< Luka 23 >

1 Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.
Ils se levèrent en masse, et conduisirent Jésus devant Pilate.
2 Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”
Ils se mirent à l'accuser, disant: «Nous avons trouvé cet homme qui poussait notre nation à la révolte, et qui défendait de payer le tribut à César, se prétendant lui-même Messie, Roi.»
3 Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”
Pilate l'interrogea, disant: «Tu es le roi des Juifs?» — «Tu le dis, » lui répondit Jésus.
4 Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”
Pilate dit aux principaux sacrificateurs et à la foule: «Je ne trouve rien de criminel en cet homme.»
5 Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”
Mais ils insistèrent, disant: «Il agite le peuple, en enseignant par toute la Judée, après avoir commencé par la Galilée, et être venu jusqu'ici.»
6 Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”
Pilate, entendant nommer la Galilée, demanda si cet homme était Galiléen;
7 Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.
et ayant appris qu'il était de la juridiction d'Hérode, il le renvoya à Hérode, qui était aussi à Jérusalem en ces jours-là.
8 Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
Hérode eut une grande joie de voir Jésus, car depuis longtemps il en avait le désir, parce qu'il avait entendu parler de lui, et qu'il espérait le voir faire quelque miracle.
9 Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.
Il lui adressa un grand nombre de questions, mais Jésus ne lui répondit rien.
10 Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
Or les principaux sacrificateurs et les scribes étaient là, qui l'accusaient avec véhémence;
11 Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.
mais Hérode avec sa garde le traita avec mépris: il le fit revêtir par dérision d'un magnifique manteau, et le renvoya à Pilate.
12 Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.
Le jour même, Pilate et Hérode devinrent amis, d'ennemis qu'ils étaient auparavant.
13 Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,
Pilate, ayant assemblé les principaux sacrificateurs, les sénateurs et le peuple, leur dit:
14 akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.
«Vous avez traduit devant moi cet homme, comme excitant le peuple à la révolte, et, après l'avoir interrogé en votre présence, je ne l'ai trouvé coupable d'aucun des crimes dont vous l'accusez.
15 Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.
Hérode non plus, car je vous ai renvoyés à lui, et, vous le voyez, cet homme n'a rien fait qui mérite la mort.
16 Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [
Je le relâcherai donc, après l'avoir fait châtier.»
17 Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]
[Or il était obligé à chaque fête de leur relâcher un prisonnier]
18 Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”
Mais ils crièrent tous à la fois: «Fais-le mourir! Relâche-nous Barabbas.»
19 (Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)
Ce Barabbas avait été mis en prison pour une sédition qui avait eu lieu dans la ville, et pour un meurtre.
20 Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
Pilate, qui désirait relâcher Jésus, les harangua donc de nouveau;
21 Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
mais ils répondirent par les cris de «crucifie-le! crucifie-le!»
22 Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
Il leur dit pour la troisième fois: «Quel mal a-t-il donc fait? Je n'ai rien trouvé en lui qui mérite la mort; je le relâcherai donc, après l'avoir fait châtier?»
23 Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
Mais ils insistèrent, demandant à grands cris qu'il fût crucifié, et leurs clameurs et celles des principaux sacrificateurs prévalurent,
24 Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
et Pilate prononça que ce qu'ils demandaient serait exécuté:
25 Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
il leur relâcha celui qui avait été mis en prison pour sédition et pour meurtre, et qu'ils réclamaient; et il leur abandonna Jésus.
26 Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.
Comme ils l'emmenaient au supplice, ils prirent un nommé Simon, de Cyrène, qui venait des champs, et ils le chargèrent de la croix, pour qu'il la portât derrière Jésus.
27 Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.
Or, Jésus était suivi d'une grande foule de peuple, et particulièrement de femmes qui se frappaient la poitrine et pleuraient sur lui.
28 Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.
