< Luka 5 >

1 Siku moja Yesu alipokuwa amesimama karibu na Ziwa la Genesareti, watu wengi wakiwa wanasongana kumzunguka ili wapate kusikia neno la Mungu,
I stało się, gdy nań lud nalegał, aby słuchał słowa Bożego, że on stał podle jeziora Gienezaretskiego.
2 akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, zikiwa zimeachwa hapo na wavuvi waliokuwa wanaosha nyavu zao.
I ujrzał dwie łodzi stojące przy jeziorze; ale rybitwi wyszedłszy z nich, płukali sieci.
3 Akaingia katika mojawapo ya hizo mashua ambayo ilikuwa ya Simoni, akamwomba aisogeze ndani ya maji kidogo kutoka ufuoni. Kisha akaketi na kufundisha watu akiwa mle ndani ya mashua.
A wstąpiwszy w jedną z tych łodzi, która była Szymonowa, prosił go, aby maluczko odjechał od brzegu; a usiadłszy, uczył on lud z onej łodzi.
4 Alipomaliza kunena, akamwambia Simoni, “Sasa peleka mashua hadi kilindini kisha mshushe nyavu zenu mkavue samaki.”
A gdy przestał mówić, rzekł do Szymona: Zajedź na głębię, a zapuśćcie sieci wasze ku łowieniu.
5 Simoni akamjibu, “Bwana, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha na hatukuvua chochote. Lakini, kwa neno lako nitazishusha nyavu.”
A odpowiadając Szymon, rzekł mu: Mistrzu! przez całą noc robiąc, niceśmy nie pojmali, wszakże na słowo twoje zapuszczę sieć.
6 Nao walipozishusha nyavu zao, wakavua samaki wengi sana, nyavu zao zikajaa zikaanza kukatika.
A gdy to uczynili, zagarnęli ryb mnóstwo wielkie, tak że się rwała sieć ich.
7 Wakawaashiria wavuvi wenzao kwenye ile mashua nyingine ili waje kuwasaidia. Wakaja, wakajaza mashua zote mbili samaki hata zikaanza kuzama.
I skinęli na towarzysze, którzy byli w drugiej łodzi, aby przybywszy ratowali ich; i przybyli i napełnili obie łodzi, aż się zanurzały.
8 Simoni Petro alipoona haya yaliyotukia, alianguka miguuni mwa Yesu na kumwambia, “Bwana, ondoka kwangu. Mimi ni mtu mwenye dhambi!”
Co widząc Szymon Piotr, przypadł do kolan Jezusowych, mówiąc: Wynijdź ode mnie; bom jest człowiek grzeszny, Panie!
9 Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wameshangazwa sana na wingi wa samaki waliokuwa wamepata.
Albowiem go był strach ogarnął, i wszystkie, co z nim byli, z onego obłowu ryb, które byli zagarnęli.
10 Vivyo hivyo wenzake Simoni, yaani Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”
Także i Jakóba i Jana, syny Zebedeuszowe, którzy byli towarzysze Szymonowi. I rzekł Jezus do Szymona: Nie bój się; od tego czasu ludzi łowić będziesz.
11 Hivyo wakasogeza mashua zao mpaka ufuoni mwa bahari, wakaacha kila kitu na kumfuata.
A oni wyciągnąwszy łódź na brzeg, wszystko opuściwszy, poszli za nim.
12 Ikawa siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamjia. Alipomwona Yesu, alianguka chini mpaka uso wake ukagusa ardhi, akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.”
I stało się, gdy był w niektórem mieście, że oto był tam mąż pełen trądu, który ujrzawszy Jezusa, padł na twarz, i prosił go, mówiąc: Panie! jeźli chcesz, możesz mię oczyścić.
13 Yesu akanyoosha mkono wake, akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Na mara ukoma wake ukatakasika.
Tedy wyciągnąwszy Jezus rękę, dotknął się go, mówiąc: Chcę, bądź oczyszczony; i zaraz odszedł trąd od niego.
14 Yesu akamwagiza akisema, “Usimwambie mtu yeyote, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
I przykazał mu, aby tego nikomu nie powiadał: ale rzekł: Idź, a ukaż się kapłanowi, i ofiaruj za oczyszczenie twoje, tak jako rozkazał Mojżesz, na świadectwo przeciwko nim.
15 Lakini habari zake Yesu zikazidi sana kuenea kotekote kuliko wakati mwingine wowote. Makutano makubwa ya watu yalikuwa yakikusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
I rozchodziła się tem więcej powieść o nim; i schodziły się mnóstwa wielkie, aby go słuchały i uzdrowieni byli od niego od niemocy swoich.
16 Lakini mara kwa mara Yesu alijitenga nao ili kwenda mahali pa faragha kuomba.
Ale on odchodził na pustynią, i modlił się.
17 Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na walimu wa sheria, waliokuwa wametoka kila kijiji cha Galilaya na kutoka Uyahudi na Yerusalemu, walikuwa wameketi huko. Nao uweza wa Bwana ulikuwa juu yake kuponya wagonjwa.
I stało się dnia niektórego, że on nauczał, a siedzieli też tam i Faryzeuszowie i nauczyciele Zakonu, którzy się byli zeszli ze wszystkich miasteczek Galilejskich i Judzkich, i z Jeruzalemu; a moc Pańska przytomna była uzdrawianiu ich.
