< Luka 8 >

1 Baada ya haya Yesu alikwenda, akawa anazunguka katika miji na vijiji akihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walikuwa pamoja naye,
Pagamaliki ago Yesu akahamba mumiji na muhijiji hingi kuvajovela vandu Lilovi la Bwina la Unkosi wa Chapanga. Vawuliwa vaki kumi na vavili vakalongosana nayu.
2 pia baadhi ya wanawake waliokuwa wametolewa pepo wachafu na kuponywa magonjwa. Miongoni mwao alikuwepo Maria Magdalene, aliyetolewa pepo wachafu saba;
Pamonga na vadala vevawusiwi mizuka na vevalamisiwi matamu na Yesu, venavo vavi, Maliya mkolonjinji wa Magidala mweawusiwi mizuka saba yihakau,
3 Yoana mkewe Kuza, msimamizi wa nyumba ya watu wa nyumbani mwa Herode; Susana; na wengine wengi waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
na Yoana mdala waki Kuza, Kuza mweavi myimilila nyumba ya Helodi, Susana na vadala vangi vamahele. Vevawusili vindu yavi ndava ya kumtangatila Yesu na vawuliwa vaki vayendelela na lihengu lavi.
4 Umati mkubwa wa watu ulipokuwa ukija kwa Yesu kutoka kila mji, akawaambia mfano huu:
Vandu vamahele vambwelalili Yesu kuhuma kukila muji, na msambi uvaha pawakonganiki, Yesu akavajovela luhumu ulu.
5 “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia; zikakanyagwa, nao ndege wa angani wakazila.
Mundu mweahambili kumija mbeyu zaki. Na peamija mbeyu, zingi zikagwilila munjila na vandu vakazilivatila, na videge vikahola.
6 Mbegu nyingine zilianguka penye miamba, nazo zilipoota, hiyo mimea ikakauka kwa kukosa unyevu.
Zingi zikagwilila paludaka luna maganga pezatumbulayi kumela zikanyala muni pavi lepi na manji.
7 Nazo mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo ile miiba ikakua pamoja nazo, na kuisonga hiyo mimea.
Zingi zikagwilila muminga, ndi minga zikamela pamonga nazu, zikazihinya.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri. Zikaota na kuzaa mara mia moja zaidi ya mbegu alizopanda.” Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti, akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
Zingi zagwili paludaka lwabwina, zikamela limonga likapambika ng'onyo. Yesu akamalisila kwa lwami luvaha, “Mweavi na makutu ga kuyuwana ayuwana!”
9 Wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano huo.
Vawuliwa vaki vakamkota Yesu, luhumu lula mana yaki kyani.
10 Naye akasema, “Ninyi mmepewa kufahamu siri za Ufalme wa Mungu, lakini kwa wengine nazungumza kwa mifano, ili, “‘ingawa wanatazama, wasione; ingawa wanasikiliza, wasielewe.’
Mwene akavayangula, “Nyenye muhotiswi kumanya ufiyu wa Unkosi wa Chapanga, nambu lepi kwa avo vangi, vene vijoviwa kwa luhumu, muni vakalolayi nakuhotola kulola na vakayuwana nakumanya.”
11 “Maana ya mfano huu ni hii: Mbegu ni neno la Mungu.
“Luhumu ulu mana yaki. Mbeyu ndi lilovi la Chapanga.
12 Zile zilizoanguka kando ya njia ni wale ambao husikia neno, naye ibilisi anakuja na kuliondoa neno kutoka mioyoni mwao, ili wasije wakaamini na kuokoka.
Chechihumili kwa mbeyu zezagwili munjila, ndi luhumu lwa vandu veviyuwana lilovi la Chapanga, kangi Setani peibwela na kuliwusa mumitima yavi vakotoka kusadika na kusanguliwa.
13 Zile mbegu zilizoanguka kwenye mwamba ni wale ambao hulipokea neno kwa furaha wanapolisikia, lakini hawana mizizi. Wanaamini kwa muda mfupi, lakini wakati wa kujaribiwa huiacha imani.
Mewawa chechehumili kwa mbeyu zezagwili pamaganga, ndi luhumu wa vandu veviyuwana lilovi na kulipokela kwa luheku. Nambu vandu vangali mikiga mugati yavi, na lukumbi pevilingiwa vikotoka.
14 Zile mbegu zilizoanguka kwenye miiba ni mfano wa wale wanaosikia, lakini wanapoendelea husongwa na masumbufu ya maisha haya, utajiri na anasa, nao hawakui.
Kangi chechihumili kwa mbeyu zezagwili paminga, ndi luhumu wa vandu veviyuwana lilovi la Chapanga, pa lukumbi luhupi peviyendelela na Lilovi lenilo, vene vihinyiwa na mahengu ga kuvya na vindu vyamahele na mambu ga bwina ga pamulima, ndi na kupambika matunda gakakangala.
