< Luka 7 >

1 Baada ya Yesu kumaliza kusema haya yote watu wakiwa wanamsikiliza, akaingia Kapernaumu.
After He had finished teaching all these things in the hearing of the people, He went into Capernaum.
2 Mtumishi wa jemadari mmoja wa Kirumi, ambaye bwana wake alimthamini sana, alikuwa mgonjwa sana karibu kufa.
Here the servant of a certain Captain, a man dear to his master, was ill and at the point of death;
3 Jemadari huyo aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee wa Kiyahudi kwake, wakamwomba aje kumponya mtumishi wa huyo jemadari.
and the Captain, hearing about Jesus, sent to Him some of the Jewish Elders, begging Him to come and restore his servant to health.
4 Wale wazee walipofika kwa Yesu, wakamsihi sana amsaidie yule jemadari wakisema, “Mtu huyu anastahili wewe umfanyie jambo hili,
And they, when they came to Jesus, earnestly entreated Him, pleading, "He deserves to have this favour granted him,
5 kwa sababu analipenda taifa letu tena ametujengea sinagogi.”
for he loves our nation, and at his own expense he built our synagogue for us."
6 Hivyo Yesu akaongozana nao, lakini alipokuwa hayuko mbali na nyumbani, yule jemadari akatuma rafiki zake kumwambia Yesu, “Bwana, usijisumbue, kwani mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu.
Then Jesus went with them. But when He was not far from the house, the Captain sent friends to Him with the message: "Sir, do not trouble to come. I am not worthy of having you come under my roof;
7 Ndiyo maana sikujiona hata ninastahili kuja kwako wewe. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona.
and therefore I did not deem myself worthy to come to you. Only speak the word, and let my young man be cured.
8 Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”
For I too am a man obedient to authority, and have soldiers under me; and I say to one, 'Go,' and he goes; to another, 'Come,' and he comes; and to my slave, 'Do this or that,' and he does it."
9 Yesu aliposikia maneno haya, alishangazwa naye sana. Akaugeukia ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akawaambia, “Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli.”
Jesus listened to the Captain's message and was astonished at him, and He turned and said to the crowd that followed Him, "I tell you that not even in Israel have I found faith like that."
10 Nao wale watu waliokuwa wametumwa kwa Yesu waliporudi nyumbani walimkuta yule mtumishi amepona.
And the friends who had been sent, on returning to the house, found the servant in perfect health.
11 Baadaye kidogo, Yesu alikwenda katika mji mmoja ulioitwa Naini. Nao wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu walikwenda pamoja naye.
Shortly afterwards He went to a town called Nain, attended by His disciples and a great crowd of people.
12 Alipokaribia lango la mji, alikutana na watu waliokuwa wamebeba maiti wakitoka nje ya mji. Huyu aliyekufa alikuwa mwana pekee wa mwanamke mjane. Umati mkubwa wa watu wa mji ule ulikuwa pamoja na huyo mwanamke.
And just as He reached the gate of the town, they happened to be bringing out for burial a dead man who was his mother's only son; and she was a widow; and a great number of the townspeople were with her.
13 Bwana Yesu alipomwona yule mjane, moyo wake ulimhurumia, akamwambia, “Usilie.”
The Lord saw her, was moved with pity for her, and said to her, "Do not weep."
14 Kisha akasogea mbele akaligusa lile jeneza na wale waliokuwa wamelibeba wakasimama kimya. Akasema, “Kijana, nakuambia inuka.”
Then He went close and touched the bier, and the bearers halted. "Young man," He said, "I command you, wake!"
15 Yule aliyekuwa amekufa akaketi akaanza kuongea, naye Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
The dead man sat up and began to speak; and He restored him to his mother.
16 Watu wote wakajawa na hofu ya Mungu, nao wakamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea miongoni mwetu, Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”
All were awe-struck, and they gave glory to God--some saying, "A Prophet, a great Prophet, has risen up among us." Others said, "God has not forgotten His People."
