< Luka 4 >

1 Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan River and was led by the Spirit into the desert,
2 mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
where he was tempted by the devil for forty days. He didn't eat anything during that whole time, so at the end he was starving.
3 Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
The devil said to him, “If you are the Son of God, command this stone to become bread.”
4 Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
“It is written in Scripture, ‘You shall not live on bread alone,’” Jesus answered.
5 Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
The devil led him up to a high place, and in a rapid view showed him all the kingdoms of the world.
6 Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
Then the devil said to Jesus, “I will give you authority over all of them, and their glory. This authority has been given to me, and I can give it to anyone I want.
7 Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
Bow down and worship me and you can have it all.”
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
“It is written in Scripture, ‘You shall worship the Lord your God, and you shall serve only him,’” Jesus replied.
9 Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
The devil took Jesus to Jerusalem, set him on the top of the Temple, and told him, “If you are the Son of God, then jump!
10 kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
For it is written in Scripture, ‘He will order his angels to care for you,
11 nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
holding you up to protect you from stumbling over a stone.’”
12 Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
“It is written in Scripture, ‘You shall not tempt the Lord your God,’” Jesus replied.
13 Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
When the devil had completed all his temptations, he waited for another opportunity.
14 Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
Jesus returned to Galilee, full of the Spirit's power. News about him spread everywhere.
15 Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
Jesus taught in their synagogues, and everyone praised him.
16 Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
When he arrived in Nazareth, where he had grown up, he went to the synagogue on the Sabbath day as usual.
17 naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
The scroll of the prophet Isaiah was handed to him. Jesus unrolled the scroll and found the place where it's written:
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
“The Spirit of the Lord is upon me, for he has anointed me to announce good news to the destitute. He has sent me to proclaim that prisoners will be released, the blind will see, the oppressed will be freed,
19 na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
and to proclaim the time of the Lord's favor.”
20 Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
He rolled up the scroll and gave it back to the attendant. Then he sat down. Everybody in the synagogue was staring at him.
21 Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
“This Scripture you've just heard has been fulfilled today!” he told them.
22 Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
Everybody expressed their approval of him, amazed at the gracious words that came from his lips. “Isn't this Joseph's son?” they wondered.
23 Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
Jesus replied, “I'm sure you'll repeat this proverb to me, ‘Physician, heal yourself!’ and ask, ‘Why don't you do here in your own hometown what we heard you did in Capernaum?’
24 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
But I tell you the truth, no prophet is accepted in his hometown.
25 Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
I guarantee that there were many widows in Israel during the time of Elijah when there was a drought for three and a half years, causing a great famine throughout the country.
26 Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
Yet Elijah wasn't sent to any of them. He was sent to a widow in Zarephath in the region of Sidon!
27 Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
Even though there were many lepers in Israel in the time of Elisha, the only one who was healed was Naaman the Syrian!”
28 Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
When they heard this everyone in the synagogue became furious.
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
They jumped to their feet and threw him out of the town. Then they dragged him to the top of the hill on which the town was built in order to throw him off the cliff.
30 Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
But he walked right through them and went on his way.
31 Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
Jesus went down to Capernaum, a town in Galilee. On Sabbath he started teaching them.
32 Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
They were amazed at what he taught them for he spoke with authority.
33 Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
In the synagogue there was a man who was possessed by a demon. He cried out,
34 “Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
“So, what do you want with us, Jesus of Nazareth? Have you come to destroy us? I know who you are: God's Holy One!”
35 Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
Jesus interrupted him, saying. “Be quiet!” Then he ordered the demon, “Come out of him!” Throwing him to the ground right before them, the demon left the man without injuring him.
36 Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
They were all amazed and asked each other, “What is this teaching? With power and authority he orders evil spirits to leave—and they do!”
37 Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
News about Jesus spread throughout the nearby region.
38 Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
Leaving the synagogue, Jesus went to Simon's house. Simon's mother-in-law was sick with a high fever and those who were there asked Jesus to help.
39 Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
Jesus went and stood over her. He told the fever to leave her—which it did. She got up right away and prepared a meal for them.
40 Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
When the sun set, they brought to him all who were sick, suffering from various diseases. Jesus placed his hands on them, one after the other, and he healed them.
41 Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
Demons came out of many people, shouting, “You are the Son of God.” But Jesus stopped them and refused to let them speak because they knew he was the Christ.
42 Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
Early the following morning Jesus left to find some peace and quiet. But the crowds went out looking for him, and finally found him. They tried to stop him leaving because they did not want him to go.
43 Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
But he told them, “I have to go to other towns to tell them the good news of the kingdom of God too, because that is what I was sent to do.”
44 Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.
So Jesus went on traveling around, teaching the good news in the synagogues of Judea.

< Luka 4 >