15 Lakini zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo mzuri ni mfano wa wale ambao hulisikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mnyofu wa utiifu, nao kwa kuvumilia kwingi huzaa matunda.
Ndi mbeyu zezagwili paludaka lwabwina, ndi luhumu wa vandu vevayuwini lilovi na kulivika mumitima yavi na kuyidakila bwina. Vikangamala mumitima mbaka kupambika matunda.”
16 “Hakuna mtu awashaye taa na kuificha ndani ya gudulia au kuiweka mvunguni mwa kitanda. Badala yake, huiweka juu ya kinara, ili wale waingiao ndani waone mwanga.
“Vandu vipambika lepi hahi na kuyigubika na chiviga amala kuyivika kuhi kuchitanda. Nambu vandu vivika hahi panani pachibokoselu, muni vandu veviyingila mugati valola bwina.”
17 Kwa maana hakuna jambo lolote lililofichika ambalo halitafichuliwa, wala lolote lililositirika ambalo halitajulikana na kuwekwa wazi.
“Muni chochoha chechifiyiki, yati chigubukuliwa na chindu chochoha cha mfiyu yati chimanyikana na voha.”
18 Kwa hiyo, kuweni waangalifu mnavyosikia. Kwa maana yeyote aliye na kitu atapewa zaidi. Lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani anacho atanyangʼanywa.”
“Mujiyangalilayi chemwiyuwana, muni mweavi nachu yati iyonjokeswa, nambu mundu mwanga chindu, hati chila chidebe cheihololela kuvya nachu yati chinyagiwa.”
19 Wakati mmoja mama yake Yesu na ndugu zake walikuja kumwona, lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya msongamano wa watu.
Nyina waki na valongo vaki Yesu vakamuhambalila, ndava ya msambi wa vandu wula nakuhotola kumuhegelela.
20 Mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje wanataka kukuona.”
Mundu mmonga akamjovela Yesu, “Nyina waku na valongo vaku vayimili kuvala, vigana kukulola.”
21 Yesu akamjibu, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wote wanaolisikia neno la Mungu na kulifanya.”
Nambu Yesu akavajovela vandu, “Nyina wangu na valongo vangu ndi vala veviyuwana lilovi la Chapanga na kulikamula.”
22 Siku moja Yesu alipanda ndani ya mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo ya ziwa.” Nao wakaondoka.
Na kavili ligono limonga Yesu peakweli muwatu pamonga na vawuliwa vaki, akavajovela, “Tikupuka kumwambu ya nyanja.” Vakatumbula kukupuka.
23 Hivyo walipokuwa wakienda, akalala usingizi. Dhoruba kali ikatokea mle ziwani, hata mashua ikawa inajaa maji, nao walikuwa katika hatari kubwa.
Pavahambayi muwatu wula, Yesu agonili lugono. Ndi chimbungululu chikatumbula kutova munyanja mula na manji gakatumbula kuyingila muwatu wavi mkulemala neju.
24 Wanafunzi wake wakamwendea na kumwamsha, wakisema, “Bwana, Bwana, tunaangamia!” Yeye akaamka, akaukemea ule upepo na yale mawimbi; dhoruba ikakoma, nako kukawa shwari.
Vawuliwa vaki vamhambali vakamuyumusa na vakamjovela, “Bambu, Bambu Tifwa!” Yesu akayumuka, akachilakalila chimbungululu chila na luyuga lwa manji ndi vikaguna na kukavya teke.
25 Akawauliza wanafunzi wake, “Imani yenu iko wapi?” Kwa woga na mshangao wakaulizana, “Huyu ni nani, ambaye anaamuru hata upepo na maji, navyo vikamtii?”
Kangi akavajovela vawuliwa vaki, “Kusadika kwinu kuvi koki?” Vene vakakangasa na kuyogopa kuni vijovelana, “Mundu uyu wa namuna yoki? Hati ihotola kugunisa chimbungululu na luyuga na vyene vimyidikila!”
26 Basi wakafika katika nchi ya Wagerasi, ambayo iko upande wa pili wa ziwa kutoka Galilaya.
Vakakupuka na kuhika kumbwani ya kumuji wa mulima wa Vagelasi wewalolasini na Galilaya kumwambu ya nyanja.
27 Yesu aliposhuka kutoka mashua na kukanyaga ufuoni, alikutana na mtu mmoja wa mji ule aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, naye kwa muda mrefu alikuwa havai nguo wala kuishi nyumbani, bali aliishi makaburini.
Yesu peahulwiki muwatu na kulivatila mbwani, mundu mmonga wa muji wula, mweavi na mizuka ambwelalili. Mundu mwenuyo kwa magono gamahele awala lepi nyula wala atamili lepi munyumba yoyoha yila, ndi atamali mumbugu la kuzikila vandu.
