< Luka 3 >

1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
In the fiftenthe yeer of the empire of Tiberie, the emperoure, whanne Pilat of Pounce gouernede Judee, and Eroude was prince of Galilee, and Filip, his brothir, was prince of Iturye, and of the cuntre of Tracon, and Lisanye was prince of Abilyn,
2 nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
vndir the princis of prestis Annas and Caifas, the word of the Lord was maad on Joon, the sone of Zacarie, in desert.
3 Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
And he cam in to al the cuntre of Jordan, and prechide baptym of penaunce in to remyssioun of synnes.
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
As it is wrytun in the book of the wordis of Isaye, the prophete, The voice of a crier in desert, Make ye redi the weie of the Lord, make ye hise pathis riyt.
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
Ech valey schal be fulfillid, and euery hil and litil hil schal be maad lowe; and schrewid thingis schulen ben in to dressid thingis, and scharp thingis in to pleyn weies;
6 Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
and euery fleisch schal se the heelthe of God.
7 Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
Therfor he seid to the puple, which wente out to be baptisid of hym, Kyndlyngis of eddris, who schewide to you to fle fro the wraththe to comynge?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
Therfor do ye worthi fruytis of penaunce, and bigynne ye not to seie, We han a fadir Abraham; for Y seie to you, that God is myyti to reise of these stoonys the sones of Abraham.
9 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
And now an axe is sett to the roote of the tree; and therfor euery tre that makith no good fruyt, schal be kit doun, and schal be cast in to the fier.
10 Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
And the puple axide hym, and seiden, What thanne schulen we do?
11 Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
He answeride, and seide to hem, He that hath twei cootis, yyue to hym that hath noon; and he that hath metis, do in lijk maner.
12 Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
And pupplicans camen to be baptisid; and thei seiden to hym, Maister, what schulen we do?
13 Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
And he seide to hem, Do ye no thing more, than that that is ordeyned to you.
14 Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
And knyytis axiden hym, and seiden, What schulen also we do? And he seide to hem, Smyte ye wrongfuli no man, nethir make ye fals chalenge, and be ye apayed with youre sowdis.
15 Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
Whanne al the puple gesside, and alle men thouyten in her hertis of Joon, lest perauenture he were Crist,
16 Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Joon answeride, and seide to alle men, Y baptize you in watir; but a stronger than Y schal come aftir me, of whom Y am not worthi to vnbynde the lace of his schoon; he schal baptize you in the Hooli Goost and fier.
17 Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
Whos `wynewyng tool in his hond, and he schal purge his floor of corn, and schal gadere the whete in to his berne; but the chaffis he schal brenne with fier vnquenchable.
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
And many othere thingis also he spak, and prechide to the puple. But Eroude tetrark, whanne he was blamed of Joon for Erodias,
19 Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
the wijf of his brother, and for alle the yuelis that Eroude dide,
20 Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
encreside this ouer alle, and schitte Joon in prisoun.
21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
And it was don, whanne al the puple was baptised, and whanne Jhesu was baptised, and preiede, heuene was openyd.
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
And the Hooli Goost cam doun in bodili licnesse, as a dowue on hym; and a vois was maad fro heuene, Thou art my derworth sone, in thee it hath plesid to me.
23 Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
And Jhesu hym silf was bigynninge as of thritti yeer, that he was gessid the sone of Joseph, which was of Heli,
24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
which was of Mathath, which was of Leuy, which was of Melchi, that was of Jamne,
25 Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
that was of Joseph, that was of Matatie, that was of Amos, that was of Naum, that was of Hely, that was of Nagge,
26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
that was of Mathath, that was of Matatie, that was of Semei, that was of Joseph, that was of Juda, that was of Johanna,
27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
that was of Resa, that was of Zorobabel, that was of Salatiel,
28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
that was of Neri, that was of Melchi, that was of Addi, that was of Cosan, that was of Elmadan, that was of Her,
29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
that was of Jhesu, that was of Eleasar, that was of Jorum, that was of Matath,
30 Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
that was of Leuy, that was of Symeon, that was of Juda, that was of Joseph, that was of Jona, that was of Eliachym,
31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
that was of Melca, that was of Menna, that of Mathatha, that was of Nathan,
32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
that was of Dauid, that was of Jesse, that was of Obeth, that was of Boz, that was of Salmon, that was of Nason,
33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
that was of Amynadab, that was of Aram, that was of Esrom, that was of Fares,
34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
that was of Judas, that was of Jacob, that was of Isaac, that was of Abraham, that was of Tare, that was of Nachor,
35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
that was of Seruth, that was of Ragau, that was of Faleth, that was of Heber,
36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
that was of Sale, that was of Chaynan, that was of Arfaxath, that was of Sem, that was of Noe, that was of Lameth,
37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
that was of Matussale, that was of Enok, that was of Jareth, that was of Malaliel, that was of Cainan, that was of Enos,
38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.
that was of Seth, that was of Adam, that was of God.

< Luka 3 >