17 Habari hizi za mambo aliyoyafanya Yesu zikaenea Uyahudi wote na sehemu zote za jirani.
And the report of what Jesus had done spread through the whole of Judaea and in all the surrounding districts.
18 Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakamweleza Yohana mambo haya yote. Hivyo Yohana akawaita wanafunzi wake wawili
John's disciples brought him an account of all these things;
19 na kuwatuma kwa Bwana ili kumuuliza, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
so John called two of his disciples and sent them to the Lord. "Are you the Coming One?" he asked, "or is there another that we are to expect?"
20 Wale watu walipofika kwa Yesu wakamwambia, “Yohana Mbatizaji ametutuma tukuulize, ‘Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?’”
The men came to Jesus and said, "John the Baptist has sent us to you with this question: 'Are you the Coming One, or is there another that we are to expect?'"
21 Wakati huo huo, Yesu aliwaponya wengi waliokuwa na magonjwa, maradhi na pepo wachafu, na pia akawafungua vipofu wengi macho wakapata kuona.
He immediately cured many of diseases, severe pain, and evil spirits, and to many who were blind He gave the gift of sight.
22 Hivyo akawajibu wale wajumbe, “Rudini mkamwambie Yohana yote mnayoyaona na kuyasikia: Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa habari njema.
Then He answered the messengers, "Go and report to John what you have seen and heard. Blind men receive sight, the lame walk, lepers are purified, deaf persons hear, the dead are raised to life, the poor have the Good News proclaimed to them.
23 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
And blessed is every one who does not stumble and fall because of my claims."
24 Wajumbe wa Yohana walipoondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
When John's messengers were gone, He proceeded to say to the multitude concerning John, "What did you go out into the Desert to gaze at? A reed waving in the wind?
25 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari na kuishi maisha ya anasa wako katika majumba ya kifalme.
But what did you go out to see? A man wearing luxurious clothes? People who are gorgeously dressed and live in luxury are found in palaces.
26 Lakini mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
But what did you go out to see? A Prophet? Aye, I tell you, and far more than a Prophet.
27 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
John is the man about whom it is written, 'See, I am sending My messenger before thy face, and he shall make ready thy way before thee.'
28 Nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hakuna aliye mkuu kuliko Yohana. Lakini yeye aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko Yohana.”
"I tell you that among all of women born there is not one greater than John. Yet one who is of lower rank in the Kingdom of God is greater than he.
29 (Watu wote hata watoza ushuru waliposikia maneno ya Yesu, walikubali kwamba mpango wa Mungu ni haki, maana walikuwa wamebatizwa na Yohana.
And all the people, including the tax-gatherers, when they listened to him upheld the righteousness of God, by being baptized with John's baptism.
30 Lakini Mafarisayo na wataalamu wa sheria walikataa mpango wa Mungu kwao kwa kutokubali kubatizwa na Yohana.)
But the Pharisees and expounders of the Law have frustrated God's purpose as to their own lives, by refusing to be baptized.
31 Yesu akawauliza, “Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Wanafanana na nini?
"To what then shall I compare the men of the present generation, and what do they resemble?
32 Wao ni kama watoto waliokaa sokoni wakiitana wao kwa wao, wakisema: “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkulia.’
They are like children sitting in the public square and calling out to one another, 'We have played the flute to you, and you have not danced: we have sung dirges, and you have not shown sorrow.'
33 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali mkate wala hanywi divai, nanyi mkasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
For John the Baptist has come eating no bread and drinking no wine, and you say, 'He has a demon!'
34 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nanyi mnasema: ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’
The Son of Man has come eating and drinking, and you say, 'Look, there is a man who is overfond of eating and drinking--he is a friend of tax-gatherers and notorious sinners!'
35 Nayo hekima huthibitishwa kuwa kweli na watoto wake wote.”
But wisdom is justified by all who are truly wise."