28 Alipomwona Yesu, alipiga kelele, akajitupa chini mbele yake na kusema kwa sauti kuu, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Nakuomba, usinitese!”
Peamuweni Yesu akavemba kwa lwami luvaha na kumgwilila pamagendelu, “Wa, Yesu veve Mwana wa Chapanga Mkulu! Una kyani na nene? Pepayi chonde kotoka kuning'aha!”
29 Wakati huo Yesu alikuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke huyo mtu. Mara nyingi huyo pepo mchafu alimpagaa, na hata alipofungwa kwa minyororo mikono na miguu na kuwekwa chini ya ulinzi, alikata hiyo minyororo na kupelekwa na huyo pepo mchafu kwenda nyikani.
Ajovili genago muni Yesu amali kuuhakalila mzuka wula umuwukayi mundu yula. Pamahele mzuka wamzangila mundu yula pamonga na vandu kumuvika mugati na kumkunga minyololo mu mawoko na mumagendelu nambu pamahele adenyayi vifungo vyenivyo, na kujumbiswa kwa makakala ga mzuka wenuwo mbaka kulugangatu.
30 Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Legioni,” kwa kuwa alikuwa ameingiwa na pepo wachafu wengi mno.
Yesu akamkota, “Liina laku yani?” Akayangula, “Liina langu Msambi.” Ndava mizuka yamahele yamuyingili.
31 Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda katika Shimo. (Abyssos g12)
Mizuka yila yikamjovela Yesu pepayi chonde akotoka kuyipeleka kuligodi langali mwishu. (Abyssos g12)
32 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe hapo likilisha kando ya kilima. Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu awaruhusu wawaingie hao nguruwe, naye akawaruhusu.
Kwavi na maguluvi gamahele gevadimayi kuchitumbi pandu penapo, ndi mizuka yila yikamuyupa Yesu yihamba kuyingila mumaguluvi gala. Yesu akayileka yihamba.
33 Wale pepo wachafu walipomtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nalo kundi lote likateremkia gengeni kwa kasi, likatumbukia ziwani na kuzama.
Ndi mizuka yila yikamuwuka mundu yula yikagayingila maguluvi gala, na msambi wa maguluvi ukahelela munyanja na kuyongomela, gakafwa mumanji.
34 Wale watu waliokuwa wakichunga lile kundi la nguruwe walipoona yaliyotukia, wakakimbia, wakaeneza habari hizi mjini na mashambani.
Vadimaji va maguluvi pevaloli gegahumali vakajumba, kuhamba kumuji na kumigunda kuvajovela vandu ujumbi.
35 Nao watu wakatoka kwenda kujionea wenyewe yaliyotukia. Walipofika hapo alipokuwa Yesu, wakamkuta yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu amekaa karibu na Yesu, akiwa amevaa nguo na mwenye akili timamu! Wakaogopa.
Vandu vakabwela kulola gegahumalili, vakamuhambalila Yesu, vamuwene mundu mwe yamuhumili mizuka yula, atamili papipi na magendelu ga Yesu, awali nyula, na avi na luhala lwaki bwina. Voha vakayogopa.
36 Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine jinsi yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu alivyoponywa.
Vandu vevagaweni mambu genago, vakavajovela vayavi chealamiswi mundu yula.
37 Ndipo watu wote wa nchi ile ya Wagerasi wakamwomba Yesu aondoke kwao, kwa sababu walikuwa wamejawa na hofu. Basi akaingia katika mashua, akaondoka zake.
Vakolonjinji voha wa ku Gelasi vakavya na wogohi neju. Vakamuyupa Yesu awukayi ahamba kungi. Yesu akakwela muwatu akawuka.
38 Yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu akamsihi Yesu afuatane naye, lakini Yesu akamuaga, akamwambia:
Mundu mweamuwusi mizuka yula, amuyupili Yesu valongosanayi. Nambu Yesu nakumuyidakila, ndi akamjovela,
39 “Rudi nyumbani ukawaeleze mambo makuu Mungu aliyokutendea.” Kwa hiyo yule mtu akaenda, akatangaza katika mji wote mambo makuu ambayo Yesu alimtendea.
“Wuya kunyumba yaku ukavajovelayi gaakuhengili Chapanga.” Ndi mundu yula akahamba kila pandu kumuji woha akuvajovela vandu chaamhengili Yesu.
40 Basi Yesu aliporudi, umati mkubwa wa watu ukampokea kwa furaha, kwani walikuwa wakimngojea.
Yesu paawuyili kumwambu yingi ya nyanja, avakoli msambi wa vandu vampokali chaluheku, ndava voha vamlindilayi.
