< Luka 6 >

1 Ikawa siku moja ya Sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya nafaka, nao wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke ya nafaka, wakayafikicha kwa mikono yao na kula punje zake.
And it came to pass, on a Sabbath, that he was passing along through cornfields, and his disciples were plucking and eating the ears of corn, rubbing them with their hands.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya mambo yasiyo halali kufanywa siku ya Sabato?”
But, certain of the Pharisees, said—Why are ye doing what is not allowed on the Sabbath?
3 Yesu akawajibu, “Je, ninyi hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa?
And, making answer unto them, Jesus said—Have ye never read, even this, what David did when he hungered, he, and they who were with him—
4 Aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akaichukua na kuila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
How he entered into the house of God, and, the presence-bread, receiving, did eat, and gave to them who were with him, which it is not allowable to eat, save alone, to the priests?
5 Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
And he was saying to them—The Son of Man is, Lord of the Sabbath.
6 Ikawa siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia ndani ya sinagogi na akawa anafundisha. Huko palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
And it came to pass, on another Sabbath, that he entered into the synagogue, and was teaching, and there was a man there, and, his right hand, was withered.
7 Mafarisayo na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu. Kwa hivyo wakawa wanamwangalia sana ili waone kama ataponya katika siku ya Sabato.
Now the Scribes and the Pharisees were narrowly watching him, whether, on the Sabbath, he healeth, —that they might find whereof to accuse him.
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, hivyo akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka usimame mbele ya watu wote.” Hivyo yule mtu akainuka, akasimama mbele yao wote.
But, he, knew their reasonings, and said to the man who had the, withered, hand—Arise, and stand forward in the midst! And, arising, he stood forward.
9 Ndipo Yesu akawaambia wale walimu wa sheria na Mafarisayo, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya Sabato? Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
And Jesus said unto them—I ask you, whether it is allowed, on the Sabbath, to do good or to do harm, —life, to save, or, to destroy.
10 Akawatazama watu wote waliokuwepo, kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukaponywa kabisa.
And, looking round upon them all, he said unto him—Stretch forth thy hand! and, he, did so, and his hand was restored.
11 Wale wakuu wakakasirika sana, wakashauriana wao kwa wao ni nini watakachomtendea Yesu.
But, they, were filled with folly, and began conversing one with another, as to, what they might do with Jesus.
12 Ikawa katika siku hizo Yesu alikwenda mlimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.
And it came to pass, in these days, that he went forth into the mountain to pray, and was spending the night in the prayer-house of God.
13 Kulipopambazuka, akawaita wanafunzi wake, naye akachagua kumi na wawili, ambao pia aliwaita mitume:
And, when it became day, he called his disciples, and chose from them, twelve, whom also he named, Apostles, —
14 Simoni aliyemwita Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo,
Simon, whom also he named Peter, and Andrew his brother; and James and John; and Philip and Bartholomew;
15 Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni aliyeitwa Zelote,
and Matthew and Thomas; and James, son of Alphaeus, and Simon, who was called Zealot; and Judas, [son] of James,
16 Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote ambaye alikuwa msaliti.
and Judas Iscariot, who became betrayer; —
17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali penye uwanja tambarare. Hapo palikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu kutoka sehemu zote za Uyahudi, kutoka Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
and, coming down with them, he stood upon a level place, also a great multitude of his disciples, —and a great throng of the people, from all Judaea and Jerusalem and the sea-coast of Tyre and Zidon, who had come to hearken unto him and to be healed from their diseases;
18 Walikuwa wamekuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu akawaponya.
and, they who were molested by impure spirits, were being cured;
19 Watu wote walikuwa wanajitahidi kumgusa kwa sababu nguvu zilikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.
and, all the multitude, were seeking to touch him, because, power, from him, was coming forth, and healing all.
20 Akawatazama wanafunzi wake, akasema: “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa sababu Ufalme wa Mungu ni wenu.
And, he, lifting up his eyes towards his disciples, was saying: —Happy, ye destitute, for, yours, is the kingdom of God.
21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka.
Happy, ye that hunger now, for ye shall be filled. Happy, ye that weep now, for ye shall laugh.
22 Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia, watakapowatenga na kuwatukana na kulikataa jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
Happy, are ye, whensoever men shall hate you, and whensoever they shall separate you, and reproach you, and cast out your name as evil, for the sake of the Son of Man:
23 “Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.
be rejoiced in that day, and leap, for lo! your reward, is great in heaven; for, according to the same things, were their fathers doing unto the prophets.
24 “Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, kwa sababu mmekwisha kupokea faraja yenu.
But alas! for you, ye wealthy, for ye are duly receiving you consolation.
25 Ole wenu ninyi mlioshiba sasa, maana mtaona njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtaomboleza na kulia.
Alas! for you, ye who are filled full now, for ye shall hunger. Alas! ye that laugh now, for ye shall mourn and weep.
26 Ole wenu watu watakapowasifu, kwani ndivyo baba zao walivyowasifu manabii wa uongo.
Alas! whensoever all men shall, speak well of you, for, according to the same things, were their fathers doing unto the false prophets.
27 “Lakini nawaambia ninyi mnaonisikia: Wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia.
