< Luka 3 >

1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
У петнаестој години владања ћесара Тиверија, кад беше Понтије Пилат судија у Јудеји, и Ирод четворовласник у Галилеји, а Филип брат његов четворовласник у Итуреји и у трахонитској, и Лисанија четворовласник у Авилини,
2 nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
За поглавара свештеничких Ане и Кајафе, рече Бог Јовану сину Заријином у пустињи,
3 Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
И дође у сву околину јорданску проповедајући крштење покајања за опроштење греха;
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
Као што је написано у књизи речи пророка Исаије који говори: Глас оног што виче у пустињи: Приправите пут Господњи; поравните стазе Његове;
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
Све долине нека се испуне, и све горе и брегови нека се слегну; и шта је криво нека буде право, и храпави путеви нека буду глатки;
6 Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
И свако ће тело видети спасење Божије.
7 Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
Јован, пак, говораше људима који излажаху да их крсти: Породи аспидини! Ко вам каза да бежите од гнева који иде?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
Родите дакле родове достојне покајања, и не говорите у себи: Оца имамо Авраама; јер вам кажем да Бог може и од овог камења подигнути децу Аврааму.
9 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
Јер већ и секира стоји дрвету код корена; и свако дрво које добар род не рађа сече се и у огањ се баца.
10 Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
И питаху га људи говорећи: Шта ћемо дакле чинити?
11 Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
Он пак одговарајући рече им: Који има две хаљине нека да једну ономе који нема; и ко има хране нека чини тако.
12 Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
Дођоше пак и цариници да их крсти, и рекоше му: Учитељу! Шта ћемо чинити?
13 Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
А он им рече: Не тражите више него што вам је речено.
14 Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
Питаху га пак и војници говорећи: А ми шта ћемо чинити? И рече им: Никоме да не чините силе нити кога да опадате, и будите задовољни својом платом.
15 Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
А кад народ беше у сумњи и помишљаху сви у срцима својим за Јована: Да није он Христос?
16 Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Одговараше Јован свима говорећи: Ја вас крстим водом; али иде за мном јачи од мене, коме ја нисам достојан одрешити ремен на обући Његовој; Он ће вас крстити Духом Светим и огњем.
17 Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
Он има лопату у руци својој, и очистиће гумно своје, и скупиће пшеницу своју, а плеву ће сажећи огњем вечним.
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
И друго много којешта јавља народу и напомиња.
19 Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
Ирода пак четворовласника кораше Јован за Иродијаду, жену брата његовог, и за сва зла што учини Ирод;
20 Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
И сврх свега учини и то те затвори Јована у тамницу.
21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
А кад се крсти сав народ, и Исус пошто се крсти и мољаше се Богу, отвори се небо,
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
И сиђе на Њ Дух Свети у телесном облику као голуб, и чу се глас с неба говорећи: Ти си Син мој љубазни, Ти си по мојој вољи.
23 Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
И тај Исус имаше око тридесет година кад поче; и беше, као што се мишљаше, син Јосифа сина Илијиног,
24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
Сина Мататовог, сина Левијевог, сина Мелхијиног, сина Јенејевог, сина Јосифовог,
25 Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
Сина Мататијиног, сина Амосовог, сина Наумовог, сина Еслијиног, сина Нангејевог,
26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
Сина Маатовог, сина Мататијиног, сина Семејиног, сина Јосифовог, сина Јудиног,
27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
Сина Јоаниног, сина Рисиног, сина Зоровавељевог, сина Салатииловог, сина Ниријиног,
28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
Сина Мелхијиног, сина Адијиног, сина Косамовог, сина Ировог,
29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
Сина Јосијиног, сина Елијезеровог, сина Јоримовог, сина Мататовог, сина Левијевог,
30 Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
Сина Симеуновог, сина Јудиног, сина Јосифовог, сина Јонановог, сина Елијакимовог,
31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
Сина Мелејиног, сина Маинановог, сина Мататиног, сина Натановог, сина Давидовог,
32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
Сина Јесејевог, сина Овидовог, сина Воозовог, сина Салмоновог, сина Наасоновог,
33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
Сина Аминадавовог, сина Арамовог, сина Есромовог, сина Фаресовог, сина Јудиног,
34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
Сина Јаковљевог, сина Исаковог, сина Авраамовог, сина Тариног, сина Нахоровог,
35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
Сина Серуховог, сина Рагавовог, сина Фалековог, сина Еверовог, сина Салиног,
36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
Сина Каинановог, сина Арфаксадовог, сина Симовог, сина Нојевог, сина Ламеховог,
37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
Сина Матусаловог, сина Еноховог, сина Јаредовог, сина Малелеиловог, сина Каинановог,
38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.
Сина Еносовог, сина Ситовог, сина Адамовог, сина Божијег.

< Luka 3 >