41 Kisha mtu mmoja, jina lake Yairo, aliyekuwa kiongozi wa sinagogi, akaja na kuanguka miguuni mwa Yesu, akimwomba afike nyumbani kwake,
Penapo akabwela mundu mmonga liina laki Yailusi avi chilongosi wa nyumba ya kukonganekela akamfugamila Yesu mumagendelu, akamuyupa Yesu ahamba kunyumba yaki,
42 kwa kuwa binti yake wa pekee, mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa anakufa. Yesu alipokuwa akienda, umati wa watu ukamsonga sana.
muni msikana waki ngayuyoyo mmonga, wa miiyaka kumi na yivili avi mtamu papipi kufwa. Yesu avi mukuhamba, msambi wa vandu wavi kumuhinya kila upandi.
43 Katika umati huo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa na tatizo la kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Tena alikuwa amegharimia yote aliyokuwa nayo kwa ajili ya matibabu, wala hakuna yeyote aliyeweza kumponya.
Kwavi na mdala mmonga pagati ya msambi wula wa vandu, avi na utamu wa kuhuma ngasi miyaka kumi na yivili, amalili kuwusa vindu vyaki vyoha kuvapela valamisa, kawaka mweahotwili kumlamisa.
44 Huyo mwanamke akaja kwa nyuma ya Yesu na kugusa upindo wa vazi lake. Mara kutokwa damu kwake kukakoma.
Mdala yula akamlanda Yesu mumbele akapamisa lugunyilu lwa pahi lwa nyula ya Yesu. Bahapo akalama.
45 Yesu akauliza, “Ni nani aliyenigusa?” Watu wote walipokana, Petro akasema, “Bwana, huu umati wa watu unakusonga na kukusukuma kila upande.”
Yesu akajova, “Yani mweanipamisi?” Vandu vakajova, Kawaka mundu mwaakupamisi. Petili akajova, “Bambu msambi wa vandu vakutindili na kukuhinya!”
46 Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, kwa maana nimetambua kuwa nguvu zimenitoka.”
Nambu Yesu akajova, “Avili mundu mweanipamisi, muni nijiyuwini makakala ganihumili.”
47 Yule mwanamke alipofahamu ya kuwa hawezi kuendelea kujificha, alikuja akitetemeka, akaanguka miguuni mwa Yesu. Akaeleza mbele ya watu wote kwa nini alimgusa na jinsi alivyoponywa mara.
Mdala yula paajiloli nakuhotola kujifiha, akabwela kuni hivagaya akamfugamila Yesu mumagendelu. Akamjovela pavandu voha ndava ya kumpamisa Yesu na chaalami bahapo.
48 Basi Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
Yesu akamjovela, “Msikana wangu, kusadika kwaku kukulamisi, uhamba na uteke.”
49 Yesu alipokuwa bado anasema, akaja mtumishi kutoka nyumbani kwa Yairo, yule kiongozi wa sinagogi, kumwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Usiendelee kumsumbua Mwalimu.”
Yesu paavi akona ilongela, akabwela mundu kuhuma kunyumba ya Yailo, akamjovela Yailo, “Leka kumung'aha Muwula, mwana waku mwene afwili.”
50 Yesu aliposikia jambo hili, akamwambia Yairo, “Usiogope. Amini tu, naye binti yako atapona.”
Yesu peayuwini genago, akamjovela Yailo, “Kotoka kuyogopa, sadika ndu, yati ilama.”
51 Walipofika nyumbani kwa Yairo, hakumruhusu mtu yeyote aingie ndani naye isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, pamoja na baba na mama wa yule binti.
Peahikili panyumba pala, akavatola Petili na Yohani na Yakobo pamonga na dadi na nyina wa msikana yula akayingila nawu mugati, vandu vangi avalekili kuvala.
52 Wakati ule ule watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili ya huyo binti. Yesu akawaambia, “Acheni kulia. Huyu binti hajafa, ila amelala.”
Vandu voha vavembayi na malilu kwa lipyanda ndava ya mwana yula. Nambu Yesu akavajovela, “Mkotoka kuvemba, muni mwana uyu afwili lepi, agonili ndu.”
53 Wao wakamcheka kwa dharau, wakijua kuwa amekwisha kufa.
Voha vakamuheka, muni vamanyili kuvya mwana yula afwili.
54 Yesu akamshika yule binti mkono na kuita, “Binti, amka!”
Kangi Yesu akamkamula chiwoko mwana yula na kumkemela, “Mwana yimuka!”
55 Roho yake ikamrudia, naye akainuka mara moja. Akaamuru apewe kitu cha kula.
Mpungu waki ukamuwuyila, bahapo akayimuka. Yesu akavajovela mumpela chakulya.
56 Wazazi wake wakastaajabu sana, lakini Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote juu ya yale yaliyotukia.
Dadi na nyina wa mwana yula vakakangasa, Nambu Yesu akavajovela vakotoka kumjovela mundu yoyoha mambu gala gegahengiki.

< Luka 8 >