< Luka 9 >

1 Yesu kisha akawaita wale kumi na wawili pamoja, akawapa mamlaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote,
Then calling the Twelve together He conferred on them power and authority over all the demons and to cure diseases;
2 kisha akawatuma waende wakahubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
and sent them out to proclaim the Kingdom of God and to cure the sick.
3 Akawaagiza akisema, “Msichukue chochote safarini: sio fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, hata msichukue kanzu ya ziada.
And He commanded them, "Take nothing for your journey; neither stick nor bag nor bread nor money; and do not have an extra under garment.
4 Katika nyumba yoyote mwingiayo, kaeni humo hadi mtakapoondoka katika mji huo.
Whatever house you enter, make that your home, and from it start afresh.
5 Kama watu wasipowakaribisha, mnapoondoka katika mji wao, kungʼuteni mavumbi kutoka kwenye miguu yenu ili kuwa ushuhuda dhidi yao.”
Wherever they refuse to receive you, as you leave that town shake off the very dust from your feet as a protest against them."
6 Hivyo wale wanafunzi wakaondoka wakaenda kutoka kijiji hadi kijiji, wakihubiri habari njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
So they departed and visited village after village, spreading the Good News and performing cures everywhere.
7 Basi Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za yote yaliyotendeka. Naye akafadhaika, kwa kuwa baadhi ya watu walikuwa wakisema Yohana Mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu.
Now Herod the Tetrarch heard of all that was going on; and he was bewildered because of its being said by some that John had come back to life,
8 Wengine wakasema Eliya amewatokea, na wengine wakasema kwamba mmoja wa manabii wa kale amefufuka.
by others that Elijah had appeared, and by others that some one of the ancient Prophets had come back to life.
9 Herode akasema, “Yohana nilimkata kichwa. Lakini ni nani huyu ambaye ninasikia mambo kama haya kumhusu?” Akatamani sana kumwona.
And Herod said, "John I have beheaded; but who is this, of whom I hear such reports?" And he sought for an opportunity of seeing Jesus.
10 Mitume wake waliporudi, wakamweleza Yesu yote waliyofanya. Akawachukua, akaenda nao faraghani mpaka mji uitwao Bethsaida.
The Apostles, on their return, related to Jesus all they had done. Then He took them and withdrew to a quiet retreat, to a town called Bethsaida.
11 Lakini umati wa watu ukafahamu alikokwenda, ukamfuata. Akawakaribisha na kunena nao kuhusu Ufalme wa Mungu na kuwaponya wale wote waliokuwa wanahitaji uponyaji.
But the immense crowd, aware of this, followed Him; and receiving them kindly He proceeded to speak to them of the Kingdom of God, and those who needed to be restored to health, He cured.
12 Ilipokaribia jioni, wale mitume kumi na wawili wakaenda kwa Yesu na kumwambia, “Waage makutano ili waende vijijini jirani na mashambani, ili wapate chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tuko nyikani.”
Now when the day began to decline, the Twelve came to Him and said, "Send the people away, that they may go to the villages and farms round about and find lodging and a supply of food; because here we are in an uninhabited district."
13 Yesu akawajibu, “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakajibu, “Hatuna zaidi ya mikate mitano na samaki wawili. Labda twende tukanunue chakula cha kuwatosha watu hawa wote.”
"You yourselves," He said, "must give them food." "We have nothing," they replied, "but five loaves and a couple of fish, unless indeed we were to go and buy provisions for all this host of people."
14 Walikuwako wanaume wapatao 5,000. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Waketisheni katika makundi ya watu hamsini hamsini.”
(For there were about 5,000 adult men.) But He said to His disciples, "Make them sit down in parties of about fifty each."
15 Wanafunzi wakafanya hivyo, wakawaketisha wote.
They did so, making them all, without exception, sit down.
16 Yesu akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akavibariki na kuvimega. Kisha akawapa wanafunzi ili wawagawie watu.
Then He took the five loaves and the two fish, and looking up to Heaven He blessed them and broke them into portions which He gave to the disciples to distribute to the people.
17 Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
So they ate and were fully satisfied, all of them; and what they had remaining over was gathered up, twelve baskets of fragments.
18 Wakati mmoja, Yesu alipokuwa akiomba faraghani, nao wanafunzi wake wakiwa pamoja naye, akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
One day when He was praying by Himself the disciples were present; and He asked them, "Who do the people say that I am?"