But, unto you, I say, who are hearkening: Be loving your enemies; be doing, good, unto them that hate you;
28 Wabarikini wale wanaowalaani, waombeeni wale wanaowatendea mabaya.
Be blessing them that curse you; be praying for them that wantonly insult you.
29 Kama mtu akikupiga shavu moja, mgeuzie na la pili pia. Mtu akikunyangʼanya koti lako, usimzuie kuchukua joho pia.
To him who is smiting thee upon the one cheek, be offering, the other also; and, from him who is taking away thy mantle, thy tunic also, do not forbid:
30 Mpe kila akuombaye, na kama mtu akichukua mali yako usitake akurudishie.
To every one asking thee, give, and, from him that taketh away thy possessions, ask them not back.
31 Watendeeni wengine kama ambavyo mngetaka wawatendee ninyi.
And, according as ye desire that men be doing unto you, be ye doing unto them, in like manner.
32 “Kama mkiwapenda tu wale wanaowapenda, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwapenda wale wawapendao.
And, if ye love them that love you, what sort of thanks are there for you? for, even sinners, love, such as love them.
33 Tena mkiwatendea mema wale tu wanaowatendea ninyi mema, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ hufanya vivyo hivyo.
[For], if ye even do good unto them that do good unto you, what sort of thanks are there for you? Even sinners, the same, are doing.
34 Tena mnapowakopesha wale tu mnaotegemea wawalipe, mwapata sifa gani? Hata ‘wenye dhambi’ huwakopesha ‘wenye dhambi’ wenzao wakitarajia kulipwa mali yao yote.
And, if ye lend to them from whom ye are hoping to receive, what sort of thanks are there for you? Even sinners, unto sinners, do lend, that they may receive back, as much.
35 Lakini wapendeni adui zenu, watendeeni mema, wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo thawabu yenu itakapokuwa kubwa, nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu Sana, kwa sababu yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na kwa wale waovu.
But love your enemies, and do good and lend, hoping for, nothing, back; and your reward shall be, great, and ye shall be sons of the Most High, —for, he, is, gracious, unto the ungrateful and wicked.
36 Kuweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
Become ye compassionate, according as, your Father, is, compassionate;
37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa. Msilaumu, nanyi hamtalaumiwa. Sameheni, nanyi mtasamehewa.
And do not judge, and in nowise shall ye be judged; and do not condemn, and in nowise shall ye be condemned; release, and ye shall be released;
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”
Give, and it shall be given unto you: good measure, pressed down, shaken together, running over, will they give into your lap; for, with what measure ye mete, shall it be measured back unto you.
39 Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu aweza kumwongoza kipofu? Je, wote wawili hawatatumbukia shimoni?
He spake, moreover, a parable also, unto them: Can, the blind, guide, the blind? will not, both, fall into, a ditch?
40 Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu wake, ila yule aliyehitimu aweza kuwa kama mwalimu wake.
A disciple is not above the teacher; but, when trained, every one shall be as his teacher.
41 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
But why beholdest thou the mote that is in the eye of thy brother, while, the beam that is in thine own eye, thou dost not consider?
42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, acha nitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako? Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
How canst thou say to thy brother—Brother! let me cast out the mote that is in thine eye, —thyself, the beam in thine own eye, not beholding? Hypocrite! cast out, first, the beam out of thine own eye, and, then, shalt thou see clearly, to cast out, the mote that is in the eye of thy brother.
43 “Hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
For a good tree doth not produce worthless fruit, neither again doth, a worthless tree, produce good fruit.
44 Kila mti hujulikana kwa matunda yake. Kwa maana watu hawachumi tini kwenye miiba, wala zabibu kwenye michongoma.
For, every tree, by its own fruit, becometh known. For not, of thorns, do they gather figs, neither, of a bramble-bush, do they gather, a bunch of grapes.
45 Vivyo hivyo mtu mwema hutoa mambo mema kutoka kwenye hazina ya moyo wake, naye mtu mwovu hutoa mambo maovu kutoka kwenye hazina ya moyo wake. Kwa kuwa mtu hunena kwa kinywa chake yale yaliyoujaza moyo wake.
The good man, out of the good treasure of the heart, bringeth forth that which is good; and, the wicked man, out of the wicked heart, bringeth forth that which is wicked; for, out of an overflowing of heart, speaketh, his mouth.
46 “Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamfanyi ninayowaambia?
And why call ye me, Lord! Lord! and not do the things that I say?
47 Nitawaonyesha jinsi alivyo mtu yule anayekuja kwangu na kusikia maneno yangu na kuyatenda.
Every one coming unto me, and hearkening unto my words, and doing them, I will suggest to you, whom he is like:
48 Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba, akachimba chini sana, na kuweka msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipokuja, maji ya ghafula yaliipiga ile nyumba, lakini haikutikisika, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
He is like unto a man building a house, who digged, and deepened, and laid a foundation upon the rock, —and, a flood, coming, the stream burst against that house, and was not strong enough to shake it, because it had been, well, built.
49 Lakini yeye anayesikia maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ikaanguka mara na kubomoka kabisa.”
But, he that hath heard and not done, is like unto a man having built a house upon the earth, without a foundation, —against which the stream burst, and, straightway, it fell in; and it came to pass, that, the crash of that house, was, great.

< Luka 6 >