< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
He looked up and saw the rich people who were putting their gifts into the treasury.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
He saw a certain poor widow casting in two small brass coins.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
He said, “Truly I tell you, this poor widow put in more than all of them,
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
for all these put in gifts for God from their abundance, but she, out of her poverty, put in all that she had to live on.”
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
As some were talking about the temple and how it was decorated with beautiful stones and gifts, he said,
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
“As for these things which you see, the days will come in which there will not be left here one stone on another that will not be thrown down.”
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
They asked him, “Rabbi, so when will these things be? What is the sign that these things are about to happen?”
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
He said, “Watch out that you don’t get led astray, for many will come in my name, saying, ‘I am he,’ and, ‘The time is at hand.’ Therefore don’t follow them.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
When you hear of wars and disturbances, don’t be terrified, for these things must happen first, but the end won’t come immediately.”
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Then he said to them, “Nation will rise against nation, and kingdom against kingdom.
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
There will be great earthquakes, famines, and plagues in various places. There will be terrors and great signs from heaven.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
But before all these things, they will lay their hands on you and will persecute you, delivering you up to synagogues and prisons, bringing you before kings and governors for my name’s sake.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
It will turn out as a testimony for you.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Settle it therefore in your hearts not to meditate beforehand how to answer,
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
for I will give you a mouth and wisdom which all your adversaries will not be able to withstand or to contradict.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
You will be handed over even by parents, brothers, relatives, and friends. They will cause some of you to be put to death.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
You will be hated by all men for my name’s sake.
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
And not a hair of your head will perish.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
“By your endurance you will win your lives.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
“But when you see Jerusalem surrounded by armies, then know that its desolation is at hand.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Then let those who are in Judea flee to the mountains. Let those who are in the middle of her depart. Let those who are in the country not enter therein.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
For these are days of vengeance, that all things which are written may be fulfilled.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
Woe to those who are pregnant and to those who nurse infants in those days! For there will be great distress in the land and wrath to this people.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
They will fall by the edge of the sword, and will be led captive into all the nations. Jerusalem will be trampled down by the Gentiles until the times of the Gentiles are fulfilled.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
“There will be signs in the sun, moon, and stars; and on the earth anxiety of nations, in perplexity for the roaring of the sea and the waves;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
men fainting for fear and for expectation of the things which are coming on the world, for the powers of the heavens will be shaken.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
Then they will see the Son of Man coming in a cloud with power and great glory.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
But when these things begin to happen, look up and lift up your heads, because your redemption is near.”
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
He told them a parable. “See the fig tree and all the trees.
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
When they are already budding, you see it and know by your own selves that the summer is already near.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
Even so you also, when you see these things happening, know that God’s Kingdom is near.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Most certainly I tell you, this generation will not pass away until all things are accomplished.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Heaven and earth will pass away, but my words will by no means pass away.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
“So be careful, or your hearts will be loaded down with carousing, drunkenness, and cares of this life, and that day will come on you suddenly.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
For it will come like a snare on all those who dwell on the surface of all the earth.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Therefore be watchful all the time, praying that you may be counted worthy to escape all these things that will happen, and to stand before the Son of Man.”
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
Every day Yeshua was teaching in the temple, and every night he would go out and spend the night on the mountain that is called Olivet.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
All the people came early in the morning to him in the temple to hear him.

< Luka 21 >