< Marko 10 >

1 Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
Soon on His feet once more, He enters the district of Judaea and crosses the Jordan: again the people flock to Him, and ere long, as was usual with Him, He was teaching them once more.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
Presently a party of Pharisees come to Him with the question--seeking to entrap Him, "May a man divorce his wife?"
3 Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
"What rule did Moses lay down for you?" He answered.
4 Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
"Moses," they said, "permitted a man to draw up a written notice of divorce, and to send his wife away."
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
"It was in consideration of your stubborn hearts," said Jesus, "that Moses enacted this law for you;
6 Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
but from the beginning of the creation the rule was, 'Male and female did God make them.
7 Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
For this reason a man shall leave his father and his mother, and shall cling to his wife,
8 Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
and the two shall be one'; so that they are two no longer, but 'one.'
9 Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
What, therefore, God has joined together let not man separate."
10 Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
Indoors the disciples began questioning Jesus again on the same subject.
11 Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
He replied, "Whoever divorces his wife and marries another woman, commits adultery against the first wife;
12 Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
and if a woman puts away her husband and marries another man, she commits adultery."
13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
One day people were bringing young children to Jesus for Him to touch them, but the disciples interfered.
14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
Jesus, however, on seeing this, was moved to indignation, and said to them, "Let the little children come to me: do not hinder them; for to those who are childlike the Kingdom of God belongs.
15 Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
In solemn truth I tell you that no one who does not receive the Kingdom of God like a little child will by any possibility enter it."
16 Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
Then He took them in His arms and blessed them lovingly, one by one, laying His hands upon them.
17 Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
As He went out to resume His journey, there came a man running up to Him, who knelt at His feet and asked, "Good Rabbi, what am I to do in order to inherit the Life of the Ages?" (aiōnios g166)
18 Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
"Why do you call me good?" asked Jesus in reply; "there is no one truly good except One--that is, God.
19 Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
You know the Commandments--'Do not murder;' 'Do not commit adultery;' 'Do not steal;' 'Do not lie in giving evidence;' 'Do not defraud;' 'Honour thy father and thy mother.'"
20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
"Rabbi," he replied, "all these Commandments I have carefully obeyed from my youth."
21 Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
Then Jesus looked at him and loved him, and said, "One thing is lacking in you: go, sell all you possess and give the proceeds to the poor, and you shall have riches in Heaven; and come and be a follower of mine."
22 Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
At these words his brow darkened, and he went away sad; for he was possessed of great wealth.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
Then looking round on His disciples Jesus said, "With how hard a struggle will the possessors of riches enter the Kingdom of God!"
24 Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
The disciples were amazed at His words. Jesus, however, said again, "Children, how hard a struggle is it for those who trust in riches to enter the Kingdom of God!
25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
It is easier for a camel to go through the eye of a needle than for a rich man to enter the Kingdom of God."
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
They were astonished beyond measure, and said to one another, "Who then can be saved?"
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
Jesus looking on them said, "With men it is impossible, but not with God; for everything is possible with God."
28 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
"Remember," said Peter to Him, "that we forsook everything and have become your followers."
29 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
"In solemn truth I tell you," replied Jesus, "that there is no one who has forsaken house or brothers or sisters, or mother or father, or children or lands, for my sake and for the sake of the Good News,
30 ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn g165, aiōnios g166)
but will receive a hundred times as much now in this present life--houses, brothers, sisters, mothers, children, lands--and persecution with them--and in the coming age the Life of the Ages. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
But many who are now first will be last, and the last, first."
32 Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
They were still on the road going up to Jerusalem, and Jesus was walking ahead of them; they were full of wonder, and some, though they followed, did so with fear. Then, once more calling to Him the Twelve, He began to tell them what was about to happen to Him.
33 Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
"See," He said, "we are going up to Jerusalem, where the Son of Man will be betrayed to the High Priests and the Scribes. They will condemn Him to death, and will hand Him over to the Gentiles;
34 ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
they will insult Him in cruel sport, spit on Him, scourge Him, and put Him to death; but on the third day He will rise to life again."
35 Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
Then James and John, the sons of Zabdi, came up to Him and said, "Rabbi, we wish you would grant us whatever request we make of you."
36 Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
"What would you have me do for you?" He asked.
37 Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
"Allow us," they replied, "to sit one at your right hand and the other at your left hand, in your glory."
38 Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
"You know not," said He, "what you are asking. Are you able to drink out of the cup from which I am to drink, or to be baptized with the baptism with which I am to be baptized?"
39 Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
"We are able," they replied. "Out of the cup," said Jesus, "from which I am to drink you shall drink, and with the baptism with which I am to be baptized you shall be baptized;
40 lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
but as to sitting at my right hand or at my left, that is not mine to give: it will be for those for whom it is reserved."
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
The other ten, hearing of it, were at first highly indignant with James and John.
42 Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
Jesus, however, called them to Him and said to them, "You are aware how those who are deemed rulers among the Gentiles lord it over them, and their great men make them feel their authority;
43 Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
but it is not to be so among you. No, whoever desires to be great among you must be your servant;
44 na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
and whoever desires to be first among you must be the bondservant of all.
45 Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
For the Son of Man also did not come to be waited upon, but to wait on others, and to give His life as the redemption-price for a multitude of people."
46 Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
They came to Jericho; and as He was leaving that town--Himself and His disciples and a great crowd--Bartimaeus (the son of Timaeus), a blind beggar, was sitting by the way-side.
47 Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Hearing that it was Jesus the Nazarene, he began to cry out, "Son of David, Jesus, have pity on me."
48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Many angrily told him to leave off shouting; but he only cried out all the louder, "Son of David, have pity on me."
49 Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
Then Jesus stood still. "Call him," He said. So they called the blind man. "Cheer up," they said; "rise, he is calling you."
50 Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
The man flung away his outer garment, sprang to his feet, and came to Jesus.
51 Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
"What shall I do for you?" said Jesus. "Rabboni," replied the blind man, "let me recover my sight."
52 Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.
"Go," said Jesus, "your faith has cured you." Instantly he regained his sight, and followed Him along the road.

< Marko 10 >