best seats in the synagogues and at dinner parties,
40 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
and who swallow up the property of widows and then mask their wickedness by making long prayers: these men will receive far heavier punishment."
41 Kisha Yesu akaketi mkabala na sehemu ambapo sadaka zilikuwa zinawekwa na kuangalia umati wa watu wakiweka fedha zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu. Matajiri wengi wakaweka kiasi kikubwa cha fedha.
Having taken a seat opposite the Treasury, He observed how the people were dropping money into the Treasury, and that many of the wealthy threw in large sums.
42 Lakini mjane mmoja maskini akaja na kuweka sarafu mbili ndogo za shaba zenye thamani ya senti mbili.
But there came one poor widow and dropped in two farthings, equal in value to a halfpenny.
43 Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka katika sanduku la hazina zaidi ya watu wengine wote.
So He called His disciples to Him and said, "In solemn truth I tell you that this widow, poor as she is, has thrown in more than all the other contributors to the Treasury;
44 Wengine wote wametoa kutokana na ziada ya mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake, akaweka kila kitu alichokuwa nacho, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
for they have all contributed out of what they could well spare, but she out of her need has thrown in all she possessed--all she had to live on."

< Marko 12 >