18 Wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwenye mkeka. Wakajaribu kumwingiza ndani ili wamweke mbele ya Yesu.
A oto mężowie nieśli na łożu człowieka powietrzem ruszonego, i szukali, jakoby go wnieść i postawić przed nim.
19 Walipokuwa hawawezi kufanya hivyo kwa sababu ya umati wa watu, wakapanda juu ya paa, wakaondoa baadhi ya matofali, wakamteremsha yule mgonjwa kwa mkeka wake hadi katikati ya ule umati pale mbele ya Yesu.
A gdy nie znaleźli, którędy by go wnieśli, dla ciżby, wstąpiwszy na dach, przez posowę spuścili go łożem w pośrodek przed Jezusa.
20 Yesu alipoiona imani yao, akamwambia yule mgonjwa, “Rafiki, dhambi zako zimesamehewa.”
Który ujrzawszy wiarę ich, rzekł mu: Człowiecze! odpuszczone są tobie grzechy twoje.
21 Mafarisayo na wale walimu wa sheria wakaanza kuuliza, “Ni nani mtu huyu anayesema maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
Tedy poczęli myślić nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie, mówiąc: Któż to jest, co mówi bluźnierstwa? Któż może odpuszczać grzechy, tylko sam Bóg.
22 Yesu akijua mawazo yao akawauliza, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
Ale Jezus poznawszy myśli ich, odpowiadając rzekł do nich: Cóż myślicie w sercach waszych?
23 Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
Cóż jest łatwiejszego, rzec: Odpuszczone są tobie grzechy twoje, czyli rzec: Wstań a chodź?
24 Lakini ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Akamwambia yule aliyepooza, “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
Ale iżbyście wiedzieli, że Syn człowieczy ma moc na ziemi odpuszczać grzechy, (rzekł powietrzem ruszonemu: ) Tobie mówię: Wstań, a wziąwszy na się łoże swoje, idź do domu twego.
25 Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua mkeka wake, akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu.
A on zarazem wstawszy przed nimi, wziąwszy na się to, na czem leżał, szedł do domu swego, wielbiąc Boga.
26 Kila mmoja akashangaa na kumtukuza Mungu. Wakajawa na hofu ya Mungu, wakasema, “Leo tumeona mambo ya ajabu.”
I zdumieli się wszyscy, i chwalili Boga, i napełnieni byli bojaźnią, mówiąc: Widzieliśmy dziś dziwne rzeczy.
27 Baada ya haya, Yesu alitoka na kumwona mtoza ushuru mmoja jina lake Lawi akiwa amekaa forodhani, mahali pake pa kutoza ushuru. Akamwambia, “Nifuate.”
A potem wyszedł i ujrzał celnika, imieniem Lewiego, siedzącego na cle, i rzekł mu: Pójdź za mną.
28 Naye Lawi akaacha kila kitu, akaondoka, akamfuata.
I opuścił wszystko, a wstawszy, szedł za nim.
29 Kisha Lawi akamfanyia Yesu karamu kubwa nyumbani kwake, nao umati mkubwa wa watoza ushuru na watu wengine walikuwa wakila pamoja nao.
I sprawił mu lewi ucztę wielką w domu swoim; a było wielkie zgromadzenie celników i innych, którzy z nim za stołem siedzieli.
30 Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wa dhehebu lao wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
Tedy szemrali nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie, mówiąc do uczniów jego: Przecz z celnikami i z grzesznikami jecie i pijecie?
31 Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.
A Jezus odpowiadając, rzekł do nich: Nie potrzebująć zdrowi lekarza, ale ci, co się źle mają;
32 Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.”
Nie przyszedłem, wzywać sprawiedliwych, ale grzesznych do pokuty.
33 Wakamwambia Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo mara kwa mara hufunga na kuomba, lakini wanafunzi wako wanaendelea kula na kunywa.”
A oni mu rzekli: Przecz uczniowie Janowi często poszczą i modlą się, także i Faryzejscy, a twoi jedzą i piją?
34 Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwafanya wageni wa bwana arusi kufunga wakati yuko pamoja nao?
A on im rzekł: Izali możecie uczynić, żeby synowie łożnicy małżeńskiej pościli, póki z nimi jest oblubieniec?
35 Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.”
Lecz przyjdą dni, gdy oblubieniec odjęty będzie od nich; tedy w one dni pościć będą.
36 Yesu akawapa mfano huu, akawaambia: “Hakuna mtu achanaye kiraka kutoka kwenye nguo mpya na kukishonea kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, atakuwa amechana nguo mpya, na kile kiraka hakitalingana na ile nguo iliyochakaa.
Powiedział im też podobieństwo: Iż żaden łaty z szaty nowej nie przyprawia do szaty wiotchej; bo inaczej to, co jest nowego, drze wiotche, a do wiotchego nie zgadza się łata z nowego.
37 Hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo yote itamwagika.
I nikt nie leje wina nowego w stare statki; bo inaczej wino młode rozsadzi statki, i samo wyciecze, i statki się popsują.
38 Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
Ale młode wino ma być wlewane w statki nowe; a tak oboje bywają zachowane.
39 Wala hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai ya zamani, bali husema, ‘Ile ya zamani ni nzuri zaidi.’”
A nikt, kto się napił starego, nie zaraz chce młodego; ale mówi: Lepsze jest stare.

< Luka 5 >