< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
Jésus, ayant levé les yeux, vit les riches qui mettaient leurs offrandes dans le tronc.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
Il vit aussi une femme, une veuve très pauvre, qui y mettait deux pites;
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
et il dit: «Je vous assure que cette pauvre veuve a mis plus que personne,
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
car tous les autres ont fait offrande à Dieu de leur superflu, tandis qu'elle a donné de son nécessaire, tout ce qu'elle avait pour vivre.
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
Comme quelques personnes parlaient du temple, des pierres magnifiques et des offrandes qui l'ornent, Jésus dit:
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
«Le temps viendra où, de tout ce que vous regardez là, il ne restera pierre sur pierre qui ne soit renversée.»
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
Ses disciples lui demandèrent: «Maître, quand sera-ce donc, et quel sera le signe précurseur de cet événement?»
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
Il dit: «Prenez garde de vous laisser séduire; car plusieurs viendront sous mon nom, disant: «C'est moi qui suis le Messie, et le temps est proche.» Ne vous attachez pas à eux.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
Quand vous entendrez parler de guerres et de troubles, ne vous alarmez pas; car il faut que cela arrive premièrement, mais la fin ne viendra pas de sitôt.»
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Alors il ajouta: «Une nation s'élèvera contre une nation, et un royaume contre un royaume;
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
il y aura de grands tremblements de terre, et çà et là des pestes et des famines; et il paraîtra dans le ciel d'effrayants phénomènes et de grands signes.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
Mais auparavant l’on se saisira de vous, et l’on vous persécutera: on vous traînera dans les synagogues et dans les prisons; on vous traduira devant les rois et les gouverneurs à cause de mon nom.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
Cela vous arrivera pour que vous me rendiez témoignage.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Mettez-vous donc bien dans l'esprit de ne point préparer de défense,
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
car je vous donnerai une parole et une sagesse, à laquelle tous vos adversaires ne pourront ni répondre, ni résister.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
Vous serez livrés même par vos pères et par vos mères, par vos frères, par vos parents et par vos amis; plusieurs d'entre vous seront mis à mort,
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
et vous serez haïs de tout le monde à cause de mon nom;
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
mais il ne se perdra pas un cheveu de votre tête:
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
par votre persévérance vous conquerrez vos âmes.»
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
«Lorsque vous verrez que Jérusalem va être investie par les armées, sachez que sa ruine est proche.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Alors que ceux qui sont en Judée s'enfuient aux montagnes; que ceux qui demeurent dans la ville en sortent, et que ceux qui demeurent dans les campagnes n'y entrent point;
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
parce que ce sont les temps où la justice va accomplir tout ce qui est écrit.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
Malheur aux femmes qui seront enceintes et à celles qui allaiteront en ce temps-là! car une grande calamité fondra sur le pays, et un grand châtiment sera, infligé à ce peuple:
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
les uns tomberont sous le tranchant de l'épée, les autres seront emmenés en esclavage parmi toutes les nations, et Jérusalem sera foulée par les Gentils, jusqu’à ce que les temps des Gentils soient accomplis.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
Et il y aura des signes extraordinaires dans le soleil, dans la lune et dans les étoiles; et sur la terre, on verra l'angoisse des nations troublées par le fracas de la mer et des flots,
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
et celle des hommes mourant de frayeur dans l'attente des événements qui menacent la terre; car les puissances des cieux seront ébranlées.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
Alors on verra le Fils de l'homme venir dans une nuée, revêtu d'une grande puissance et d'une grande gloire.»
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
Quand ces phénomènes commenceront à arriver redressez-vous et levez la tête, parce que votre délivrance approche.
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
Et il ajouta une parabole: «Voyez le figuier et tous les arbres:
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
dès qu'ils ont commencé à pousser, vous connaissez de vous-mêmes, en les voyant, que déjà l'été est proche;
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
de même, quand vous verrez ces événements se produire, sachez que le royaume de Dieu est proche.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
En vérité, je vous dis que cette génération ne passera point, que tous ces événements n'arrivent.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Le ciel et la terre passeront, mais mes paroles ne passeront point.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
Prenez garde à vous-mêmes; craignez que vos coeurs ne viennent à s'appesantir par les excès, par l'ivresse et par les soucis de la vie, et que ce jour ne fonde sur vous à l’improviste;
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
car il viendra, comme un filet, s'abattre sur tous ceux qui habitent sur la face de la terre.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Mais veillez, priant en tout temps, afin d'être jugés dignes d'échapper à tous ces malheurs à venir, et de trouver place devant le Fils de l'homme.»
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
Jésus passait ses journées dans le temple, à enseigner, et il s'en allait passer les nuits à la montagne appelée Bois d'oliviers;
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
et tout le peuple venait dès le matin vers lui, dans le temple, pour l'entendre.

< Luka 21 >