< Luka 3 >

1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
Piecpadsmitā ķeizara Tiberijus valdīšanas gadā, kad Poncius Pilatus bija zemes valdītājs Jūdejā un Hērodus valdnieks Galilejā un Filips, viņa brālis, valdnieks Iturejā un Trakonites tiesā un Lizanijus valdnieks Abilenē,
2 nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
Apakš tiem augstiem priesteriem Annasa un Kajafasa, Dieva vārds notika uz Jāni, Zaharijas dēlu, tuksnesī.
3 Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
Un viņš gāja pa visu Jardānes apgabalu, sludinādams kristību uz atgriešanos no grēkiem par grēku piedošanu.
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
Itin kā rakstīts pravieša Jesajas grāmatā, kas saka: “Saucēja balss tuksnesī: “Sataisiet Tā Kunga ceļu, dariet līdzenas Viņa tekas.
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
Visas ielejas lai top pildītas, un visi kalni un pakalni lai top zemoti, un kas nelīdzens, lai top līdzens, un kas celmains, par staigājamu ceļu;
6 Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
Un visa miesa redzēs Tā Kunga pestīšanu.””
7 Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
Tāpēc viņš sacīja uz tiem ļaudīm, kas izgāja, ka no viņa tiktu kristīti: “Jūs odžu dzimums, kas jums ir rādījis izbēgt no nākamās dusmības?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
Tāpēc nesiet pienākamus atgriešanās augļus; un nesākat savā prātā sacīt: “Mums ir Ābrahāms par tēvu.” Jo Es jums saku, ka Dievs no šiem akmeņiem Ābrahāmam spēj bērnus radīt.
9 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
Jau arī cirvis kokiem pie saknes pielikts; tāpēc ikkatrs koks, kas nenes labus augļus, top nocirsts un ugunī iemests.”
10 Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
Un tie ļaudis tam jautāja un sacīja: “Ko tad mums būs darīt?”
11 Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
Viņš atbildēja un uz tiem sacīja: “Kam divi svārki, tas lai dod tam, kam nav; un kam ir barība, lai dara tāpat.”
12 Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
Bet arī muitnieki nāca, ka liktos kristīties, un uz to sacīja: “Mācītāj, ko mums būs darīt?”
13 Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
Un viņš uz tiem sacīja: “Neņemiet vairāk, nekā jums ir nospriests.”
14 Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
Bet arī karavīri tam jautāja un sacīja: “Ko tad mums būs darīt?” Un viņš uz tiem sacīja: “Nedariet nevienam pāri, neapmelojiet nevienu un esat mierā ar savu algu.”
15 Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
Bet tiem ļaudīm gaidot un visiem savā prātā par Jāni domājot, vai tas neesot Kristus,
16 Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Jānis visiem atbildēja sacīdams: “Es jūs gan kristīju ar ūdeni, bet Viens nāks, spēcīgāks, nekā es, Tam es neesmu cienīgs atraisīt Viņa kurpju siksnas. Tas jūs kristīs ar Svētu Garu un uguni;
17 Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
Tam vēteklis rokā, un Viņš tīrīs Savu klonu caur caurim un sakrās kviešus Savā klētī, bet pelavas sadedzinās ar neizdzēšamu uguni.”
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
Arī vēl daudz citu ko mācīdams, viņš pasludināja tiem ļaudīm prieka vēsti.
19 Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
Bet Hērodus, viens no tiem četriem valdniekiem, no viņa pārmācīts Hērodeijas, Filipa, sava brāļa, sievas dēļ, un visa ļauna dēļ, ko Hērodus bija darījis,
20 Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
Pie visa tā arī šo vēl darīja, ka Jāni ieslēdza cietumā.
21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
Un notikās, kad visi ļaudis tapa kristīti, un arī Jēzus bija kristīts un Dievu pielūdza, tad debesis atvērās,
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
Un Svētais Gars nolaidās uz Viņu redzamā ģīmī kā balodis; un balss atskanēja no debesīm sacīdama: “Tu esi Mans mīļais Dēls, pie Tevis Man ir labs prāts.”
23 Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
Un Viņš pats, Jēzus, bija trīsdesmitā gadā un bija pēc ļaužu domām Jāzepa dēls, tas bija Elus dēls,
24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
Tas Matata, tas Levja, tas Melkus, tas Janna, tas Jāzepa dēls,
25 Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
Tas Matatijas, tas Amosa, tas Naūma, tas Eslus, tas Nagaja dēls,
26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
Tas Maāta, tas Matatijas, tas Zemeja, tas Jāzepa, tas Jūdas dēls,
27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
Tas Jāņa, tas Rezas, tas Corobabeļa, tas Zalatiēļa, tas Nerus dēls,
28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
Tas Melķus, tas Addas, tas Kozama, tas Elmodama, tas Era dēls,
29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
Tas Jāzepa, tas Eliēcera, tas Jorema, tas Matata, tas Levja dēls,
30 Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
Tas Sīmeana, tas Jūdas, tas Jāzepa, tas Jonana, tas Eliaķima dēls,
31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
Tas Meleas, tas Menas, tas Matatas, tas Natana, tas Dāvida dēls,
32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
Tas Isajus, tas Obeda, tas Boasa, tas Zalmana, tas Nahšona dēls,
33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
Tas Aminadaba, tas Arama, tas Hecrona, tas Vāreca, tas Jūdas dēls,
34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
Tas Jēkaba, tas Īzaka, tas Ābrahāma, tas Tārus, tas Nahora dēls,
35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
Tas Serugs, tas Regus, tas Pelegs, tas Ēbera, tas Šalus dēls,
36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
Tas Kainana, tas Arvaksada, tas Zema, tas Noas, tas Lāmeha dēls,
37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
Tas Matuzalas, tas Enoha, tas Jareda, tas Mahalaleēla, tas Kainana dēls,
38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.
Tas Enosa, tas Seta, tas Ādama dēls, tas Dieva.

< Luka 3 >