Il se tourna vers elles, et leur dit: «Filles de Jérusalem, ne pleurez pas sur moi, mais pleurez sur vous-mêmes et sur vos enfants;
29 Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’
car les temps viennent où l’on dira: «Heureuses les stériles! Heureux le sein qui n'a point enfanté! Heureuses les mamelles qui n'ont point nourri!»
30 Ndipo “‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!”’
Alors on se mettra à dire aux montagnes: «Tombez sur nous; » et aux collines: «Couvrez-nous; »
31 Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”
car si l'on fait ces choses au bois vert, que fera-t-on au bois sec?»
32 Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.
Les soldats conduisaient en même temps deux malfaiteurs pour être mis à mort avec lui.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.
Quand ils furent arrivés au lieu appelé Calvaire, ils y crucifièrent Jésus, ainsi que les malfaiteurs, l'un à sa droite, l'autre à sa gauche;
34 Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.
et Jésus dit: «Père, pardonne-leur, car ils ne savent ce qu'ils font.» Ils se partagèrent ses vêtements en les tirant au sort.
35 Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
Le peuple était là qui regardait. Les sénateurs se moquaient et disaient: «Il en a sauvé d'autres, qu'il se sauve lui-même, s'il est le Messie, l'élu de Dieu.»
36 Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
Les soldats aussi, s'approchant pour lui présenter du vinaigre, le raillaient,
37 na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
et disaient: «Si tu es le roi des Juifs, sauve-toi toi-même.»
38 Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
Il y avait même une inscription au-dessus de sa tête, portant: «Celui-ci est le Roi des Juifs.»
39 Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
L'un des malfaiteurs pendus à la croix, l'injuriait, disant: «N'es-tu pas le Messie? Sauve-toi toi-même, et nous avec toi.»
40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
Mais l'autre le reprenait: «N'as-tu point de crainte de Dieu, toi qui subis le même jugement?
41 Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
Pour nous, c'est justice; car nous recevons la peine que nos crimes ont méritée; mais lui, il n'a rien fait de mal.»
42 Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
Et il dit à Jésus: «Souviens-toi de moi, quand tu seras dans ton règne.»
43 Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
Et Jésus répondit: «Je te dis en vérité, qu'aujourd'hui même tu seras avec moi dans le paradis.»
44 Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
Il était déjà environ la sixième heure, quand des ténèbres se répandirent sur tout le pays jusqu’à la neuvième heure.
45 kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
Le soleil pâlit; le voile du temple se déchira par le milieu;
46 Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
et Jésus s'écria d'une voix forte: «Père, je remets mon esprit entre tes mains.» En prononçant ces mots, il expira.
47 Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
Le centurion, témoin de ces événements, donna gloire à Dieu, disant: «Assurément cet homme était juste; »
48 Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
et les foules que ce spectacle avait attirées, voyant ce qui s'était passé, s'en retournaient toutes en se frappant la poitrine.
49 Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
Mais tous ceux qui connaissaient Jésus, et les femmes qui l'avaient suivi de Galilée, se tenaient là, à l'écart, regardant ce qui se passait.
50 Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
Il y avait un sénateur, nommé Joseph, homme droit et juste,
51 lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
qui ne s'était associé ni au dessein, ni aux actes des autres sénateurs; il était originaire d'Arimathée. ville des Juifs, et il attendait le royaume de Dieu.
52 Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
Il se rendit auprès de Pilate et lui demanda le corps de Jésus.
53 Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
Il le descendit de la croix, l'enveloppa d'un linceul, et le déposa dans un sépulcre taillé dans le roc, où personne n'avait encore été mis.
54 Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
C'était le jour de la préparation, et le sabbat allait commencer.
55 Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
Les femmes qui étaient venues de la Galilée avec Jésus, ayant accompagné Joseph, virent le sépulcre et la manière dont le corps de Jésus y fut placé,
56 Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.
puis, s'en étant retournées, elles préparèrent des aromates et des parfums.

< Luka 23 >