19 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema kwamba ni mmoja wa manabii wa kale amefufuka kutoka kwa wafu.”
"John the Baptist," they replied; "but others say Elijah; and others that some one of the ancient Prophets has come back to life."
20 Kisha akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo wa Mungu.”
"But you," He asked, "who do you say that I am?" "God's Anointed One," replied Peter.
21 Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote jambo hilo.
And Jesus strictly forbad them to tell this to any one;
22 Yesu akasema, “Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na itampasa auawe, lakini siku ya tatu kufufuliwa kutoka mauti.”
and He said, "The Son of Man must suffer much cruelty, be rejected by the Elders and High Priests and Scribes, and be put to death, and on the third day be raised to life again."
23 Kisha akawaambia wote, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
And He said to all, "If any one is desirous of following me, let him ignore self and take up his cross day by day, and so be my follower.
24 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
For whoever desires to save his life shall lose it, and whoever loses his life for my sake shall save it.
25 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akapoteza au kuangamiza nafsi yake?
Why, what benefit is it to a man to have gained the whole world, but to have lost or forfeited his own self.
26 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu atakapokuja katika utukufu wake na katika utukufu wa Baba, pamoja na malaika watakatifu.
For whoever shall have been ashamed of me and my teachings, of him the Son of Man will be ashamed when He comes in His own and the Father's glory and in that of the holy angels.
27 Amin, nawaambia, wako baadhi ya watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu.”
I tell you truly that there are some of those who stand here who will certainly not taste death till they have seen the Kingdom of God."
28 Yapata siku nane baada ya Yesu kusema hayo, aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana, akaenda nao mlimani kuomba.
It was about eight days after this that Jesus, taking with Him Peter, John, and James, went up the mountain to pray.
29 Alipokuwa akiomba, sura ya uso wake ikabadilika, nayo mavazi yake yakametameta kama mwanga wa umeme wa radi.
And while He was praying the appearance of His face underwent a change, and His clothing became white and radiant.
30 Ghafula wakawaona watu wawili, ndio Mose na Eliya, wakizungumza naye.
And suddenly there were two men conversing with Him, who were Moses and Elijah.
31 Walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea huko Yerusalemu.
They came in glory, and kept speaking about His death, which He was so soon to undergo in Jerusalem.
32 Petro na wenzake walikuwa wamelala usingizi mzito. Walipoamka, wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
Now Peter and the others were weighed down with sleep; but, keeping themselves awake all through, they saw His glory, and the two men standing with Him.
33 Mose na Eliya walipokuwa wanaondoka, Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri tukae hapa! Tutajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.” Lakini Petro alikuwa hajui asemacho.
And when they were preparing to depart from Him, Peter said to Jesus, "Rabbi, we are thankful to you that we are here. Let us put up three tents--one for you, one for Moses, and one for Elijah." He did not know what he was saying.
34 Alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu, likawafunika, nao wakaogopa walipoingia mle kwenye wingu.
But while he was thus speaking, there came a cloud which spread over them; and they were awe-struck when they had entered into the cloud.
35 Sauti ikatoka kwenye lile wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, niliyemchagua. Msikieni yeye.”
Then there came a voice from within the cloud: "This is My Son, My Chosen One: listen to Him."
36 Baada ya sauti hiyo kusema, walimkuta Yesu akiwa peke yake. Wale wanafunzi wakalihifadhi jambo hili, wala kwa wakati huo hawakumwambia mtu yeyote yale waliyokuwa wameyaona.
After this voice had spoken, Jesus was found alone. They kept it to themselves, and said not a word to any one at that time about what they had seen.
37 Kesho yake waliposhuka kutoka mlimani, alikutana na umati mkubwa wa watu.
On the following day, when they were come down from the mountain, a great crowd came to meet Him;
38 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akapaza sauti, akasema, “Mwalimu, naomba umwangalie mwanangu, kwani ndiye mtoto wangu wa pekee.
and a man from the crowd called out, "Rabbi, I beg you to pity my son, for he is my only child.
39 Mara kwa mara pepo mchafu humpagaa na kumfanya apige kelele, kisha humwangusha na kumtia kifafa hata akatokwa na povu kinywani. Huyo pepo mchafu anamtesa sana, na hamwachi ila mara chache.
At times a spirit seizes him and he suddenly cries out. It convulses him, and makes him foam at the mouth, and does not leave him till it has well-nigh covered him with bruises.
