< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
And looking up, He saw the rich casting their gifts into the treasury.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
And He also saw a certain poor widow, casting in thither two mites.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
And He said; Truly I say unto you, That this poor widow cast in more than all.
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
For they all of that which abounds unto them cast into the gifts of God: but she out of her scarcity cast in all her living which she had.
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
And certain ones speaking concerning the temple, that it was ornamented with beautiful stones and offerings, He said,
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
These things which you see, the days will come, in which stone will not be left upon stone, which shall not be thrown down.
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
And they asked Him, saying, Teacher, when then shall these things be? and what shall be the sign when these things may be about to come to pass?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
And He said, See that you are not deceived. For many will come in my name, saying, I am He; and The time is at hand: go ye not after them.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
And when ye may hear of wars and commotions, be not affrighted: for it behooveth these things first to take place; but the end is not immediately.
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Then He said to them, Nation shall rise up against nation, and kingdom against kingdom:
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
and there shall be great earthquakes, famines and pestilences in divers places; and there shall be great terrors and signs from heaven.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
And before all of these things, they will lay their hands on you, and persecute you, delivering you into their synagogues and prisons, led before kings and governors on account of my name.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
And it shall come to pass to you for a testimony.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
Place it in your hearts, not to premeditate your defense:
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
for I will give to you mouth and wisdom, which all who are opposed to you will not be able to gainsay nor resist.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
And you shall be delivered up also by your parents, and brothers, and relatives, and friends; and they will kill some of you.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
And you shall be hated by all, on account of my name:
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
and not a hair from your head shall perish.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
In your patience gain your souls.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
And when you may see Jerusalem shut up by the armies, then know that her desolation is nigh.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Then let those in Judea fly to the mountains; and let those in the midst of it depart out; and let not those in the country come into it.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
Because these are the days of vengeance, to fill up all things which have been written.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
But alas to those in gestation and nursing in those days! For there shall be great distress upon the earth, and wrath to this people.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
And they shall fall by the edge of the sword, and be led captive into all nations: and Jerusalem shall be trodden down by the Gentiles, until the times of the Gentiles may be fulfilled.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
And there will be signs in the sun and in the moon and in the stars; and commotion of the nations of the earth in their perplexity, the sea and the wave roaring;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
the souls of men failing from fear, and expectation of those things coming upon the world: for the powers of the heavens will be shaken.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
And then they will see the Son of man coming in a cloud with power and great glory.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
And these things beginning to take place, straighten up, and lift up your heads; because your redemption is nigh.
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
And He spoke a parable to them: Behold the fig-tree, and all the trees:
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
when they may already put forth, seeing, know for yourselves that summer is nigh.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
So you also, when you see these things take place, know that the kingdom of God is nigh.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Truly I say unto you, that this race may not pass away, until all these things shall be fulfilled.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
But heaven and earth shall pass away, but my word can not pass away.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
But take heed to yourselves, lest your hearts may be burdened with luxury, and drunkenness, and worldly cares, and that day may come on you unanticipated.
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
For as a lasso it will come upon all the people who are sitting down upon the face of the whole earth.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
Therefore watch, praying all the time, that you may be counted worthy to escape all these things which are about to come to pass, and to stand before the Son of man.
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
And He was teaching in the temple during the days; and during the nights going out, He was lodging in the mountain called Mount of Olives.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
And all the people gathered in the temple to hear Him.

< Luka 21 >