36 Basi Farisayo mmoja alimwalika Yesu nyumbani kwake kwa chakula. Hivyo Yesu akaenda nyumbani mwa yule Farisayo na kukaa katika nafasi yake mezani.
Now one of the Pharisees repeatedly invited Him to a meal at his house; so He entered the house and reclined at the table.
37 Naye mwanamke mmoja kwenye ule mji, ambaye alikuwa mwenye dhambi, alipojua kwamba Yesu alikuwa akila chakula nyumbani kwa yule Farisayo, akaleta chupa ya marhamu yenye manukato.
And there was a woman in the town who was a notorious sinner. Having learnt that Jesus was at table in the Pharisee's house she brought a flask of perfume,
38 Yule mwanamke akasimama nyuma ya miguu ya Yesu akilia. Akailowanisha miguu yake kwa machozi yake, kisha akaifuta kwa nywele zake, akaibusu na kuimiminia manukato.
and, standing behind close to His feet, weeping, began to wet His feet with her tears; and with her hair she wiped the tears away again, while she lovingly kissed His feet and poured the perfume over them.
39 Yule Farisayo aliyemwalika Yesu alipoona yanayotendeka, akawaza moyoni mwake, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua kwamba ni nani anayemgusa, na kwamba yeye ni mwanamke wa namna gani, na ya kuwa huyu mwanamke ni mwenye dhambi.”
Noticing this, the Pharisee, His host, said to himself, "This man, if he were really a Prophet, would know who and what sort of person this woman is who is touching him--and would know that she is an immoral woman."
40 Yesu akanena akamwambia, “Simoni, nina jambo la kukuambia.” Simoni akajibu, “Mwalimu, sema.”
In answer to his thoughts Jesus said to him, "Simon, I have a word to say to you." "Rabbi, say on," he replied.
41 “Palikuwa na mtu mmoja aliyewakopesha watu wawili fedha: Mmoja alidaiwa dinari 500na mwingine dinari hamsini.
"There were once two men in debt to one money-lender," said Jesus; "one owed him five hundred shillings and the other fifty.
42 Wote wawili walipokuwa hawawezi kulipa, aliyafuta madeni yao wote wawili. Sasa ni yupi kati yao atakayempenda yule aliyewasamehe zaidi?”
But neither of them could pay anything; so he freely forgave them both. Tell me, then, which of them will love him most?"
43 Simoni akajibu, “Nadhani ni yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi.” Naye Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
"I suppose," replied Simon, "the one to whom he forgave most." "You have judged rightly," Jesus rejoined.
44 Kisha akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, “Je, unamwona mwanamke huyu? Nilipoingia nyumbani mwako, hukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini huyu ameninawisha miguu kwa machozi yake, na kunifuta kwa nywele zake.
Then turning towards the woman He said to Simon, "Do you see this woman? I came into your house: you gave me no water for my feet; but she has made my feet wet with her tears, and then wiped the tears away with her hair.
45 Hukunisalimu kwa busu, lakini huyu mwanamke hajaacha kuibusu miguu yangu tangu nilipoingia.
No kiss did you give me; but she from the moment I came in has not left off tenderly kissing my feet.
46 Hukunipaka mafuta kichwani mwangu, lakini yeye ameipaka miguu yangu manukato.
No oil did you pour even on my head; but she has poured perfume upon my feet.
47 Kwa hiyo, nakuambia, dhambi zake zilizokuwa nyingi zimesamehewa, kwani ameonyesha upendo mwingi. Lakini yule aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo.”
This is the reason why I tell you that her sins, her many sins, are forgiven--because she has loved much; but he who is forgiven little, loves little."
48 Kisha akamwambia yule mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa.”
And He said to her, "Your sins are forgiven."
49 Lakini wale waliokuwa wameketi pamoja naye chakulani wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani ambaye hata anasamehe dhambi?”
Then the other guests began to say to themselves, "Who can this man be who even forgives sins?"
50 Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”
But He said to the woman, "Your faith has cured you: go, and be at peace."

< Luka 7 >