40 Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
I entreated your disciples to expel the spirit, but they could not."
41 Yesu akawajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”
"O unbelieving and perverse generation!" replied Jesus; "how long shall I be with you and bear with you? Bring your son here to me."
42 Hata yule mtoto alipokuwa akija, yule pepo mchafu akamwangusha, akamtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu amtoke, akamponya yule mtoto, na akamrudisha kwa baba yake.
Now while the youth was coming, the spirit dashed him to the ground and cruelly convulsed him. But Jesus rebuked the foul spirit, and cured the youth and gave him back to his father.
43 Watu wote wakastaajabia uweza mkuu wa Mungu. Wakati bado watu walikuwa wanastaajabia hayo yote aliyokuwa akiyafanya Yesu, yeye akawaambia wanafunzi wake:
And all were awe-struck at the mighty power of God. And while every one was expressing wonder at all that He was doing, He said to his disciples,
44 “Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.”
"As for you, store these my sayings in your memory; for, before long, the Son of Man will be betrayed into the hands of men."
45 Lakini wao hawakuelewa alimaanisha nini. Maana ya maneno hayo ilifichika kwao, hivyo hawakuyaelewa, nao wakaogopa kumuuliza maana yake.
But they did not understand His meaning: it was veiled from them that they might not perceive it, and they were afraid to ask Him about it.
46 Kukazuka mabishano miongoni mwa wanafunzi kuhusu ni nani miongoni mwao atakayekuwa mkuu kuliko wote.
Now there arose a dispute among them, which of them was to be the greatest.
47 Lakini Yesu akayatambua mawazo yao, naye akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kando yake.
And Jesus, knowing the reasoning that was in their hearts, took a young child and made him stand by His side
48 Kisha akawaambia, “Yeyote amkaribishaye mtoto huyu mdogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi, na yeyote atakayenikaribisha mimi, atakuwa amemkaribisha yeye aliyenituma. Kwa maana yeye aliye mdogo miongoni mwenu, ndiye aliye mkuu kuliko wote.”
and said to them, "Whoever for my sake receives this little child, receives me; and whoever receives me, receives Him who sent me. For the lowliest among you all--he is the greatest."
49 Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamzuia, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
"Rabbi," replied John, "we have seen a man making use of your name to expel demons; and we forbad him, because he does not come with us."
50 Yesu akasema, “Msimzuie, kwa sababu yeyote ambaye si kinyume nanyi, yu upande wenu.”
"Do not forbid him," said Jesus, "for he who is not against you is on your side."
51 Wakati ulipokaribia wa yeye kuchukuliwa mbinguni, alikaza uso wake kwenda Yerusalemu.
Now when the time drew near for Him to be received up again into Heaven, He proceeded with fixed purpose towards Jerusalem, and sent messengers before Him.
52 Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu;
They went and entered a village of the Samaritans to make ready for Him.
53 lakini watu wa kijiji kile hawakumkaribisha kwa sababu alikuwa anakwenda zake Yerusalemu.
But the people there would not receive Him, because He was evidently going to Jerusalem.
54 Wanafunzi wake, yaani Yakobo na Yohana, walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuagize moto kutoka mbinguni ili uwaangamize?”
When the disciples James and John saw this, they said, "Master, do you wish us to order fire to come down from Heaven and consume them?"
55 Yesu akageuka na kuwakemea,
But He turned and rebuked them.
56 nao wakaenda kijiji kingine.
And they went to another village.
57 Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote uendako.”
And, as they proceeded on their way, a man came to Him and said, "I will follow you wherever you go."
58 Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”
"The foxes have holes," said Jesus, "and the birds of the air have nests; but the Son of Man has nowhere to lay His head."
59 Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”
"Follow me," He said to another. "Master," the man replied, "allow me first to go and bury my father."
60 Yesu akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze Ufalme wa Mungu.”
"Leave the dead," Jesus rejoined, "to bury their own dead; but you must go and announce far and wide the coming of the Kingdom of God."
61 Mtu mwingine akamwambia, “Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa yangu.”
"Master," said yet another, "I will follow you; but allow me first to go and say good-bye to my friends at home."
62 Yesu akamwambia, “Mtu yeyote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.”
Jesus answered him, "No one who has put his hand to the plough, and then looks behind him, is fit for the Kingdom of God.

< Luka 9 >